- Source #1
- View Source #1
Wakuu nimekutana na hii sauti inadaiwa kuwa ni ya Gwajima akimjibu Msukuma na Muro.
- Tunachokijua
- Madai
Kuna kipande cha sauti kinachosambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikielezwa kuwa ni sauti ya Askofu Josephat Gwajima akiwajibu Mbunge wa Geita vijini Joseph Kasheku Msukuma na aliyewahi kuwa mkuu wa wilaya Jerry Muro.
Sauti hiyo imeambatanishwa na grafiki yenye nembo na kufanana na Millard ayo ikidaiwa kuwa ni ya Mei 26, 2025.
Uhalisia wa madai hayo
JamiiCheck imefuatilia taarifa hiyo na kubaini kuwa inapotosha kwani si ya Mei 26, 2025 kama inavyoelezwa. Ufuatiliaji kwa njia ya maneno muhimu (keywords search) yanayosikika katika kipande hiko cha video na kujiridhisha kuwa sauti hiyo ni Julai 24, 2016.
Ufuatiliaji umebaini kuwa sauti hiyo ilichapishwa katika mtandao wa Youtube unaojulikana kama Josephat Gwajima Rudisha TV mwezi Julai 24, 2016 na hadi kufikia wakati ripoti hii inaandaliwa video hiyo ilikuwa na watizamaji zaidi ya laki moja na elfu tisini na tano.
Sauti hiyo iliambatanishwa na ujumbe katika mtandao huo ikisomeka Gwajima amjibu Makamba 24/07/2016, aidha video hiyo ina urefu wa dakika 13:55 ambapo pamoja na maneno mengine alitamka maneno ambayo yamesambazwa tena Mei 26, 2025 na kudaiwa kuwa ni ya wakati huo.
Vyanzo mbalimbali viliripoti pia tukio hilo ikiwemo Tikisa media na Global publishers kupitia tovuti zao waliripoti taarifa hiyo ikiwa na vichwa vilivyosomeka “Gwajima amjibu katibu mkuu wa zamani wa CCM Yusuf Makamba”
Taarifa hizo zilieleza kuwa Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amemjibu katibu mkuu wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba aliyemtuhumu kuwa ni mwongo akisema leseni yake ni ya kuendesha magari makubwa na siyo vibajaji na maguta.
Akihubiri katika kanisa lake jana, Gwajima bila kutaja jina la Makamba, alisema: “Siwezi kushughulika na vigari vidogovidogo nyie mnanifahamu, mimi nina leseni ya kuendesha semi trailer …nadhani mmenielewa,” alisema huku waumini wake wakimshangilia