Ulukolokwitanga
JF-Expert Member
- Sep 18, 2010
- 8,396
- 7,968
Sukari na saruji zinazoingizwa nchini na wahindi hawa mabingwa wa kukwepa kodi tangu lini zimeanza kulipiwa kodi halali? Wewe huijui Tanzania ndo maana unaamini kuna kitu kinaendeshwa bila rushwa. Ukifuata ushauri wako nchi inazama kaburini maana hatutakuwa hata na senti moja ya dola kwa kuagiza kila kitu toka nje.Viwanda vya ndani vinawaza kupiga hela tu, vinawanyonya wakulima wa miwa na wananchi wanao nunua sukari pia, ni wavivu wa kubuni njia za kuongeza uzalishaji na kupunguza gharama za uendeshaji. Hawana tofauti na viwanda vya saruji nchini. Haiingii akili sukari (au saruji) iliyotengenezwa nje, imeingizwa nchini na ikalipiwa kodi zote bila kusahau shiping costs halafu inauzwa nafuu kuliko hiyo ya ndani. Inahitaji mwenye mamlaka awe anakunywa viroba ili aweze kuzuia sukari (au saruji) isiingie toka nje, kwanza inaongeza ushindani katika ubora wa bidhaa na unafuu wa bei hivyo mwananchi wa chini anafaidika zaidi.