Ghana yasherekea miaka 63 ya Uhuru

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Raia wa Ghana, leo wanasherehekea miaka 63 ya uhuru wa Taifa hilo.

Ghana itawaliwa na Uingereza na kupata uhuru wake Machi Sita mwaka 1957, chini ya Mwanasiasa mashuhuri na mwanamapinduzi wa Taifa hilo Kwame Nkurumah.

Nkurumah ndiye alikua Waziri Mkuu wa kwanza wa Ghana baada ya uhuru na baadaye Rais wa Taifa hilo ambalo hapo awali lilijulikana kama Gold Coast.

Ghana ilikuwa ni nchi ya kwanza Kusini mwa Jangwa la Sahara kupata uhuru wake na baada ya hapo chini ya Mwanasiasa huyo mashuhuri Nkurumah, ilijitahidi kuhakikisha nchi nyingine za Afrika ikiwemo Tanzania zinapata uhuru wake.

Shamrashamra za kuadhimisha siku ya uhuru wa Ghana zinaendelea hivi sasa katika uwanja wa michezo wa Baba Yara uliopo kwenye mji wa Kumasi, ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika katika mji huo.

Kwa kawaida siku hiyo ya uhuru huwa ikisherehekewa na raia wa Ghana waliopo nchini humo na wale waliopo nje ya nchi, ambao wamekua wakifanya shughuli mbalimbali ili kuienzi siku hiyo.

Siku ya uhuru Ghana ni ya mapumziko ambapo wafanyakazi wa umma na wale wa sekta binafsi nao wanakua mapumziko ili kusherehekea siku hiyo ambayo wanaiona muhimu katika Taifa hilo ambalo lilikua likifahamika sana kwa utajiri wa dhahabu pamoja na pembe za ndovu.
 
Raia wa Ghana, leo wanasherehekea miaka 63 ya uhuru wa Taifa hilo.

Ghana itawaliwa na Uingereza na kupata uhuru wake Machi Sita mwaka 1957, chini ya Mwanasiasa mashuhuri na mwanamapinduzi wa Taifa hilo Kwame Nkurumah.

Nkurumah ndiye alikua Waziri Mkuu wa kwanza wa Ghana baada ya uhuru na baadaye Rais wa Taifa hilo ambalo hapo awali lilijulikana kama Gold Coast.

Ghana ilikuwa ni nchi ya kwanza Kusini mwa Jangwa la Sahara kupata uhuru wake na baada ya hapo chini ya Mwanasiasa huyo mashuhuri Nkurumah, ilijitahidi kuhakikisha nchi nyingine za Afrika ikiwemo Tanzania zinapata uhuru wake.

Shamrashamra za kuadhimisha siku ya uhuru wa Ghana zinaendelea hivi sasa katika uwanja wa michezo wa Baba Yara uliopo kwenye mji wa Kumasi, ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika katika mji huo.

Kwa kawaida siku hiyo ya uhuru huwa ikisherehekewa na raia wa Ghana waliopo nchini humo na wale waliopo nje ya nchi, ambao wamekua wakifanya shughuli mbalimbali ili kuienzi siku hiyo.

Siku ya uhuru Ghana ni ya mapumziko ambapo wafanyakazi wa umma na wale wa sekta binafsi nao wanakua mapumziko ili kusherehekea siku hiyo ambayo wanaiona muhimu katika Taifa hilo ambalo lilikua likifahamika sana kwa utajiri wa dhahabu pamoja na pembe za ndovu.
Afadhali ya MKOLONi wangelikuwa mbali zaidi ya upuuzi walionao sasa
 
Uhuru wa Ghana wana haki ya kusherehekea,uhuru una maana kubwa sana kwao na una thamani. Hata wanapofanya uchaguzi kweli unakuwa huru na haki,akipita mpinzani kwenye sanduku la kura kweli anakabidhiwa uongozi,hawana ujinga ujinga wa kufanya tofauti na wapiga kura walichoamua. Ile nchi iko huru kabisa. Ni mfano wa kuigwa barani Africa. Hongera kwao sana Ghana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa ndio walikuwa nchi ya kwanza Kusini mwa jangwa la Sahara kupata uhuru yaani waliwafungua macho wengine wakatambua kumbe kuwa huru na kujitawala ni jambo linalowezekana.

Hongera kubwa Sana kwao.
 
Back
Top Bottom