rosemarie
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 6,887
- 3,439
WAKATI tuzo ya kuuenzi Muungano iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete kwa Jaji Joseph Warioba ikiibua maswali, Rais mstaafu wa Bunge la Afrika, Gertrude Mongela, amekosoa upendeleo uliofanywa na Rais Jakaya Kikwete katika utoaji wa tuzo hiyo.
Mongela ambaye amepata kuwa Mbunge wa Ukerewe kwa muda mrefu, amemshangaa Rais Kikwete kuwatunukia wanaume pekee nishani ya kuuenzi Muungano na kuwaacha wanawake ambao wapo waliofanya mambo makubwa ya kuuenzi Muungano kuliko hao waliopewa.
Akizungumza katika mkutano wa pili wa masuala ya jinsia katika nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Mongela alisema ameshangaa kuona katika orodha ya waliopewa tuzo hakuna mwanamke hata mmoja wakati anawafahamu wanawake wengi waliofanya mambo makubwa katika kuuenzi Muungano.
"Wapo wanawake wengi ambao wameuenzi Muungano huu kama kina Mwanaidi Makame, mwanamke ambaye alikuwa akiimba nyimbo za kuhamasisha Muungano, kwanini mwanamke kama huyo asingepewa tuzo?" alihoji Mongela.
Mongela aliwataja wanawake wengine aliosema wangepaswa kupata tuzo hiyo kuwa ni Mama Sophia Kawawa, aliyeanzisha mapambano ya kumkomboa mwanamke wakati huo akiwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ambapo alipigania kuondoa sheria ya kuwazuia watoto wa kike kusoma moja kwa moja na badala yake waishie kidato cha sita na kupewa kazi.
"Mwanamama huyo pamoja na elimu yake ndogo ya kujua kusoma na kuandika lakini alikuwa na upeo mkubwa wa kupambanua mambo na hatimaye alifanikiwa kumshawishi Mwalimu Nyerere kuondoa sheria hiyo na kuwaruhusu watoto wa kike kusoma moja kwa moja hadi Chuo Kikuu," alisema.
Kwa mujibu wa Mongela, mwanamke mwingine aliyestahili tuzo hiyo ni Mama Maria Nyerere, aliyemtunza Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere wakati alipokuwa akipigania Muungano.
Hata hivyo Mama Maria Nyerere alipewa nishani ya Muungano ya daraja la nne.
Akizungumzia kuhusu mwenendo wa mchakato wa Katiba Mpya, Mongela alionyesha kukerwa na namna ambavyo Bunge limeendeshwa, kutokana na wajumbe wengi kutoleana lugha za matusi na kusahau kujadili masuala muhimu yaliyowaleta bungeni.
"Wajumbe walikuwa wakitumia muda mwingi kujadili muundo wa serikali wakati wanajua kabisa wingi wa serikali hauna masilahi kwa Watanzania wengi. Hadi sasa tuna serikali nyingi, kwani zipo za mitaa, vijiji na serikali kuu," alisema.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia kwa Wanawake (TGNP), Lilian Liundi, alitoa wito kwa serikali kuhakikisha wanakamilisha malengo waliyojiwekea ya kuwa na uwakilishi wa 50 kwa 50 kati ya wanaume na wanawake ifikapo mwaka 2015.
Ingawa Liundi alikiri kwamba hadi sasa Tanzania imefanikiwa kupata asilimia 30 ya uwakilishi wa wanawake katika ngazi za maamuzi, lakini alishauri nafasi hizo zisiishie eneo la siasa na badala yake ziwe pia katika sehemu nyingine, zikiwamo za kiuchumi, sayansi na teknolojia.
Liundi alifafanua kuwa suala la 50 kwa 50 linatakiwa kuanzia ngazi ya chini hadi juu na kwa kila sekta.
Akizungumzia changamoto zilizopo kwa wanawake, alisema ni pamoja na kuongezeka kwa vitendo vya kikatili, wanawake wengi kutomiliki mali, hali inayowafanya kutokopesheka huku watoto wa kike wakikosa elimu kwa usawa.
Mbali na Jaji Warioba, wengine waliopewa nishani katika daraja hilo ni Aboud Jumbe Mwinyi, aliyekuwa Rais wa Pili wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, John Malecela, Cleopa Msuya na Dk. Salmin Amour Juma.
Wamo pia Dk. Omar Ali Juma na Idriss Abdul Wakil, ambao sasa ni marehemu.
Walioanza kupata tuzo na nishani hizo ni waasisi wa Muungano wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Aman Karume (wote ni marehemu) na kufuatiwa na Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa.
Wengine ni pamoja na viongozi wa majeshi ya ulinzi na usalama, akiwamo Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jenerali Davis Mwamunyange na Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu.
Wakuu wa JWTZ wastaafu pia walikumbukwa, akiwamo, Jenerali Mirisho Sarakikya na Jenerali David Musuguri.
Waliotunukiwa nishani ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano Daraja la Nne, walikuwa ni Mama Maria Nyerere na Mama Fatma Karume; Bendi ya Msondo Ngoma pia ilipewa tuzo kwa kuuenzi Muungano.
Naye Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, alipewa tuzo maalumu akiwa raia wa Tanzania aliyetoa mchango muhimu katika huduma za jamii.
Source: Tanzania Daima
Mongela ambaye amepata kuwa Mbunge wa Ukerewe kwa muda mrefu, amemshangaa Rais Kikwete kuwatunukia wanaume pekee nishani ya kuuenzi Muungano na kuwaacha wanawake ambao wapo waliofanya mambo makubwa ya kuuenzi Muungano kuliko hao waliopewa.
Akizungumza katika mkutano wa pili wa masuala ya jinsia katika nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Mongela alisema ameshangaa kuona katika orodha ya waliopewa tuzo hakuna mwanamke hata mmoja wakati anawafahamu wanawake wengi waliofanya mambo makubwa katika kuuenzi Muungano.
"Wapo wanawake wengi ambao wameuenzi Muungano huu kama kina Mwanaidi Makame, mwanamke ambaye alikuwa akiimba nyimbo za kuhamasisha Muungano, kwanini mwanamke kama huyo asingepewa tuzo?" alihoji Mongela.
Mongela aliwataja wanawake wengine aliosema wangepaswa kupata tuzo hiyo kuwa ni Mama Sophia Kawawa, aliyeanzisha mapambano ya kumkomboa mwanamke wakati huo akiwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ambapo alipigania kuondoa sheria ya kuwazuia watoto wa kike kusoma moja kwa moja na badala yake waishie kidato cha sita na kupewa kazi.
"Mwanamama huyo pamoja na elimu yake ndogo ya kujua kusoma na kuandika lakini alikuwa na upeo mkubwa wa kupambanua mambo na hatimaye alifanikiwa kumshawishi Mwalimu Nyerere kuondoa sheria hiyo na kuwaruhusu watoto wa kike kusoma moja kwa moja hadi Chuo Kikuu," alisema.
Kwa mujibu wa Mongela, mwanamke mwingine aliyestahili tuzo hiyo ni Mama Maria Nyerere, aliyemtunza Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere wakati alipokuwa akipigania Muungano.
Hata hivyo Mama Maria Nyerere alipewa nishani ya Muungano ya daraja la nne.
Akizungumzia kuhusu mwenendo wa mchakato wa Katiba Mpya, Mongela alionyesha kukerwa na namna ambavyo Bunge limeendeshwa, kutokana na wajumbe wengi kutoleana lugha za matusi na kusahau kujadili masuala muhimu yaliyowaleta bungeni.
"Wajumbe walikuwa wakitumia muda mwingi kujadili muundo wa serikali wakati wanajua kabisa wingi wa serikali hauna masilahi kwa Watanzania wengi. Hadi sasa tuna serikali nyingi, kwani zipo za mitaa, vijiji na serikali kuu," alisema.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia kwa Wanawake (TGNP), Lilian Liundi, alitoa wito kwa serikali kuhakikisha wanakamilisha malengo waliyojiwekea ya kuwa na uwakilishi wa 50 kwa 50 kati ya wanaume na wanawake ifikapo mwaka 2015.
Ingawa Liundi alikiri kwamba hadi sasa Tanzania imefanikiwa kupata asilimia 30 ya uwakilishi wa wanawake katika ngazi za maamuzi, lakini alishauri nafasi hizo zisiishie eneo la siasa na badala yake ziwe pia katika sehemu nyingine, zikiwamo za kiuchumi, sayansi na teknolojia.
Liundi alifafanua kuwa suala la 50 kwa 50 linatakiwa kuanzia ngazi ya chini hadi juu na kwa kila sekta.
Akizungumzia changamoto zilizopo kwa wanawake, alisema ni pamoja na kuongezeka kwa vitendo vya kikatili, wanawake wengi kutomiliki mali, hali inayowafanya kutokopesheka huku watoto wa kike wakikosa elimu kwa usawa.
Mbali na Jaji Warioba, wengine waliopewa nishani katika daraja hilo ni Aboud Jumbe Mwinyi, aliyekuwa Rais wa Pili wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, John Malecela, Cleopa Msuya na Dk. Salmin Amour Juma.
Wamo pia Dk. Omar Ali Juma na Idriss Abdul Wakil, ambao sasa ni marehemu.
Walioanza kupata tuzo na nishani hizo ni waasisi wa Muungano wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Aman Karume (wote ni marehemu) na kufuatiwa na Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa.
Wengine ni pamoja na viongozi wa majeshi ya ulinzi na usalama, akiwamo Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jenerali Davis Mwamunyange na Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu.
Wakuu wa JWTZ wastaafu pia walikumbukwa, akiwamo, Jenerali Mirisho Sarakikya na Jenerali David Musuguri.
Waliotunukiwa nishani ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano Daraja la Nne, walikuwa ni Mama Maria Nyerere na Mama Fatma Karume; Bendi ya Msondo Ngoma pia ilipewa tuzo kwa kuuenzi Muungano.
Naye Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, alipewa tuzo maalumu akiwa raia wa Tanzania aliyetoa mchango muhimu katika huduma za jamii.
Source: Tanzania Daima