Ghana kuongeza umri wa kuolewa

Ghana kuongeza umri wa kuolewa

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,686
110805153003_wedding_ring_304x171_1_nocredit.jpg


Mtakwimu Mkuu wa serikali ya Ghana, Bi Philomena Nyarko, amesema umri halali wa mwanamke kuolewa unapaswa kuongezwa kutoka miaka 18 hadi23.
Bi. Nyarko amesema, hatua hiyo itawafanya wanawake kujiandaa vyema kiakili na kimwili kuzaa watoto, na kwamba, itapunguza ongezeko la idadi ya watu nchini Ghana kwa kati ya 15% hadi 20%.
Mapendekezo yake yamekuja wakati Wabunge nchini Nigeria wanajadili kuhusu kupunguza umri wa kuolewa kutoka miaka 18 ya sasa ili watu waweze kuoa na kuolewa katika umri mdogo zaidi.
Baadhi ya Wabunge Waislam, wametoa hoja kwamba, kuzuia watu kuolewa kabla ya miaka 18, unakiuka sheria za Kiislam ambazo zinaruhusu ndoa katika umri mdogo.
Nigeria ambayo inaongoza kwa idadi kubwa ya watu barani Afrika, imegawanyika kati ya Waislam na Wakristo.
Bi. Nyarko amesema kwamba, wanawake wanaochelewa kuolewa ama kuzaa hadi umri wamiaka 23 wanakuwa na afya njema.
Inafahamika vizuri kwamba, matokeo ya afya njema kwa mama na mtoto, endapo atachelewa kuzaa hadi msichana anapokuwa amekomaa vya kutosha kwa ajili ya kuolewa na kubeba mimba ili kuokoa maisha ya mama na mtoto, amesema Bi. Nyarko.
Watu wengi nchini Ghana ambayo ina watu takriban milioni25.5 ni Wakristo.

Source: BBC
 
uhusiano kati ya kuzaa na kuolewa ulishaisha long time,,, wengi wanaolewa wamama arleady,,,
 
Back
Top Bottom