Habari zenu
Naitwa Chad
Ni mjasiriamali mwenye taaluma ya Mauzo na Masoko, CEO wa kampuni ya CHAD CREATION CO Ltd inajishughulisha na Real estate,
Nimeanzisha program ya kuwawezesha vijana kwa mawazo , na kwa na kwa vitendo katika kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.
Tayari vijana wapatao 6 0 wameshajiunga na tunahitaji vijana 100 ambao watakua katika makundi ya vijana 20 /20 na kuunda kampuni 5 za kwanza .
Kampuni hizi zitajishughulisha na kilimo cha biashara ambacho kitazingatia kanuni za kitaalamu toka uandaaji wa mashamba hadi masoko.
Kampuni hizi zitazalisha ajira, kipato,chakula, kukuza biashara, ushuru kwa serikali na kubadili fikra za vijana, pia kuongeza uzoefu wa kiongozi kwa vijana.
Kampuni hizi zitakua chini ya kampuni ya ushauri wenye wataalam wa kilimo, biashara,utafiti,sheria, bima nk ambayo itatoa miongozo muhimu kwa kampuni za vijana.
Kampuni hizi za vijana zitajishughulisha na kilimo cha mazao ya msimu mrefu, mfupi na ufugaji.
Wataalamu watawashauri kuanzia upimaji wa udongo, mbegu, mbolea, mifumo ya umwagiliaji, matumizi ya madawa ya kuua wadudu, uvunaji wa kisasa ,uhifadhi wa mazao na hatimae masoko ya uhakika.
Kampuni zitaongozwa na vijana wenyewe Kama watendaji hadi hapo zitakapo amua vinginevyo, ila chini ya uangalizi maalum kwa muda wa miaka 5 .
Katika mpango huu kampuni ya ushauri itazisaidia kampuni za vijana kutafuta mitaji toka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo.
Pia wanachama watapewa mafunzo ya taaluma mbalimbali kila mara ila kuwajengea uzoefu.
Mfumo wa kampuni hizi utatakuwa wa kumiliki hisa hivyo kila mmiliki atakuwa anamiliki hisa , hivyo kugawana faida na hasara kulingana na hisa. Wanachama wa kampuni hizi watasajiliwa na kutoa taarifa zao za msingi ikiwa ni pamoja na warithi wao.
Usajiri umeanza kwa kujiunga katika what's up group kwa namba 0762781778 na pia utatakiwa kutuma cv yako kwa email:
graduatehands@outlook.com.
Tutakuwa na vikao online kilasiku saa mbili usiku.
Tupo katika hatua za mwisho za usajiri hivyo tunahitaji vijana active sana Kama huna nafasi usishiriki.