Chachasteven
JF-Expert Member
- Jul 4, 2014
- 1,878
- 1,849
Tittle: A confession of a mad man
Author: DIZASTA VINA
Jina lake silikumbuki kwa sababu sikumuuliza anaitwa nani. Lakini kwa sasa hivi nikitafakari, ninaweza kumbatiza jina la Malaika. Ndiyo! Malaika kwa sababu ya mionekano yake. Lazima nikiri nimeona wanawake wengi warembo wa kila rangi na kabila, lakini huyu, ninayemuita Malaika alikuwa ni wa kipekee sana. Aliyemuumba alikuwa amempendelea kwa kiwango cha ajabu. Kuuelezea uzuri wake utanichukua muda mrefu sana na bado nisitoe taswira kamili. Labda nikuulize mpenzi msomaji, Umewahi kupigwa shoti ya umeme ghafla? Kama hapana, basi uzuri wa Malaika ulikuwa na uwezo wa kumpiga shoti yeyote atakayemtazama. Kuna muda ninahisi hata wanawake wenzake walimuonea wivu au na wao walitamani wawe wanaume ili wamtongoze yeye!
Huyo ndiye Malaika. Na sasa hadithi ndefu kwa ufupi ni kwamba nilikutana naye juzi. Nilikuwa nimekaa kiwanja f'lanif'lani hapa mjini mida ya usiku kupiga mbili tatu. Na kusema kweli, lengo langu ninapotembelea viwanja sio kunywa bia. Nilikuwa nipo mawindoni. Nikiwa natupa macho huku na kule, akaja huyu msichana mrembo hadi mahala nilipokaa. Kilichotokea nilihisi shoti mwilini mwangu! Labda ni kipindi hiki nilichokuwa nimezubaa ndiyo aliniambia jina lake, ila sikumsikia. Kusema kweli sijui. Nilikuwa nimeduwaa mpaka aliponistua.
"Dude, Upo mbali sana kimawazo? Umeachwa?"
"Hapana." Nilimjibu.
"Naomba nikujoin," Hakusubiri jibu langu akawa amekaa pembeni yangu. "Kaka, nimekuangalia toka umeingia hapa ndani na kusema kweli ilikuwa ni kama naona pepo. Kama naiona nchi ya ahadi. Nimevutiwa na wewe."
Sikusema kitu. Nilihisi pengine pombe zilikuwa zinamuendesha, lakini kila alivyoendelea kuongea niligundua ana hisia f'lani ambazo hawezi kuzizuia. Ni wazi alikuwa tayari hata kunipa mchezo kwa usiku uleule.
"Kwani hauamini kwenye 'love in a first sight?" Alinikurupua kutoka kwenye mawazo yangu.
"Mbona una kasi ya jini?" Nilimuuliza.
Kabla hajanijibu akacheka. Tabasamu lake likanipa mshangao mwingine.
Akaanza kuongea baada ya ukimya kidogo, "Brother, wasiwasi wa nini?" Sauti yake sasa hivi ilikuwa laini na ya kuvutia. Au zilikuwa ni pombe nilizokunywa?
"Wewe ni handsome, na pia ni mpole. Mchizi kama wewe unahitaji manzi kama mimi." Aliendelea kuongea.
Nilimtazama na kusema kweli nilimstahili. Alikuwa na Summer body. Kiufupi alikuwa ni pisi kali ya kwenda! Na machoni nilimtamani sana, ila nafsi ndiyo ikawa inagoma.
Nikayarudisha macho yangu kwenye pombe yangu. Ghafla akanishika sikio na kuninong'oneza kimahaba. "Dude, I love you."
Akaanza kuniita majina kama Babes mara Boo huku akijitomasatomasa kwenye chuchu. Waungwana f'lani waliokuwa meza ya pembeni yetu nikawasikia wanaambiana nina juju!
"Naomba unibusu!" Aliniambia.
Mimi nikakataa. Angekuwa mtu mwingine hii bahati asingeiacha iteleze kwenye viganja vya mikono yake. Malaika akala mingo akanibusu kwenye shingo nikaguna tu. Hakuna mwitikio wowote! Ilimshangaza hata yeye! Nadhani hata shetani alishangaa pia.
"Umeoa?"
"No." Nilimjibu.
"Kwanini hunipendi?"
Nilimwangalia machoni halafu nikasema, "Dada, nakuonea huruma."
"Huruma ya nini? Au una vibinti bar?" Kabla sijajibu akaendelea, "Achana navyo ili niku-treat kama minister. Kwani hivi ninavyokupenda hadi nakufuata hauhisi raha. Nikubalie tuwe wote mbona hakuna ugumu. Au una UKIMWI unaogopa kuusambaza?"
Nikamwambia kwa sauti ya chini, "Sikia! Mimi nachinja watu nauza mioyo yao na figo."
Akacheka kwa mashauzi ya kinafki nafki. Ilikuwa wazi hakuamini kauli yangu. Na watu wengi ninapowaambia hivi huwa hawaamini. Sikushangaa!
Akatulia kidogo halafu akasema, "Au hauna kazi, huh! Hiyo mioyo na figo ukichinja unauza wapi?"
"Napigiwa simu za oda. Kuna watu wanahitaji hivi viuongo na huwa ninazisafirisha mpaka India."
Akacheka sana mpaka akaniegemea. Wakati kichwani ninajiambia '... Dada angejua kitachokwenda kumtokea, angebeba pochi yake angetembea.'
Nikamwambia, "Nenda nyumbani usigeuke nyuma. Kalale kesho uende ibadani ukatoe ushuhuda. Ninakupa nafasi ya kuishi uujuze umma ili ukaandike kumbukumbu umenusurika kufa."
"Sio mbaya nzi kufia kwenye kidonda. Nakupenda sana. Please niweke moyoni, na hata ukiwa muuaji n'tafurahi kufia mikononi mwako." Alinijibu.
Hakutaka kusikia mambo mengi. Kama ni bidhaa alikuwa amekwishalipia anasubiri huduma. Akanikaribia kisha akanibusu kimahaba tena shingoni.
"Do you have a car or some' brother?" Aliniuliza.
Alikuwa anataka kujua kama nina usafiri. Nikarudia kumwambia mimi muuaji akagoma. Akaniambia twende naye kwangu halafu akaniegemea kifuani ghafla. Ile nafsi ikanirudia tena. Nikajikuta najiambia kichwani '... Dada angejua kitachokwenda kumtokea, angebeba pochi yake angekwenda mbali.'
Baada ya ubishi nikajikokota naye tukazama kwenye Harrier yangu iliyokuwa maegeshoni. Safari kwenda nyumbani ikaanza. Tulitumia nusu saa barabarani na muda wote alikuwa anaongea kuhusu hisia zake kwangu.
Tulipofika nyumbani kwangu nikampa mvinyo wa baridi wa kiitalia. Kitu ambacho hakujua ni kwamba ndani ya glasi yake nilikuwa nimemuwekea Valium. Akapiga fundo kadhaa kisha akaweka glasi mezani. Muda wote nilikuwa namuangalia tu. Alitabasamu akasogea hadi jirani nilipokuwa nimekaa akaweka mkono wake begani kwangu.
"Honey, haujaniambia unafanya kazi gani?" Akaniuliza kiudadisi.
Nilinyanyuka nikamuonesha picha za mademu kama mia niliowachora. Zilimsisimua kwa kweli. Na nikuambie tu msomaji, Mimi ninajua kuchora sana.
"Baby, Wewe ni genius." Aliniambia.
"Niliowachora wote nishawachinja. Wewe ndiye unafuata!"
Akasema, "Baby, haupo serious. Anyways acha nikuoneshe kipaji changu pia"
Nilitulia kumtazama. Alianza kuniimbia wimbo. Mwanzo alikuwa anaimba vizuri, lakini maneno yakaanza kukata kama ishara ya kwamba dawa imeanza kumkolea. Alipozidiwa akaanguka nikampeleka mpaka chumbani.
Chumba chenyewe huwa sio cha kulala. Huwa hakuna kitanda ila meza tu. Nilimlaza mezani hapo kwa pozi f'lani la mvuto nikaanza kumchora. Kazi ya muda mrefu kidogo. Nilipomaliza nilimbusu kwenye paji la uso kisha nikatoa visu vitatu vikali na nyundo.
MWISHO.
As inspired by Dizasta Vina's song titled A confession of a mad man.
Author: DIZASTA VINA
Jina lake silikumbuki kwa sababu sikumuuliza anaitwa nani. Lakini kwa sasa hivi nikitafakari, ninaweza kumbatiza jina la Malaika. Ndiyo! Malaika kwa sababu ya mionekano yake. Lazima nikiri nimeona wanawake wengi warembo wa kila rangi na kabila, lakini huyu, ninayemuita Malaika alikuwa ni wa kipekee sana. Aliyemuumba alikuwa amempendelea kwa kiwango cha ajabu. Kuuelezea uzuri wake utanichukua muda mrefu sana na bado nisitoe taswira kamili. Labda nikuulize mpenzi msomaji, Umewahi kupigwa shoti ya umeme ghafla? Kama hapana, basi uzuri wa Malaika ulikuwa na uwezo wa kumpiga shoti yeyote atakayemtazama. Kuna muda ninahisi hata wanawake wenzake walimuonea wivu au na wao walitamani wawe wanaume ili wamtongoze yeye!
Huyo ndiye Malaika. Na sasa hadithi ndefu kwa ufupi ni kwamba nilikutana naye juzi. Nilikuwa nimekaa kiwanja f'lanif'lani hapa mjini mida ya usiku kupiga mbili tatu. Na kusema kweli, lengo langu ninapotembelea viwanja sio kunywa bia. Nilikuwa nipo mawindoni. Nikiwa natupa macho huku na kule, akaja huyu msichana mrembo hadi mahala nilipokaa. Kilichotokea nilihisi shoti mwilini mwangu! Labda ni kipindi hiki nilichokuwa nimezubaa ndiyo aliniambia jina lake, ila sikumsikia. Kusema kweli sijui. Nilikuwa nimeduwaa mpaka aliponistua.
"Dude, Upo mbali sana kimawazo? Umeachwa?"
"Hapana." Nilimjibu.
"Naomba nikujoin," Hakusubiri jibu langu akawa amekaa pembeni yangu. "Kaka, nimekuangalia toka umeingia hapa ndani na kusema kweli ilikuwa ni kama naona pepo. Kama naiona nchi ya ahadi. Nimevutiwa na wewe."
Sikusema kitu. Nilihisi pengine pombe zilikuwa zinamuendesha, lakini kila alivyoendelea kuongea niligundua ana hisia f'lani ambazo hawezi kuzizuia. Ni wazi alikuwa tayari hata kunipa mchezo kwa usiku uleule.
"Kwani hauamini kwenye 'love in a first sight?" Alinikurupua kutoka kwenye mawazo yangu.
"Mbona una kasi ya jini?" Nilimuuliza.
Kabla hajanijibu akacheka. Tabasamu lake likanipa mshangao mwingine.
Akaanza kuongea baada ya ukimya kidogo, "Brother, wasiwasi wa nini?" Sauti yake sasa hivi ilikuwa laini na ya kuvutia. Au zilikuwa ni pombe nilizokunywa?
"Wewe ni handsome, na pia ni mpole. Mchizi kama wewe unahitaji manzi kama mimi." Aliendelea kuongea.
Nilimtazama na kusema kweli nilimstahili. Alikuwa na Summer body. Kiufupi alikuwa ni pisi kali ya kwenda! Na machoni nilimtamani sana, ila nafsi ndiyo ikawa inagoma.
Nikayarudisha macho yangu kwenye pombe yangu. Ghafla akanishika sikio na kuninong'oneza kimahaba. "Dude, I love you."
Akaanza kuniita majina kama Babes mara Boo huku akijitomasatomasa kwenye chuchu. Waungwana f'lani waliokuwa meza ya pembeni yetu nikawasikia wanaambiana nina juju!
"Naomba unibusu!" Aliniambia.
Mimi nikakataa. Angekuwa mtu mwingine hii bahati asingeiacha iteleze kwenye viganja vya mikono yake. Malaika akala mingo akanibusu kwenye shingo nikaguna tu. Hakuna mwitikio wowote! Ilimshangaza hata yeye! Nadhani hata shetani alishangaa pia.
"Umeoa?"
"No." Nilimjibu.
"Kwanini hunipendi?"
Nilimwangalia machoni halafu nikasema, "Dada, nakuonea huruma."
"Huruma ya nini? Au una vibinti bar?" Kabla sijajibu akaendelea, "Achana navyo ili niku-treat kama minister. Kwani hivi ninavyokupenda hadi nakufuata hauhisi raha. Nikubalie tuwe wote mbona hakuna ugumu. Au una UKIMWI unaogopa kuusambaza?"
Nikamwambia kwa sauti ya chini, "Sikia! Mimi nachinja watu nauza mioyo yao na figo."
Akacheka kwa mashauzi ya kinafki nafki. Ilikuwa wazi hakuamini kauli yangu. Na watu wengi ninapowaambia hivi huwa hawaamini. Sikushangaa!
Akatulia kidogo halafu akasema, "Au hauna kazi, huh! Hiyo mioyo na figo ukichinja unauza wapi?"
"Napigiwa simu za oda. Kuna watu wanahitaji hivi viuongo na huwa ninazisafirisha mpaka India."
Akacheka sana mpaka akaniegemea. Wakati kichwani ninajiambia '... Dada angejua kitachokwenda kumtokea, angebeba pochi yake angetembea.'
Nikamwambia, "Nenda nyumbani usigeuke nyuma. Kalale kesho uende ibadani ukatoe ushuhuda. Ninakupa nafasi ya kuishi uujuze umma ili ukaandike kumbukumbu umenusurika kufa."
"Sio mbaya nzi kufia kwenye kidonda. Nakupenda sana. Please niweke moyoni, na hata ukiwa muuaji n'tafurahi kufia mikononi mwako." Alinijibu.
Hakutaka kusikia mambo mengi. Kama ni bidhaa alikuwa amekwishalipia anasubiri huduma. Akanikaribia kisha akanibusu kimahaba tena shingoni.
"Do you have a car or some' brother?" Aliniuliza.
Alikuwa anataka kujua kama nina usafiri. Nikarudia kumwambia mimi muuaji akagoma. Akaniambia twende naye kwangu halafu akaniegemea kifuani ghafla. Ile nafsi ikanirudia tena. Nikajikuta najiambia kichwani '... Dada angejua kitachokwenda kumtokea, angebeba pochi yake angekwenda mbali.'
Baada ya ubishi nikajikokota naye tukazama kwenye Harrier yangu iliyokuwa maegeshoni. Safari kwenda nyumbani ikaanza. Tulitumia nusu saa barabarani na muda wote alikuwa anaongea kuhusu hisia zake kwangu.
Tulipofika nyumbani kwangu nikampa mvinyo wa baridi wa kiitalia. Kitu ambacho hakujua ni kwamba ndani ya glasi yake nilikuwa nimemuwekea Valium. Akapiga fundo kadhaa kisha akaweka glasi mezani. Muda wote nilikuwa namuangalia tu. Alitabasamu akasogea hadi jirani nilipokuwa nimekaa akaweka mkono wake begani kwangu.
"Honey, haujaniambia unafanya kazi gani?" Akaniuliza kiudadisi.
Nilinyanyuka nikamuonesha picha za mademu kama mia niliowachora. Zilimsisimua kwa kweli. Na nikuambie tu msomaji, Mimi ninajua kuchora sana.
"Baby, Wewe ni genius." Aliniambia.
"Niliowachora wote nishawachinja. Wewe ndiye unafuata!"
Akasema, "Baby, haupo serious. Anyways acha nikuoneshe kipaji changu pia"
Nilitulia kumtazama. Alianza kuniimbia wimbo. Mwanzo alikuwa anaimba vizuri, lakini maneno yakaanza kukata kama ishara ya kwamba dawa imeanza kumkolea. Alipozidiwa akaanguka nikampeleka mpaka chumbani.
Chumba chenyewe huwa sio cha kulala. Huwa hakuna kitanda ila meza tu. Nilimlaza mezani hapo kwa pozi f'lani la mvuto nikaanza kumchora. Kazi ya muda mrefu kidogo. Nilipomaliza nilimbusu kwenye paji la uso kisha nikatoa visu vitatu vikali na nyundo.
MWISHO.
As inspired by Dizasta Vina's song titled A confession of a mad man.