Gubu linavowatafuna wapinzani wa Liverpool

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,512
17,417
Ndani ya misimu minne ntashinda taji moja. Ndivyo Klopp alivowaambia waandishi wa habari misimu mitatu na nusu iliyopita. Jamier Ghalagher alimuonya Klopp kuwa siyo rahisi kihivyo na ni kosa kubwa sana kuahidi taji ndani ya misimu minne.

Alianza na mfumo wake wa gegen pressing kwa wachezaji plastic kama Sturidge alishindwa kabisa, wazito kama Benteke walikoma! Maumivu ya misuli yalishamiri ndani ya kikosi na madaktari wa viungo walimponda sana Klopp hata Ferguson alidiriki kusema hajawahi kuona tim ina press muda wote. Klopp alijibu kirahisi kuwa anahitaji msimu mmoja kuweka msingi wa utimamu wa mwili wa wachezaji wake.

Hakukurupuka kusajili kwa bei bali alianza kuingiza falsafa yake pole pole kwa wachezaji aliowakuta huku akiwauza wale walioshindwa na kuwaingiza wapya pole pole ndani ya timu. Hadi sasa ni wachezaji wanne tu wa kikosi cha kwanza aliowakuta wamebaki ndani ya kikosi na hata hivyo hawana uhakika wa kuanza kikosi cha kwanza. Adam Lallana, Jordan Henderson, Firmino na Origi ndiyo pekee waliobaki katika kikosi cha Klopp.

Ninapoandika huu ni msimu wa tatu na nusu kwa Klopp na ameshatwaa mataji makubwa matatu yaani UCL, FIFA CLUB W.CUP na UEFA SUPER CUP amezidi matarajio ya mashabiki wa Liverpool na sasa anaongoza ligi kwa point 13 akiwa na mchezo moja wa kiporo dhidi ya Westham.

Huyo ndiyo Klopp alietaka kuwageuza wasio na imani wawe na imani na timu yao, wakati sherehe zikishamiri mashabiki pinzani wamebaki na gubu mioyoni mwao huku wakisingizia teknolojia ya video eti inawabeba Liverpool. Wamesahau kuwa TAA amebadilishwa kuwa Kevin Debruyne, Robertson kawa Marcel Henderson kwa makelele n.k. Unathubutu vipi kusema liva inabebwa kwa VAR? hamuoni MANE, SALAH na FIRMINO wanavyofanya kazi yao? Hamuona Gini na Hendo wanavyokaba?

Hamuoni Origi alivo super sub? Acheni uchawi, Furahieni angalau mmebahatika kuona kikosi bora zaidi katika historia ya EPL. Liver hii inaenda kutawala EPL kwa miaka kumi.

Mashabiki pinzani mjilaumu wenyewe kwa tim zenu kufanya maamuzi ya hovyo!kwa mfano eti leo Ancelotti yupo Everton halafu man utd wamemkumbatia Ole wakati Massimiliano hana timu nyie mnampa Arteta timu, wakati Mourinho yupo Spurs. Chelsea eti ina Lampard. Huo ni uhuni ambao hata Masau Bwire hawezi kuufanya hapa Bongo.

Nawashauri furahieni maisha ya soka kwa kuishangilia Liverpool hii ya mabingwa ya Mjerumani JURGEN NOBERT KLOPP.

Liver.jpg
 
2015/2016 ilikuwa nusu msimu kwa hiyo huo msim haukukamilika wala hakusajili na kuandaa timu!!msim wake wa kwanza ni 2016~17,pili 2017~18,tatu 2018~2019 na huu 2019~20 nusu haujaisha!!kwa hiyo misim mitatu na nusu iliyokamilika hapo!!!umeelewa???

Zilikuwa zimecheza game ngapi? Ali-coach game ngapi za EPL msimu huo wa 2015/16?
 
Wewe hujui mpira, afu umeandika kishabiki sana. Eti utawale EPL kwa miaka kumi wakati uwezo wa kuchukua Back to back kama Pep huna.
 
alikochi kama gem 20 za EPL japo kikosi hakikuwa chake na wala hawakuwa na preseason pamoja!!!
Umipenda kitu unakua kipofu; Liverpool itatawaliwaje EPL kwa miaka kumi? yaani mwaka huu ndo wanachukua epl alafu mwakani nao unawapigia maesabu ya kuchukua EPL?

Uliona wapi timu yenye kikosi chembamba ikapata mafanikio kwa miaka minne mfululizo hapa duniani? nitajie; uwezi kutawala kama hauna back upa yenye uhakika wa kiwango kama cha Alison..Salah au Mane then ukatawala mpira.

Chukulia mpira kua wachezaji kama Salah, Mane, Alison na Van Divik wakosekane mechi nne mfululizo alafu uniambia hicho kikosi cha kushinda hizo mechi.
 
Umipenda kitu unakua kipofu; Liverpool itatawaliwaje epl kwa miaka kumi? yaani mwaka huu ndo wanachukua epl alafu mwakani nao unawapigia maesabu ya kuchukua epl?.

Uliona wapi timu yenye kikosi chembamba ikapata mafanikio kwa miaka minne mfululizo hapa duniani? nitajie; uwezi kutawala kama hauna back upa yenye uhakika wa kiwango kama cha Alison..Salah au Mane then ukatawala mpira.

Chukulia mpira kua wachezaji kama Salah..Mane...Alison na Van Divik wakosekane mechi nne mfululizo alafu uniambia hicho kikosi cha kushinda hizo mechi.

Liverpool hawajafungiwa kusajili tambua hilo.

Au kuna sehemu imesemwa Liverpool atatawala miaka mingi kwa kikosi hichihichi bila ya kusajili?
 
Embu twende sawa
October 2015 to October 2016-1
October 2016 to October 2017-2
October 2017 to October 2018-3
October 2018 to October 2019-4
Hakuna msimu unaoanza oktoba labda ligi ya mchangani!!msimu unaanza Agosti baada ya preseason na usajili!!!umenipata????
 
Tena kwa kuwasaidia msim2017/17-top four,2017/2018-top four na UCL final runners,2018/2019-UCL Winners and runners Epl,2019/2020-UCL supercup winners,Club world cup winners and Epl winners!!!Then 2020/21-Epl winners,UCL winners!!!Karibuni muendelee kutabiri mafanikio ya liverpool ndani ya miaka kumi ijayo!!!
 
Hakuna msimu unaoanza oktoba labda ligi ya mchangani!!msimu unaanza Agosti baada ya preseason na usajili!!!umenipata????
Mzee mbona haraka hivyo? Sizungumzii msimu nazungumzia muda aliokaa JK toka ajiunge na liver, au alijiunga mwezi wa8?
 
1. 2015 October ndo alijoin.

2. 2015/2016

3. 2016/2017

4. 2017/2018

5. 2018/2019

6. 2019/2020 Current season.

Unahesabu vipi misimu?
hii kauli klopp hakuisema 2015..aliisema mwanzo wa msimu wake mpya akiwa anaongezewa mkataba akasaini miaka 6 huku akiwa amekaa Liverpool kwa miezi kadhaa tu...alivyosign mwaka 2016 ndio akaahidi miaka 4 ya kujenga tim na atakua ameshinda taji ndani ya miaka hio
 
Back
Top Bottom