Gharama ya kupata hati ya kiwanja

Gharama ya kupata hati ya kiwanja

Udochi

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2015
Posts
1,073
Reaction score
1,576
Nina kiwanja kilichopimwa tayari. Kina ukubwa wa 370 sqm.
Nimefika ofisi ya ardhi ya wilaya niliyopo nimeambiwa gharama ya jumla kupata hati natakiwa nitoe 170,000/=.

Nauliza wajuzi, kwa ukubwa huo wa kiwanja ni sahihi kupata hati kwa gharama hiyo?

Lengo nijue kama ni sahihi au vinginevyo.
 
Ndio gharama zilizowekwa ma serikali,wape tu upate haki yako
Unaweza kutuwekea mchanganuo wa hizo gharama? Maana kupata hati uwa kuna gharama kama zifuatavyo: 1. Ada ya usajili wa hati 2. Kodi ya ardhi 3. Ushuru wa forodha 4. Kodi ya miundo mbinu (premium) 5. Ada ya viziduo 6. Ada ya deed plan.
 
Ni muda muafaka kwa ofisi zote za ardhi kuweka michanganuo kama hii ili kupata hati, wananchi wengi hatujui hii kitu
 
Unaweza kutuwekea mchanganuo wa hizo gharama? Maana kupata hati uwa kuna gharama kama zifuatavyo: 1. Ada ya usajili wa hati 2. Kodi ya ardhi 3. Ushuru wa forodha 4. Kodi ya miundo mbinu (premium) 5. Ada ya viziduo 6. Ada ya deed plan.
Waziri wa ardhi Mr Lukuvi alishatoa maelekezo,kama unaweza ingia youtube utamuona waziri mwenye dhamana akiliongelea hili la hati
 
Waziri wa ardhi Mr Lukuvi alishatoa maelekezo,kama unaweza ingia youtube utamuona waziri mwenye dhamana akiliongelea hili la hati
Ninachokumbuka waziri alizungumzia gharama za mwananchi kulipia upimaji eneo lake wakati wa urasimishaji wa maeneo unaohusisha watu wengi kwa wakati mmoja ambapo aliagiza gharama hizo zisizidi 150,000/=. Lakini baada ya kulipia hiyo 150,000/= ya upimaji hakutoa mchanganuo wa zile gharama zitakazokuja kulipwa baadae serikalini ili kupewa hati husika. Kifupi kuna gharama za kulipia upimaji ambazo ulipwa kwa kampuni ya upimaji (ambayo ni 150,000/=) na gharama za kulipia serikalini ili kupewa hati (ambazo ndizo tunazohitaji mchanganuo wake).
 
Usilipe, kiwanja chako na documents wanazo zinaonyesha ni chako unataka hati ili iweje, ukabandike kwenye kiwanja au ili iwe nini, au unataka kukiuza?!

Acha wakutunzie wakichoka kukaa nayo wata kupa bure.

Mpigie Lukuvi atakupa maelezo, siku hizi mfumo.ni digital na kama receipt za malipo zinaonyesha ni chako, usiwe na haraka.

Hata ukiichukua utaitunza na labda utapoteza au italiwa na panya, acha wakutunzie, ilipo iko salama.
 
Usilipe, kiwanja chako na documents wanazo zinaonyesha ni chako unataka hati ili iweje, ukabandike kwenye kiwanja au ili iwe nini, au unataka kukiuza?!

Acha wakutunzie wakichoka kukaa nayo wata kupa bure.

Mpigie Lukuvi atakupa maelezo, siku hizi mfumo.ni digital na kama receipt za malipo zinaonyesha ni chako, usiwe na haraka.

Hata ukiichukua utaitunza na labda utapoteza au italiwa na panya, acha wakutunzie, ilipo iko salama.
Kweli za kuambiwa changanya na za kwako.
 
Nina kiwanja kilichopimwa tayari. Kina ukubwa wa 370 sqm.
Nimefika ofisi ya ardhi ya wilaya niliyopo nimeambiwa gharama ya jumla kupata hati natakiwa nitoe 170,000/=.

Nauliza wajuzi, kwa ukubwa huo wa kiwanja ni sahihi kupata hati kwa gharama hiyo?

Lengo nijue kama ni sahihi au vinginevyo.
Lipa bhana acha ubahili.Afu we utakua mpigaji so kila dakika unahisi kupigwa.
Mla uliwa
 
Usilipe, kiwanja chako na documents wanazo zinaonyesha ni chako unataka hati ili iweje, ukabandike kwenye kiwanja au ili iwe nini, au unataka kukiuza?!

Acha wakutunzie wakichoka kukaa nayo wata kupa bure.

Mpigie Lukuvi atakupa maelezo, siku hizi mfumo.ni digital na kama receipt za malipo zinaonyesha ni chako, usiwe na haraka.

Hata ukiichukua utaitunza na labda utapoteza au italiwa na panya, acha wakutunzie, ilipo iko salama.
Unaweza ukanielezea vizuri utaratibu wa kufanikisha hili jambo ndugu
 
Usilipe, kiwanja chako na documents wanazo zinaonyesha ni chako unataka hati ili iweje, ukabandike kwenye kiwanja au ili iwe nini, au unataka kukiuza?!

Acha wakutunzie wakichoka kukaa nayo wata kupa bure.

Mpigie Lukuvi atakupa maelezo, siku hizi mfumo.ni digital na kama receipt za malipo zinaonyesha ni chako, usiwe na haraka.

Hata ukiichukua utaitunza na labda utapoteza au italiwa na panya, acha wakutunzie, ilipo iko salama.
Mkuu,

Hiki kiwanja nimekinunua kutoka kwa mtu ambaye kapima viwanja kadhaa kwenye eneo lake na anaviuza, ambapo havina hati.

Kwenye suala la ujenzi siku hizi ukijenga bila kupata kibali cha ujenzi unaamrishwa kusimamisha ujenzi na waweza pewa penalti,
Na hati inahitajika kama kiambatanisho katika kuomba kibali.
 
Mkuu,

Hiki kiwanja nimekinunua kutoka kwa mtu ambaye kapima viwanja kadhaa kwenye eneo lake na anaviuza, ambapo havina hati.

Kwenye suala la ujenzi siku hizi ukijenga bila kupata kibali cha ujenzi unaamrishwa kusimamisha ujenzi na waweza pewa penalti,
Na hati inahitajika kama kiambatanisho katika kuomba kibali.
Hahaha huyo aliyekuuzia mlitakiwa mkabadirishe hati isome jina lako, kisha uichukue. Ila kwakuwa ulituambia hutaki kulipia ndio nikakwambia huna haja kabisa.
Hati ya nini?
 
Mkuu usipoteze pesa zako,,kiwanja chenye ukubwa wa chini ya 400sqm hupewi hati isipokua utapewa leseni ya makazi tu.
Jaribu kufatili vzr wizarani kabla hujaanza mchakato
 
Mkuu usipoteze pesa zako,,kiwanja chenye ukubwa wa chini ya 400sqm hupewi hati isipokua utapewa leseni ya makazi tu.
Jaribu kufatili vzr wizarani kabla hujaanza mchakato
Hivi majibu ya wizarani yanaweza kuwa tofauti na yale aliyopewa na ofisi ya ardhi ya wilaya aliyopo kwamba gharama ya jumla kupata hati ni 170,000/= na kwamba kiwanja cha ukubwa huo hakipati hati? Na je gharama za leseni ya makazi ndiyo zinafika 170,000/=?
 
Unaweza ukanielezea vizuri utaratibu wa kufanikisha hili jambo ndugu
Lukuvi katoa number zake ana program yake ya kusaidia watu kupata hati zao, sijui kama ni bure au ni kiasi gani jaribu kuwasiliana na wizara yake utaipata number yake.
 
Mkuu usipoteze pesa zako,,kiwanja chenye ukubwa wa chini ya 400sqm hupewi hati isipokua utapewa leseni ya makazi tu.
Jaribu kufatili vzr wizarani kabla hujaanza mchakato
Kiwanja cha size yoyote kilichopimwa unapewa hati.
Ndiyo maana ya kupimwa, hakuna kitu kinaitwa leseni ya makazi.
 
Back
Top Bottom