nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
IJUMAA, MEI 18, 2012
NA MAREGESI PAUL, DAR ES SALAAM
Amesema kuwa, pamoja na kwamba Dk. Magufuli ni kiongozi wa Serikali, amekuwa akitoa kauli zisizofaa katika jamii ambapo alitolea mfano kauli ya kuwataka wananchi wapige mbizi kama hawawezi kulipa nauli mpya ya Kivuko cha Kigamboni.
Guninita alitoa shutuma hizo mwanzoni mwa wiki Mjini Dodoma, alipokuwa akizungumza kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM.
Chanzo chetu kilichokuwa katika kikao hicho kilisema kuwa, Guninita alisema Dk. Magufuli alitakiwa kuwaomba radhi wakazi wa Dar es Salaam kwa kuwa, kauli ya kuwataka wapige mbizi ilikuwa ni ya kejeli ambayo haiwezi kukubalika kwa namna yoyote.
"Guninita alilazimika kumpasha Magufuli kwa sababu inaonekana hakuridhishwa na kauli alizozitoa kipindi kile wakati nauli ya Kivuko cha Kigamboni inapandishwa na wananchi wakaonyesha kulalamika.
"Alisema viongozi wengine wa Serikali wanafanya maamuzi kwa kiburi na kwamba maamuzi mengine yanapofanywa, huwa hakuna ushirikishwaji kwa baadhi ya viongozi, bali mtu anaamua kufanya kama anavyotaka kisha anatoa kauli za kijeuri.
"Akatolea mfano nauli ya kigamboni, akasema Magufuli alichukua uamuzi mbaya sana kupandisha nauli wakati akijua maisha ya watu ni ya shida na kibaya zaidi ni pale aliposhindwa kuwasikiliza hata wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, walipoanza kulalamikia ongezeko hilo.
"Akasema yeye alitarajia baada ya kauli ile ya Magufuli, Waziri Mkuu angemtaka awaombe radhi wananchi wa Dar es Salaam, lakini hilo halikufanyika, sasa akasema kuna haja kwa viongozi kubadilika kwa sababu kauli nyingine zinaleta taswira mbaya kwa Serikali," kilisema chanzo chetu.
Pamoja na mashambulizi hayo, chanzo chetu kilisema Guninita alizungumzia pia msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam. Alisema msongamano huo ni kero kwa wananchi na kwamba Serikali imekuwa ikiahidi kuutatua bila utekelezaji.
Pia chanzo hicho kilisema mwana CCM huyo aligusia uendelezaji wa Mji wa Kigamboni, ambapo alisema suala la fidia kwa wananchi limekuwa ni kero kwa sababu hawajalipwa fidia, ingawa Serikali imekuwa ikiahidi kufanya hivyo ili kuuendeleza mji huo.
Kuhusu mfumuko wa bei, chanzo chetu kilisema kuwa, Guninita alionyesha kutoridhishwa nao na kutaka Serikali ichukue hatua za haraka kukabiliana nao kwa kuwa unawavunja moyo wananchi.
Kikao hicho cha NEC kilimalizika mwanzoni mwa wiki hii, huku kikitawaliwa na vijembe mbalimbali kwa baadhi ya viongozi wa Serikali pamoja na viongozi wa ngazi za juu wa CCM.
Miongoni mwa waliotoa shutuma nzito katika kikao hicho ni kada wa chama hicho, Peter Kisumo, ambaye alimshambulia Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama kwa kile alichosema kuwa kiongozi huyo ni sehemu ya chanzo cha kudhoofika kwa chama hicho.
Kwa mujibu wa Kisumo, Mukama hana mikakati ya kukiinua chama na pia hajui kufanya tathmini kujua kama chama kimepanda hadhi au kimeshuka miongoni mwa jamii.
Wengine walioshusha makombora ni Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, ambaye alimshushia lawama Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwamba hana sababu ya kubaki madarakani wakati baadhi ya mawaziri wameng'olewa madarakani kutokana na kushindwa kuwajibika.
Alisema kwamba, baadhi ya mawaziri hao wametolewa kafara kwa sababu aliyetakiwa kuwajibika ni Waziri Mkuu, kwa kuwa madudu mengi yaliyofanywa na mawaziri yamefanywa akiwa madarakani.
Sambamba na huyo, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Yusuf Makamba, naye alimshutumu Waziri Mkuu na kusema mtu akiwa na shida, ni rahisi sana kuonana na Rais Jakaya Kikwete kuliko Waziri Mkuu. Katika hatua nyingine, Makamba alimrushia kombora, Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, kwamba anakiua chama hicho kwa kuwa amekigeuza na kuwa kama kampuni yake binafsi.
Wengine walioishambulia Serikali na Chama cha Mapinduzi ni Mbunge wa Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba, Mwenyekiti wa chama hicho, Mkoa wa Arusha, Onesmo ole Nangole, Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga na mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru.
NA MAREGESI PAUL, DAR ES SALAAM
MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, amesema Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli ana kauli za kibabe ambazo haziwezi kukubalika.Amesema kuwa, pamoja na kwamba Dk. Magufuli ni kiongozi wa Serikali, amekuwa akitoa kauli zisizofaa katika jamii ambapo alitolea mfano kauli ya kuwataka wananchi wapige mbizi kama hawawezi kulipa nauli mpya ya Kivuko cha Kigamboni.
Guninita alitoa shutuma hizo mwanzoni mwa wiki Mjini Dodoma, alipokuwa akizungumza kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM.
Chanzo chetu kilichokuwa katika kikao hicho kilisema kuwa, Guninita alisema Dk. Magufuli alitakiwa kuwaomba radhi wakazi wa Dar es Salaam kwa kuwa, kauli ya kuwataka wapige mbizi ilikuwa ni ya kejeli ambayo haiwezi kukubalika kwa namna yoyote.
"Guninita alilazimika kumpasha Magufuli kwa sababu inaonekana hakuridhishwa na kauli alizozitoa kipindi kile wakati nauli ya Kivuko cha Kigamboni inapandishwa na wananchi wakaonyesha kulalamika.
"Alisema viongozi wengine wa Serikali wanafanya maamuzi kwa kiburi na kwamba maamuzi mengine yanapofanywa, huwa hakuna ushirikishwaji kwa baadhi ya viongozi, bali mtu anaamua kufanya kama anavyotaka kisha anatoa kauli za kijeuri.
"Akatolea mfano nauli ya kigamboni, akasema Magufuli alichukua uamuzi mbaya sana kupandisha nauli wakati akijua maisha ya watu ni ya shida na kibaya zaidi ni pale aliposhindwa kuwasikiliza hata wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, walipoanza kulalamikia ongezeko hilo.
"Akasema yeye alitarajia baada ya kauli ile ya Magufuli, Waziri Mkuu angemtaka awaombe radhi wananchi wa Dar es Salaam, lakini hilo halikufanyika, sasa akasema kuna haja kwa viongozi kubadilika kwa sababu kauli nyingine zinaleta taswira mbaya kwa Serikali," kilisema chanzo chetu.
Pamoja na mashambulizi hayo, chanzo chetu kilisema Guninita alizungumzia pia msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam. Alisema msongamano huo ni kero kwa wananchi na kwamba Serikali imekuwa ikiahidi kuutatua bila utekelezaji.
Pia chanzo hicho kilisema mwana CCM huyo aligusia uendelezaji wa Mji wa Kigamboni, ambapo alisema suala la fidia kwa wananchi limekuwa ni kero kwa sababu hawajalipwa fidia, ingawa Serikali imekuwa ikiahidi kufanya hivyo ili kuuendeleza mji huo.
Kuhusu mfumuko wa bei, chanzo chetu kilisema kuwa, Guninita alionyesha kutoridhishwa nao na kutaka Serikali ichukue hatua za haraka kukabiliana nao kwa kuwa unawavunja moyo wananchi.
Kikao hicho cha NEC kilimalizika mwanzoni mwa wiki hii, huku kikitawaliwa na vijembe mbalimbali kwa baadhi ya viongozi wa Serikali pamoja na viongozi wa ngazi za juu wa CCM.
Miongoni mwa waliotoa shutuma nzito katika kikao hicho ni kada wa chama hicho, Peter Kisumo, ambaye alimshambulia Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama kwa kile alichosema kuwa kiongozi huyo ni sehemu ya chanzo cha kudhoofika kwa chama hicho.
Kwa mujibu wa Kisumo, Mukama hana mikakati ya kukiinua chama na pia hajui kufanya tathmini kujua kama chama kimepanda hadhi au kimeshuka miongoni mwa jamii.
Wengine walioshusha makombora ni Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, ambaye alimshushia lawama Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwamba hana sababu ya kubaki madarakani wakati baadhi ya mawaziri wameng'olewa madarakani kutokana na kushindwa kuwajibika.
Alisema kwamba, baadhi ya mawaziri hao wametolewa kafara kwa sababu aliyetakiwa kuwajibika ni Waziri Mkuu, kwa kuwa madudu mengi yaliyofanywa na mawaziri yamefanywa akiwa madarakani.
Sambamba na huyo, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Yusuf Makamba, naye alimshutumu Waziri Mkuu na kusema mtu akiwa na shida, ni rahisi sana kuonana na Rais Jakaya Kikwete kuliko Waziri Mkuu. Katika hatua nyingine, Makamba alimrushia kombora, Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, kwamba anakiua chama hicho kwa kuwa amekigeuza na kuwa kama kampuni yake binafsi.
Wengine walioishambulia Serikali na Chama cha Mapinduzi ni Mbunge wa Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba, Mwenyekiti wa chama hicho, Mkoa wa Arusha, Onesmo ole Nangole, Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga na mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru.