google tatizo lako kabla hujalileta hapa

google tatizo lako kabla hujalileta hapa

Kwani hayo maujuzi ya itambayo ulikuwa unayapata kipindi hiko si hata google ungeweza yapata?
Aliyeandika na wewe ukiwa mmoj wa waliofaidika hakuwa na akili?
Ukiweza saidia ukishindwa nyamaza mkuu....

Labda nikupe ushauri!! Cku zote mtu akipost kitu kama hujaelewa kausha sio lazima ucomment, jua lazima uwe na source ya problem unayohitaji ndio uingie google, jua naweza andika kitu ukawa hukijui au hujawahi kukisikia den utapata faida flani den hapo ndo naingia google kupata kiundani zaidi kuhusu hiyo kitu !! Kama hujaelewa point yangu niulize tena
 
Hata huko ku google nako ni swala tusilojua jinsi ya kufanya. Kwani wewe unaona raha gani wenzio wakibaki mbumbumbu.wewe ulizaliwa unajua vitu vyote? Au baada ya kujua ku google ndo wajifanya mjaaaanja.
 
naunga mkono hoja,
nina angalizo
kuna mambo mengine yaweza kuonekana ya kawaida kwangu, au kwako lakini ikumbukwe tuna uwezo tofauti
watu wana mawazo tofauti,, kushare something kwa jF haimaanishi tu kuhitaji kwake ila pia understanding ya wana jF kwa ujumla,,, tubebeane mizigu,, ukiwa na jibu zuri na smart mind ukiliweka naamini hakutakua na trend ndefu ie thread ndefu,,, let's hold @ other
blesses
 
Acha Ukumbembe wako bana!
Unapungukiwa na nini mtu akiweka tatizo lake hapa?
Kama huna mchango, wako watakao msaidia...Vilevile Hii forum inatakiwa kutumika na kuchangamka mda wote, Ila kwa mambo ya maana!
Samahani lakini!
 
Acha Ukumbembe wako bana!
Unapungukiwa na nini mtu akiweka tatizo lake hapa?
Kama huna mchango, wako watakao msaidia...Vilevile Hii forum inatakiwa kutumika na kuchangamka mda wote, Ila kwa mambo ya maana!
Samahani lakini!

Mie sijajua maana ya forum ujue?? Eti tusiombe msaada kwani google hatuijui sie kha??...
 
guys tuacheni uvivu kuna problems nyingine uki search google unapata ufumbuzi fasta sio lazima kuja humu kuuliza! maana thread za misaada siku hizi ni nyingi mno tofauti na mwanzo ambapo tulikua tukipata maujuzi ya IT humu ndani kwa sana!! Tuwe wepesi kuumiza vichwa wenyewe mpaka itakaposhindikana ndo ujaribu hapa!! Mfano mtu anauliza wapi atapata maybe IDM crack au virtual dj keys!! Dah..!! Ila ni mtazamo tu.



All sizes | Some Questions Can't Be Answered by Google | Flickr - Photo Sharing!
 
Ni kweli kuwa jambo fulani linaweza kuwa rahisi kwangu kuliko mtu mwingine. Huo ni ukweli mmoja. Hata hivyo ni vizuri tujijengee tabia ya kupekua (google, youtube etc). Tabia hizi ni sawa na tabia za kujisomea tu...

Ni rahisi baadhi ya watu kumshambulia mleta mada kwa kuwa wao wanajiona (na huenda watu wengine/wengi wakawaona hivyo) kuwa ni "wakarimu." Ukarimu si mbadala wa uwajibikaji ama bidii. Mjadala huu ni nyeti na kunatokea ulazima wa kuchagua maneno (kwa kiasi fulani).

Binafsi nahusisha hoja ya muanzisha thread na tabia za kupenda "spoon feeding" ambazo naziona sana katika jamii zetu. Nguvu kubwa inayotumika kumshambulia jamaa inanifanya nitazame mambo haya kwa mashaka.

Mwisho, tusaidiane lakini guys tujijengee tabia za kujitafutia kwa njia ambazo ni "tiba za awali" kama google. Huo ndiyo msimamo wangu.
 
Back
Top Bottom