Good old days

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Sep 11, 2010
4,271
2,401
Inaonekana miaka inavyosogea ndivyo mambo yanavyokuwa hovyo. Hili linathibitishwa na kila mmoja ukimkumbusha miaka ya '80 na early '90. Kikweli miaka ile life ilikuwa tam ukichanganya na uyanki wa primary na sec. Nakumbuka miaka hiyo tukiwinda sana kware kipindi cha masika Moshi huko. Nakumbuka na bar moja ikiitwa kwa soka pale Soweto ilikuwa ikipiga sana vibao vya mbilia beli kama nakei nairobi na tuombe Mungu baba... Sie wakati huo tukicheza kila aina ya mchezo kwenye jengo moja la vigae maarufu kama wailes lililo jirani na bar hiyo. Nikisikia nyimbo hizo nawakumbuka rafiki zangu wote wa utotoni, mambo tuliyofanya, raha iliyokuwepo...machozi yananilengalenga
 
ila hakuna mchezo niliokuwa na naupenda kama Baba na Mama, au kujificha, maana huko unachagua wa kujificha nae hamjitokezi mpaka mmalize kunanihii, da we acha bwana
 
The concept of "good old days" is a myth, based on a sort of psychological Brownian motion if you like.

Hata katika siku hizo nzuri za zamani, kulikuwa na watu hawakuziona nzuri, bali na wao walikuwa na zao nzuri za zamani zaiidi. Na kuna wengine ambao "siku zao nzuri za zamani" ndio wakati huu.

Kwa hiyo unaposema "miaka inavyozidi kuzidi mambo ndivyo yanavyozidi kuwa ovyo" kimsingi unasema kanuni ya pili ya thermodynamics, in closed unattended systems, things tend to go from better to worse.

Lakini kuna waliozaliwa karibuni hawajaona mazuri uliyoyaona wewe, kwa hiyo kwao wao mazuri ni haya ya leo. Waswahili walilijua hili wakasema "Mla mla leo, mla jana kala nini?"

Kwa hiyo good old day is a psychological myth, everyday is a good old day to someone.
 
Kwa hiyo hii myth imewaathiri wengi sana. Ila hata we kiranga ukiangalia, watu wengi wanasisimkwa na life ya past. Maisha ya sasa yako very .com na very digital
 
Kwa hiyo hii myth imewaathiri wengi sana. Ila hata we kiranga ukiangalia, watu wengi wanasisimkwa na life ya past. Maisha ya sasa yako very .com na very digital

maisha ya sasa yako very .com na very digital........................which means or prove what?
 
maisha ya sasa yako very .com na very digital........................which means or prove what?
ukitaka chochote unapress tu cha msingi hela yako. si kama enzi zile za mtafutano
 
we umezaliwa lini? enzi za barua hukumbuki? haya madotcom si maradhi tu?

Barua mpaka leo hii zinatumika hasa kwenye masuala rasmi kwa hiyo si dhani kuwa barua tunaweza kuzihusisha na enzi moja kwa moja.

Katika nchi zilizoendelea ambazo hiyo unayoita .com imetawala, barua zinatumika zaidi na kwa ufanisi zaidi kuliko .com ilikodorora.

Haya madotcom si maradhi tu...........panahitaji ufafanuzi zaidi kabla ya kuweza kutoa mchango zaidi.

Maradhi kwa misingi ipi?
 
Barua mpaka leo hii zinatumika hasa kwenye masuala rasmi kwa hiyo si dhani kuwa barua tunaweza kuzihusisha na enzi moja kwa moja.

Katika nchi zilizoendelea ambazo hiyo unayoita .com imetawala, barua zinatumika zaidi na kwa ufanisi zaidi kuliko .com ilikodorora.

Haya madotcom si maradhi tu...........panahitaji ufafanuzi zaidi kabla ya kuweza kutoa mchango zaidi.

Maradhi kwa misingi ipi?
Dont take it so seriously G. After all ni perception tu. Hata huyo aliyesema good old dayz definitely anajiongelea yeye as Kiranga put it every day is a good old day to someone. Chill G
 
Da Womanizer

usijali wewe ....i was just playing with the wallet. Ndo katika raha zenyewe za enzi hii ya dotcom!:smile-big::glasses-nerdy:
 
Barua mpaka leo hii zinatumika hasa kwenye masuala rasmi kwa hiyo si dhani kuwa barua tunaweza kuzihusisha na enzi moja kwa moja.

Katika nchi zilizoendelea ambazo hiyo unayoita .com imetawala, barua zinatumika zaidi na kwa ufanisi zaidi kuliko .com ilikodorora.

Haya madotcom si maradhi tu...........panahitaji ufafanuzi zaidi kabla ya kuweza kutoa mchango zaidi.

Maradhi kwa misingi ipi?
kweli umeamua. naungumzia maisha ya kijamii zaidi. ukubali tu kuwa enzi zile zilikuwa na utamu fulani tofauti na leo. labda baada ya miaka 15 tutaona leo ni good old days
 
enzi zile mamboo yalikuwa burudani kabisa


Hapo umesema it was really fun unaamka alfajiri saa kumi na moja kuwahi ugawaji ili upate kilo mbili za sukari na kilo nne za unga wa muhogo hapo ni kwa kaya,na na ukishafika ugawaji unaweka jiwe ndio foleni yako kisha unaingia porini na mtoto wa watu kwenda kusuuza pembejeo za haja ndogo.Ukimakiza kusuuza unakuta ugawaji sukari imekwisha unarudi nyumbani bila kitu. Hiyo ni mpaka next week no chai.Ukiamka siku ya shule ni saa kumi na moja alfajiri.Unashika basi la UDA toka Sinza mpaka Manzese.Hapo napo unasubiria Ikarus ya kutoka Ubungo kwenda Posta basi inakuacha fire unaenda zako shule.Ukitoka shule breki ya kwanza Manzese pale Kizenga recording na watoto wa Jangwani na Zanaki huku mkisikiliza Vunja mifupa kama bado meno iko enzi hizo pakiitwa Manzese msufini .Uda ikifika nauli sh/=moja basi ni raha tu.Na Ukimwi ulikuwa haujashika kasi miaka hiyo hivyo ni pekupeku tu kama unaria vire.I wish siku zingejirudia japo kwa nusu saa tu.Bila kusahau salamu zetu yee na mwenzio anakujibu yee
 
Nadhani Wallet anamaanisha social life... Kwa mfano 1 miaka ya nyuma ilikuwa rahisi kwa Wakubwa\watoto wa mtaa mzima kama sio kitongoji kizima kujuana,sasa hali ni tofauti kila mtu na lwake... Mnajuana kwa magari tu... Pia kama kuna msiba watu watatoka mbali kuja kuhudhuria kwako lakini sii majirani zako kama awali... Kingine unakuta mtoto wako anasoma km 30 kutoka ukaapo mambo ya kwenda shuleni kwa mguu hamna... Kama unacho unalipia SCHOOL BUS aka BYE DAD BYE MUM... Gaijin na Kirnga natumai mtakuwa mmemuelewa Wallet
 
Nadhani Wallet anamaanisha social life... Kingine unakuta mtoto wako anasoma km 30 kutoka ukaapo mambo ya kwenda shuleni kwa mguu hamna... Kama unacho unalipia SCHOOL BUS aka BYE DAD BYE MUM...

mie nilitaka kujua tu tuna quantify vipi kuwa kwenda shule kwa miguu ni a good time kuliko kupanda school bus?
 
Nakumbuka hata sie miaka yetu ya '70 mambo yalikuwa mazuri sana wakati tunakula zile ngoma za kina marijani Rajab na wengineo maisha yalikuwa matamu sana wakati huo bwana....Tumevaa vitenge vyenye picha ya Nyerere nywele tumechana afro tunapaka Clearton
nakumbuka Ule wimbo wa ..oooh si sivunje ahadi uliyoniahidi dada..pole sana mimi ni bado msichana tena bado sijamaliza masomo nifanye nini kukuacha siwezi ..kweli old iz gold. kuna nyimbo za kina Kasongo yeye duuh :A S 8:
Siku hizi hii miziki ya kufoka foka hata siielewi mwenzio
 
enzi hizo raha ilikuwa kubwa, watu waliishi kwa ushirikiano mkubwa na matabaka ya wenye nacho na wasio nacho hayakuwepo kabisa tofauti na leo mitoto imekaa ndani kwenye mageti makubwa ikitoka inapelekwa shule na kurudishwa ndani haichangamani na watu wa chini, hivyo tunaandaa taifa la ubinafsi, umangimeza, ufisadi na uhuni tu, sio kama zamani watoto kucheza kombolera pamoja safi kabisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom