Habari na Picha: Kinana alipokutana uso kwa uso na Mh. Shibuda jukwaani Meatu

Na Said Mwishehe, Simiyu

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrhaman Kinana amesema wanasiasa ni watu hatari, kwani wengi wao wapo tayari kuona watu wanakufa kwa ajili ya wao kutaka madaraka.


Amesema zipo nchi nyingi ambazo zimeingia kwenye machafuko na mamia ya watu kupoteza maisha kwa sababu tu ya kusukumwa na baadhi ya wanasiasa ambao siku zote wanawaza mambo binafsi zaidi.


Akizungumza juzi katika ziara yake ya kwanza katika Mkoa wa Simiyu baada ya kumaliza ziara mkoani Shinyanga, Kinana alisema kuna wanasiasa wapo tayari kuona watu wanapoteza maisha ili tu wao waingie kwenye madaraka.


“Wanasiasa ni watu hatari. Wapo tayari watu wafe wao wapate madaraka na kisha wakiwa kwenye nafasi wanachofanya ni kutoa pole kwa waliopoteza ndugu zao na jamaa zao.


“Wanagawana vyeo wakati waliopoteza roho zao hawapo duniani. Hii si sawa lazima Watanzania muwe makini na wanasiasa wenye uchu wa madaraka na wapo tayari kuwatanguliza watu kufa ili wao wafikie malengo yao,” alisema Kinana.


Alitoa mifano ya nchi jirani ya Kenya, ambapo watu zaidi ya 800 wa nchi hiyo walipoteza maisha baada ya kufanyika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo mwaka 2008, lakini waliosababisha wakaamua kugawana vyeo.



“Kuna nchi nyingi ambazo zimeingia kwenye machafuko na watu kupoteza maisha kwa sababu tu kuna msukumo wa wanasiasa wenye malengo yao binafsi.


“Wanahamasisha watu wanaingia mtaani kuandamana, lakini mwisho wake wanaokufa, kupoteza viungo vya mwili na kujeruhiwa ni wananchi ambao walikubali kushawishiwa.


“Ikifika wakati wa kugawana vyeo wananchi walioingia kwenye maandamano hawapo tena na badala yake wanasiasa wanakaa na kuanza kugawana vyeo. Viongozi wanasema ni mipango ya Mungu. Waswahili wanasema akili za kuambiwa changanya na zako,” alisema Kinana.


Akizungumzia zaidi katika hilo, alisema ni jambo jema kwa Watanzania kutambua kuna wanasiasa ambao hawana nia njema na nchi, hivyo wanakila sababu ya kuhakikisha amani na utulivu unapewa kipaumbele.


Kuhusu mchakato wa Katiba alisema ni vema ikapatikana, lakini haina maana kuwa ikipatikana basi kila Mtanzania atakuwa na maisha mazuri.


Wakati huo huo Kinana alisema CCM itahakikisha inaendelea kuwa karibu na mabalozi wa nyumba 10 kwani wanafanya kazi kubwa ya kujenga chama hicho.


Alisema CCM inao wajumbe milioni moja nchi nzima, na hao ndio msingi wa chama hicho kwani wanachama wapo kuanzia ngazi ya chini na si ngazi ya juu kwani huko hakuna wanachama.




Jambo Leo
Wanasiasa na si chama, wakiwemo wa CCM, CHADEMA, CUF, TLP na vyama vingine vyovyote. Ni kauli iliyjaa hekima na inapaswa kutathminiwa kwa makini. Huyu katibu Mkuu ndie aliyeonya hivi majuzi kuwa swala la serikali mbili au tatu litategemea maamuzi ya wananchi na serikali ya CCM itafuata maamuzi ya wananchi na si matakwa ya watu wachache, ingawa kijana alivyoingia jukwaani povu lilimtoka akiongea kinyume kabisa na katibu wake kusisitiza hakuna hoja ya serikali tatu. Sasa hapa ni kujipanga au kuchanganyana?
 
kitendo cha Shibuda kupanda jukwaani na kuhutubia mkutano wa hadhara na viongozi wa CCM. Nape na Kinana huko Meatu ni kidhibitisho tosha cha kumtoa chamani huyu mtu.

Inakuwaje mbunge wa Chadema kuhutubia mkutano wa CCM? I
ts time to chase him away!!
 
Nitashangaa sana kikngozi yeyote wa chadema kuanza kuangaika na shibuda kabisa na uzuri kila mtu anajua kuwa shibuda anapenda watu waseme kuhusu yeye hivyo hawezi kutulia kabisa na dawa yake ni kumuacha afanye atakavyo and time will tell.
kitendo cha Shibuda kupanda jukwaani na kuhutubia mkutano wa hadhara na viongozi wa CCM. Nape na Kinana huko Meatu ni kidhibitisho tosha cha kumtoa chamani huyu mtu.

Inakuwaje mbunge wa Chadema kuhutubia mkutano wa CCM? I
ts time to chase him away!!

Hakuna kupoteza muda kumjadili mjinga kama shibuda na hata uongozi wa chadema usitumie mudA kumjadi huyu. Na kumjadili shibuda nikupoteza muda na malengo ambayo yana manufaa kwa chama muda huu.

Shibuda ni wa kupuuzwa tuu.

Shibidu asitupotezee muda na malengo.
 
Shibuda ameishafukuzwa CHADEMA siku nyingi na yeye analijua hilo kwani hakuna palipo na mjadala wa mambo muhimu ya chama Shibuda uhusishwa na hii ni wazi kuwa kwa sasa ni Mbunge wa CCM kupitia CHADEMA.
 
Lakin kasema wazi siasa sio chuki wananchi wa meatu wanawajibu wa kuwaambia viongozi wa ccm juu ya matatizo yao
 
Pole mkuu shibuda habebwi na chadema anajibeba mwenyewe wala hamuogopi mtu yuko tayari kwa lolote hakuna pia haku wa kumfukuza.
 
Nilikuwa naangalia taarifa ya habari jioni, nimebahatika kuona mh. Shibuda amejitokeza kwenye mkutano waCCM nakuisaport kwa nguvu zote. Binafsi Sijamuelewa dhamira yake sijui anataka kurudi alikotoka. Akifuata usemi wa mcheza kwao hutunzwa. Kwa walio muelewa maoni yenu plz..
 
Kwa muujibu wa taarifa ya habari itv, nimena Shibuda akimpa tano Kinana, kwnye mkutano wa CCM. Binafsi nimeshindwa kujua dhamira yake. Au cdm hakukaliki tena?
 
Nawasikitikia ndugu zangu wasukuma, sijue mmemkosea nini Mungu mpaka kawapa kiongozi kama huyu! Ongezeni maombi
 
Shibuda hajavunja kanuni yoyote na ni haki yake kwa chochote anachofanya si ana utashi? ndiyo maana wakati alipotetewa na kina Lissu na Marando kwenye ile kesi yake na yule jamaa aliyempiga ngwala OCD, Shibuda alisema yuko tayari hata kuwa mfagiaji kwenye ofisi za CDM, lakini leo hayakumbuki hayo, ndivyo binadamu tulivyo.
 
Chadema kilishaishiwa sera bangi za akina sugu ndiyo kilichobaki.



-------- hata ukimuweka wapi atabaki kuwa -------- tu

RAIS MPYA akili yako na ya Shibuda hamna tofauti na wala hamchekani hivyo si ajabu kumcheka -------- mwenzio
 
Kwa CCM kila mwananchi ni ndugu. CCM hatuna mawazo na kauli za mwenzetu na adui.

CCM tunaamini kwamba:
(1) Binadamu wote ni sawa.
(2) Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake.
(3) Ujamaa na Kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru.

CCM hatuna mtu wa jimbo la kaskazini, kusini, nyanda za juu, mashariki n.k. CCM tuna Tanzania ambayo ni moja katika serikali mbili.

Haya ni maandishi tu hata kwenye Kanga yapo.
 
Huyu -------- siku zake zinahesabika na kamwe asitegemee tena kuwa mbunge maana anajia fika anachotumiwa kukifanya ni kuanzisha migogoro ndani ya Chadema lakini watu wenye busara kama Mh Mbowe na Dr Slaa wanaamua kumpuuza maana muda sio mrefu atakufa kifo cha kawaida kisiasa.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Mbunge wa CHADEMA jimbo la Maswa Magharibi Mh. John Shibuda wakati akizungumza katika mkutano wa hadhar CCM uliofanyika kwenye viwanja vya Meatu mjini Meatu, ambapo ameelezea kuwa Siasa siyo ugonvi na alikuja Meatu kwa sababu mbili tu Moja ilikuwa ni kukutana na Ndugu Kinana kwa ajili ya kujadiliana mambo mbalimbali juu ya tatizo la zao la Pamba kuhusu bei ya zao hilo na matatizo ya pembejeo kwa wakulima wa Wilaya hiyo, Akongeza kwamba jambo la pili ni kwamba Ndugu Abdulrahman Kinana ni rafiki yake wa muda mrefu kwani hata wakati wakisoma shule wote walisoma Moshi mkoani Kilimanjaro Abdulrahman Kinana akisoma Old Moshi Sekondari na John Shibuda Mwenyewe akisoma Moshi Technical, lakini pia akasema wakati alipokuwa akigombea ubunge wa Maswa Magharibi Kinana alimchangia shilingi Milioni moja “Siasa Siyo Matusi. Ni ushirikiano na kukosoana kwa hoja” amemaliza Shibuda. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza jambo katika mkutano huo huku Mbunge wa jimbo la Maswa Magharibi John Shibuda akimsiliza, kushoto anayetabasam ni Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Nape Nnauye. Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Nape Nnauye akizungumza katika mkutano huo kushoto ni John Shibuda Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi CHADEMA. Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Nape Nnauye akikumbatiana kwa furaha na John Shibuda Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi CHADEMA mara baada ya kupanda jukwaani katika viwanja vya Meatu mjini, kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishuhudia. Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi CHADEMA Mh John Shibuda akiwasili katika mkutano wa hadhara wa Chama cha Mapinduzi uliofanyika kwenye viwanja vya Meatu mjini Meatu leo huku vijana wa Chama chaCHADEMA wakimsindikiza.. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu8 Abdulrahman Kinana akiwahutubia wana Meatu katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo mjini Meatu. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu8 Abdulrahman Kinana akielekea jukwaani mara baada ya kusimikwa Chifu Kilabanya wa wasukuma wa Meatu Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipunga usinga juu mara baada ya kusimikwa Chifu Kilabanya wa Wasukuma wa Meatu katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Meatu. kulia ni Mayanga Kidoyayi Msaidizi wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Pascal Mabiti (Chifu Kishosha) kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu Dr Titus Kamani, Nape Nnauye Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi CCM na Fale Miungumale. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimikwa na Mzee Fale na mama Kwimba Tobongo katika kutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Meatu leo jioni aliyeshika kipaza sauti ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi CCM na kushoto ni Dr Titusi Kamani mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa mgolole mweusi kama ishara ya kusimikwa kuwa chifu Kilabanya wa wasukuma wa Meatu. Mlemavu Daud Deus akikabidhiwa baiskeli na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika kutano wa hadhara uliofanyika mjini Meatu Simiyu leo Baiskeli hiyo imetolewa na Salim mmoja wa wana CCM wa Meatu. Daud Deus akijaribu kuendesha baiskeli yake mara baada ya kukabidhiwa rasmi na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana leo Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi akizungumza na wanaMeatu katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Meatu leo mkoani Simiyu.

Hivi watu hao wote walialikwa na Shibuda kwa kushirikiana na CCM au CCM pekee au Shibuda pekee? Nahisi Shibuda aliwaambia ana mkutano na waliompigia kura!
 
Back
Top Bottom