Gharama za data, airtel, halotel, smart, tigo & voda

h120

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2012
Posts
2,545
Reaction score
3,370
Nilikuwa najaribu kuangalia bei za data kwa mitandao tajwa hapo juu, nilichogundua ni voda na tigo bei zao zafanana kana kwamba walipeana copy za bei mpya baada ya kupanga. nitaweka picha za bei kwa mitandao yote.

AIRTEL




HALOTEL





SMART

Hii ni Kwa 4G data plan DSM tu


Hii 3G data plan mikoani



TIGO







VODACOM




Baada ya kuangalia kwa makini, kwa unafuu wa bei mtiririko upo hivi;
1.Halotel
2.Smart
3.Airtel, Tigo & Voda

Mfano kwa Tsh 65,000 unaweza pata GB 71.6 halotel lakini kwa Tsh 95,000 unapata GB 30 kwa tigo na voda.
Smart naona wana bei tofauti kwa DSM ambako ni 4G tu na Mikoani ambako wanatumia 3G, hawajachambua sana vifurushi vyao.

NB;
Sio tangazo la biashara ila ni uchambuzi wa bei za data, ktk mitandao tajwa, binafsi natumia Tigo na Halotel kwa eneo nililopo.

Taarifa zote zimetoka website rasmi za mitandao husika.
 
Kwa Dar..tigo na voda hawana vifurushi rafiki kwa common citizens.....
Vifurushi vya voda na tigo vinatumika maeneo yote ya Tanzania labda kuwe na offer maaulum kwa mkoa husika, au unamaanisha dar bei tofauti na mikoani?
 
Voda wana offa ,kuna dabo bando via mpesa,kuna ile ofa maalum,kuna university ofa ambayo ni nzur kuliko mtandao wowote..
Kutokana na hizo ofa na kwakujali speed basi voda wmetisha

Hivi ukipewa hata gb 100 za tigo kwa sh 500, sijui hta utazifanyia nini.
Anyway TCRA watusaidie ku control hizi bei.
 
TCRA hawawezi kufanya chochote, kama kufungia tu local channel zilipiwe mkono wao ulipendekeza na kubariki unadhani wanajema kwa watanganyika.
 
Vifurushi vya voda na tigo vinatumika maeneo yote ya Tanzania labda kuwe na offer maaulum kwa mkoa husika, au unamaanisha dar bei tofauti na mikoani?
Baadhi ya mikoa kuna offer maalumu.Kitu ambacho kwa Dar naona ni university offer tu na yenyewe ina magumashi yake.
Pili packages za siku ni ndogo na hazina mashiko kwa mtumiaji tena wa kawaida tu. Packages za week na mwezi bado bei yake ni juu kwa mtumiajia wa kawaida pia.
 
Nilishaacha kutumia data za voda.
Mambo ni Halotel wako poa na data zao kwanza ni cheap pia ziko kasi sana kuliko hiyo mitandao mizee ya Tanganyika
 
Tigo wamezidiwa na wateja. Mtandao wake unasumbua sanaa.
 
Wewe hujui nini utafanya ukipewa hizo GB 100, lakini wanao lalamika wanajua nini watafanya wakizipata.
 
Taarifa zote zipo kwenye website za mitandao husika, na pia offer hazijawekwa hapo kutokana kubadilika mara kwa mara.

Nimeona, mfano halotel, badala ya 350 MB imeshuka mpaka 250 MB kwa ths 499
 
Basi watakuwa hawajafanya updates kwenye tovuti yao.

Wakipandisha gharama hawatangazi na wanachelewa ku-update, labda kama wakipunguza gharama ndo inakuwa fasta kubadilisha huku ikiambatana na matangazo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…