GPS Katika Simu

Hope it`l work bro' let us know in case of anything!
 
ok thinkpad thats clear but Mimi natumia Tiigo na Simu ya N78 lakini GPS data inaonyesha hakuna Satellite data kabisa!!!!!What shall i do?

Kutumia tiGO sio tatizo mimi mwenyewe natumia tiGO na inafanya vizuri kabisa,
Usichanganye kitukimoja,
GPS inafanya kazi dirrect from simu to satelite,.....tigo au voda itaitajika kama utataka simu yako iwe inasend infornmation kwenye computer fulani au kwenye maping system software flani ndio utaitaita voda au tigo lakini kumbuka GPS inafanya vizuri ukiwa nje ya nyumba tena haitegemei mtandao wa simu.
N:B kama ukiwa unatumia google map kwenye simu na unategemea gps basi itabidi uwe na internent kwenye simu ambayo ni gprs ya voda ua tiGO ili iwe ina re-fresh location maaana ktk google map uki zooom inakuwa inafanya kama refreshing yaani inadownload map.

Kama simu yako haina gps download google map inafanya kazi vizuri sana yaani wakati mwingine inakuonyesha huko sehemu husika tena kwa mtandao wa voda au tiGO
 

Hamna mkuu inawezekana mawasiliano ya gps hayapitii voda wa tigo, ndio maaana yanakuwa mazuri kama utakuwa nje ya nyumba yako kuliko ndani, but kama ukiwa simu yako ina gps ila haina map ukawa unategemea map za kudownload basi itakubidi uwe na internent ili ukiwa enoa ukitaka kuliona gps itakupa lat na long then from downloaded map utajkiona upo wapi,

N:B tiGO ilikataa labda eneo ulilokuwepo gprs yao ni mfu maana tiGO kuna shida maeneomengine huwezipata net au locatuion ya mnara unaoutumia.
 

Hii kitu ipo hivi mimi nimeidownload nipo hapahapa bongo,

Inakupa eneo husika kabisa kama mtu akikwambia yupo kariakoo maeneo ya fire utajua yupo hayohayo maeneo ya fire kama yupo msimbazi utajua tu,

Yaani hii inategemea minara minara yote inasimikwa huku ikisetiwa na gps ilikuionyesha na kurahisisha ufatiliaji wake,

ukiwa kinondoni b itakuonyesha upo eneo hilo ukisogea morroco na yenyewe inasogea ukifika makumbusho na yenyewe inakuonyesha upo makumbusho au maeneo ya milenium tower.

Kwa tiGO inafanya hata voda pia ila voda ndio nzuri kidogo maana ina 3g.
 
Folks.

Ninachojua ni kwamba kuna mobile phones zenye GPS na ambazo zina A-GPS. Zile zenye GPS zina software tu ya GPS lakini hazina GPS receiver. Kwa hiyo unatakiwa kuwa na hardware ingine ya GPS receiver ambayo ita-connect na simu yako kupitia bluetooth. Simu zenye A-GPS zina GPS receiver na software yake. Hizo zinapata GPS connection bile ya kutegemea addition hardware.

Kupata GPS signal ni independent na minara ya simu kwani ni mawasiliano moja kwa moja na internet. Ill kuoanisha coordinates za GPS na ramani, inabidi kutumia minara ya simu (GPRS) iliuweze kujua upo wapi kwa kutumia internet connection. Simu yangu ni Nokia E71 na naweza hata kuona nyumba ninayoishi!! Kwa hiyo kwanza lazima ujue kuwa simu yako ina GPS au A-GPS.

Vile vile, natumia kama distance measurement instrument wakati wa safari, wastani wa speed, muda uliotumika etc.

Hakuna haja ya kubadili sim card, kwani mitandao yote inauwezo wa kuunga na internet. Hata hivyo ni vizuri zaidi kutumia mitandao yenye 3G kwani ina-download data za GPS haraka saidi. TiGo tu ndio hawana 3G.

Natumia google maps kwani ni nzuri zaidi ya Nokia maps.
 
---------------------------------------------------------------------

Chief umeniconvice chief, inabidi nianze kuipa kipaumbele zaidi. mimi nina e90 vipi hii ina A-gps au just gps? kuhusu 3G kweli tigo hawana na ndo mana hata kufanya videocalls inakua ngumu, ila voda nao hawajaweka 3G kwenye minara yote wanaendelea na hiyo project kwa sasa. so ukiface tatizo lolote labda la conection timeouts inaweza kuwa kutokana na weaklink, lakini ukiwa kwenye maeneo ambayo minara yake imewekewa 3G devices speed inakua nzuri. maeneo mengine ni kama mwenge,posta na ubungo minara ya hayo maeneo ina 3G. so kwa matokeo mazuri hakikisha unachip nyingine mbali na tIGO. i suggest VODA for that!
 
Kupata GPS signal ni independent na minara ya simu kwani ni mawasiliano moja kwa moja na internet. .

Hapo inatakiwa kusomeka satellite badala ya internet. mengine ni kama yalivyo.

Yap. Nokia E90 ina A-GPS (http://www.gsmarena.com/nokia_e90-1857.php) Kwa hiyo inaweza kupata GPS signal Nilitumia E71 yangu kwenye safari moja kujua max speed ya Boeing tuliyopanda, average speed na muda tuliotumia. Nili-set simu kwenye offline ili isitafute minara ya simu. It was fun🙂
 
Sasa wewe umesema haitegemei Network ya simu kisha unasema Voda wana 3G ndio mana ni convinient zaidi!!!!!!!!! kwa GPS??ahh mnanichanganya sasa au nije hapo kariakoo kujaribu rabda ndio satellite za GPS signals zipo! Kama kweli GPS haitegemei network! je ukiweka simu offline mode or usipoweka simcard simu inaweza kureceive?
 

Khalids.

GPS coordinates hazitegemei minara. Lakini ramani zinategemea minara. Utaweza kupata coordinates zako hata mahali hakuna network ya simu lakini hutaweza kujua hizo coordinates ni sehemu gani katika ramani bila ya kuwa na mnara. Hivyo popote utakapokuwa duniani unaweza kupata GPS coordinates lakini utaweza kutumia google map tu kama kuna minara.
 


@khalids

usichanganyikiwe man, chukua maneno ya chief and try to understand, let us know ukifeli baada ya kutest okay bro...? kama nlivyokuambia voda itakupa matokeo mazuri zaidi.
 

Mkuu naomba link basi ya uliko toa map hizo hata kama ni za kulipia mpaka sasa nimeshidwa kupata link ya map hiyo.
 
habari zenu jamani?
Mimi natumia simu ya nokia E61i, iliyowezeshwa GPS ndani yake. Ila kwenye matumizi inanipa tabu tupu. Kila nikijaribu kutumia inasema GPS not available. Nimekua nikijiuliza maswali yasiyokua na majibu, Je simu yangu ni mbovu au kuna semu zakufanya marekebisho sehemu kabla ya kutumia au hiyo huduma haipatikani Tanzania? Mimi nipo singida naomba msaada wenu kuhusu hilo.
 

E61i haina GPS.
http://www.gsmarena.com/nokia_e61i-1858.php

GPS inapatikana duniani kote kwa vile haitegemei kampuni yako ya simu, inatumia satelite za wamarekani, zilizopo kwenye orbit around earth.

Kwa wale wote ambao wana Nokia X6 32GB, Nokia X6 16GB, Nokia N97 mini, Nokia N97, E72, E55, E52, Nokia 6730 classic, Nokia 6710 Navigator, Nokia 5800 Xpressmusic, Nokia 5800 Navigation Edition, Nokia 5230 angalieni OVi Maps, ni full GPS navigation software ya Nokia ambayo ina preloaded maps, yaani hauhitaji internet connection kwenye simu kupata maps, unlike google maps. Kwa TZ ramani imekosa data lakini.

http://maps.nokia.com/ovi-services-and-apps/ovi-maps
 
List ya Map software.
Za bure:

  • Google Maps
Inapatikana for aina nyingi za simu. Android, Windows, Blackberry etc. Inahitaji mtandao kwenye simu kwasababu ramani inavuta kwenye net. Wanajitahidi kwenye ramani ya Dar.
http://www.google.com/mobile/maps/


  • Google Navigation
Hii ni full navigation software ya Google inarun kwenye some Android Phones. Ila inahitaji mtandao, maps hazihifadhiwi kwenye simu.
http://www.google.com/mobile/navigation/

  • Ovi Maps
Ni ya Full navigator ya Nokia, inapatikana kwa baadhi ya simu zao. Haihitaji mtandao, ramani zinahifadhiwa kwenye simu.
http://maps.nokia.com/ovi-services-and-apps/ovi-maps


  • Bing!
Ya Microsoft, so inafanya kazi kwenye Windows Mobile, iPhone, Blackberry na nyingine. sawa na Google Maps hii, unahitaji mtandao.
http://www.discoverbing.com/mobile/

Za kulipia:

  • Magellan:
Full navigation, ramani za bongo zidhani kama zipo.
http://www.magellangps.com/products/mobile.asp?SEGID=594


  • TomTom.
Kama Magelan.
http://www.tomtom.com/


Kwa kifupi kama una Nokia ambayo inaweza kusupport Ovi sioni sababu yoyote ya kulipia navigation software maana ni full navigation software kama Magelan au TomTom.
Google Navigator upungufu wake ni kuwa haihifadhi ramani, inabidi uwe connected.

Google Maps na Bing ni maps, sio navigators plus mtandao unahitajika.
 

GPS - Global Positioning System hii sio kwenye simu tu kuna instruents nyingi tu siku hizi ambazo zinafanya hiyo kazi , Surveyors wanaifahamu hii vizuri zaidi.

Maswali yako:

1. Kampuni ya simu haina uwezo wowote ule wa kufanya kuweza kubaini nini kinatokea kwenye simu yako, watengenezaji wa simu ambao wameweka GPS kwa kutumia hiyo technology wanaiwezesha simu yako ku-link up na minara uliyopo na satellite ambazo zipo juu kuweza kufahamu uko wapi.

2. Ukitaka kuwa accurate sana ni lazima u-link up na satellite karibu tatu utapata very accurate positioning. Tatizo la Tanzania na nchi nyingi za Afrika hakuna satellite nyingi kuweza kupata hiyo accuracy hence unakuwa almost 120m. na sababu nyingine huenda walioweka GPS yako wali-limit idadi ya kupokea mawasiliano kupitia satellite.

3. Hakuna setting yoyote unayotakiwa kufanya. Accuracy itatokana na amount ya satellite ambazo utakuwa linked.
 
Hehe sijui settings lakini GPS signal inapatikana Tanzania.
Sijui sana kuhusu GPS lakini najua kucheka, ni Heee!heee!.
Halafu najua kwamba Saif Ghadafi na baba yake walikuwa na misimu mikubwa yenye GPS wote walishikwa kirahisi tu.
 


Nimeona niyakuze haya maelezo maana watu wengi bado wanachanganya GPS na INTERNET
 

download app. ya google map kisha chek kwenye my location itakuonyesha mahali ulipo popote duniani.
 
isiwe ishu sana, kama kimeo chako kinatumia Internet kuwezesha GPS kulocate sehemu ulipo kama mimi basi all is good, kwa wanaotumia GPS Gadjets nao freshy tu,,
hapo nipo Atwn - Rchugga nakula turn by turn Navigation kama kawa',,,:lol: :lol:

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…