Gwajima anaumwa nini??

Gwajima anaumwa nini??

somijo

Senior Member
Joined
Apr 14, 2012
Posts
110
Reaction score
47
Gwajima alivyoenda kituo cha police (kati) alikuwa mzima na alikuwa akitembea!! Lakini tukaambiwa kazimia ghafla, na akalazwa!! Sijawahi kusikia afya yake labda ana kisukari, shinikizo la damu au magonjwa sugu!! "Mwaweza kunithibitishia" lakini leo ameonyeshwa na anaonekana kupata maumivu makali na ya kuja na kutoweka?? Akiongea anaonekana kuwa mzima lakini baadaye ananyong'onyea tena?? What's wrong with this man?? Mwenye kujua kilichomkumba, na kinachomsumbua atuvye tafadhali!!
Chanzo; Chanel 10
 
basi kumbe anaweza kuwa na tatizo kubwa,nae anaparamia mno watu,atakwenda na maji,ooohoo
 
Tego la mke wa mtu hilo, ana kisukar ila chakushangaza wake za watu wampitie mbali
 
mungu wake si anafufua misukule atamponya na yeye
 
Jamani uzi unauliza kama kuna mtu ana uhakika wa tatizo la afya yake!! Jamii ijulishwe!! Huyu mtu ni kioo ya jamii
 
Back to where he belongs! Anadai aliwahi kuwa kwenye wheel chair miaka mingi! Kuna cha ajabu sasa?
 
Aliamuru malaika wakampige Pengo, naona wamemgeuka.

Alidhani anaamuru malaika, kumbe anaamuru mapepo yakamdhuru Pengo, yalipokuta Pengo ana ulinzi tosha utokanao na maombi ya wakristu hayo mapepo yakashindwa kumdhuru Pengo yakamrudia Gwajima....Na asipokuwa na adabu atapigwa na Mungu...na hilo pigo litakuwa kubwa kuliko hilo la kwanza.
 
Wakati mwingine Mungu hutaka kuonyesha nguvu zake kupitia mambo kama haya!
 
Kwa kifupi tu ni kwamba Mungu anathibitisha kuwa alichofanya Gwajima sio chema na wala sio cha kuiga. Gwajima ameshuswa chini mpaka mavumbini na amedhalilika na bado atadhalilika sana kwani hata Polisi haijamaliza kumhoji na tayari ana makosa tele ikiwa ni pamoja na kumiliki silaha bila sheria na kutaka kutumia silaha hiyo akiwa ICU.

Mengine tele yataibuka jinsi siku zinavyokwenda, watu watashangaa lakini wanaojua ukweli wanaelewa jinsi Mungu anavyofanya kazi yake na jinsi anavyoweza kutumia hali yoyote ile kumrekebisha mwanadamu.

Kama Gwajima anamwelewa Mungu wa kweli basi sasa asipoteze muda isipokuwa kutubu na kujinyenyekeza kwa Mungu vinginevyo yatamfika makubwa zaidi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom