Kwa ufahamu nilionao kama mtu anahitaji kukokotoa gharama za ushuru kwenye calculator ya TRA pale aagizapo gari kuna mambo kadhaa ya kuzingatia. Pitia specification la gari husika ikiwemo. (KAMA NITAKOSEA NAOMBA KUREKEBISHWA.)
1.car make, (Toyota)
2.car model, (Allion)
3.model code (CBA-NZT240)
4.year of manufacture, (2005)
5.engine capacity (1490cc).
NOTE: Hivi utavipata kwenye car specs.
Baada ya hapo, kama umeshapakua kikokotozi cha TRA, kuna sheet 2, ya kwanza inaitwa "calculator", ya pili ni "price list". Anza kwa kuweka EXCHANGE RATE kwenye calculator sheet (kuna mahali pa kuweka hii rate). Pili, nenda upande wa PRICE LIST, tafuta gari ambalo unataka kuagiza (bofya CTRL+F, ingiza jina la gari kurahisisha utafutaji halafu bonyeza ENTER) kwa kuzingatia hivyo vitu hapo juu na utaona upande wa kulia RETAIL SELLING PRICE.
1. Nakili hiyo bei ya gari (RSP) halafu rudi kwenye sheet ya kwanza (Calculator), na andika hizo tarakimu kwenye Current retail selling price.
2. Depreciation details zipo kwenye calculator upande wa juu kulia, angalia umri wa gari utakalo halafu ingiza asilimia hizo mahala husika.
3. Kwenye freight pale ingiza gharama za kulisafirisha toka huko liliko ila mpaka hapo total taxes itakuwa ishakupa gharama halisi za ushuru wote.
ZINGATIA: Kuingiza taarifa mahala husika hasa kuhusiana na CC za engine na pia umri wa gari. Data za gari la 2500cc ukiweka mahali pa gari za chini ya 1000cc jua utapata gharama zisizo sahihi.
Marekebisho yanaruhusiwa.