Gesi nyingine yagunduliwa Mbeya

Gesi nyingine yagunduliwa Mbeya

Gesi nyingine
yangunduliwa Mbeya eneo la Isebe, Tukuyu.
Ni liquid Carbon dioxide sawa na ile ya Kyejo, Mwakaleli, uzinduzi wake
kufanyika karibuni. Ama kweli ule usemi kuwa kila mahali unapokanyaga
Tanzania ni madini tu.
Swali ni kuwa je sasa ni lazima kila madini yanapogunduliwa yachimbwe
haraka?

Hata tuvumbue sehemu ambayo ukichimba unapata USD, as long as CCM ipo madarakani, TUSAHAU juu ya kufaidika na hizo rasilimali...
 
Gesi nyingine yangunduliwa Mbeya eneo la Isebe, Tukuyu.
Ni liquid Carbon dioxide sawa na ile ya Kyejo, Mwakaleli, uzinduzi wake kufanyika karibuni. Ama kweli ule usemi kuwa kila mahali unapokanyaga Tanzania ni madini tu.
Swali ni kuwa je sasa ni lazima kila madini yanapogunduliwa yachimbwe haraka?

inufaishe walio wengi.:yo:
 
Hii gesi inatumika vipi. Wengi tunfahamu madhara ya CO2 kwenye mazingira(greenhouse gas)
 
Hii gesi inatumika vipi. Wengi tunfahamu madhara ya CO2 kwenye mazingira(greenhouse gas)

baadhi ya matumizi ya co2 ni kutumika katika uzalishaji wa vinywaji kwa mfano coca cola ile gas inayotoka ukiifungua ndiyo yenyewe, pia hutumika kwenye vifaa vya zima moto, pia hutumika kwenye maghala ya kuhifadhia chakula nk. Madhara ya kuishi karibu na eneo lenye gasi hiyo ni kwamba ikivuja kwa wingi ina tabia ya kutwama chini kwa sababu ni nzito kuliko hewa na kiumbe chochote kilicho ndani ya eneo hilo hufa kwa kukosa hewa yaani o2
 
Wamegundua gesi au upepo?

Huo ugunduzi utatusaidiaje sisi walalahoi?
 
Nashukuru kwa taarifa, ngoja niende kariakoo nikachukue wachina wawili niende nao TIC nije kuzunguushia uzio kijiji kizima!
 
Aisee! Tuombe Mungu isiwe karibu na mpaka wa Malawi, yule mama atazidi kuchanganyikiwa!

Gesi nyingine yangunduliwa Mbeya eneo la Isebe, Tukuyu.
Ni liquid Carbon dioxide sawa na ile ya Kyejo, Mwakaleli, uzinduzi wake kufanyika karibuni. Ama kweli ule usemi kuwa kila mahali unapokanyaga Tanzania ni madini tu.
Swali ni kuwa je sasa ni lazima kila madini yanapogunduliwa yachimbwe haraka?
Suala la Msingi ni kujipanga tu, Tanzania inaweza kuendeshwa kwa Utalii peke yake. Ni nchi ya pili kwa vivutio Duniani baada ya Brazili. Tanzanite na Dhahabu pia pekee vingeweza kuendesha nchi. Kila wilaya Tanzania ina Dhahabu. Shaba imetapakaa. Chuma kimeanzia ludewa hadi Bukoba kupitia Kigoma. Samaki pia wanaweza kuendesha nchi bila kutegemea kitu kingine. Hapo hatujagusa kilimo. Gasi ya Mtwara na Mafuta bado haikuwa kipaumbele cha serikali. Bandari za Tanzania zinauwezo pia wa kuiendesha Tanzania na kila mtu akasoma na kutibiwa bure. La msingi ni kujitambua na kuweka vipaumbele. Tanzania tukizingatia amani na utulivu watoto na wajukuu wataneemeka sana na sisi tutazeeka vizuri.
 
Ishu ni pale mafuta yatakapogunduliwa Musoma! Kama hawatadai kuwa wao ni nchi jirani, sijui!

Jamani sio kama yakigundulika musoma, wilaya jirani na musoma, Rorya, kijiji cha Nyamusi kijiji mpakani na Kenya kuna gesi aina ya methane, na iligunduliwa muda mrefu sana na Tanzania Oxygen wana habari napo
 
Gesi nyingine yangunduliwa Mbeya eneo la Isebe, Tukuyu.
Ni liquid Carbon dioxide sawa na ile ya Kyejo, Mwakaleli, uzinduzi wake kufanyika karibuni. Ama kweli ule usemi kuwa kila mahali unapokanyaga Tanzania ni madini tu.
Swali ni kuwa je sasa ni lazima kila madini yanapogunduliwa yachimbwe haraka?
Je ina uhusiaino na uwepo wa volcano apo Mbeya?
 
Hata tuvumbue sehemu ambayo ukichimba unapata USD, as long as CCM ipo madarakani, TUSAHAU juu ya kufaidika na hizo rasilimali...
Nini kifanyike sasa wakati wanaiba kura???
 
Hi gesi ipo siku nyng sana na imeua walevi weng sana ukiwa umekunywa pombe unakufa na mnyama yeyote akpta asubuhi au jion ucku anakufa,TUSHAOKOTA SANA NDEGE KAMA KWALE,VICHECHE NA WANYAMA WADOGO WADOGO,WAZUNGU WA KILA AINA WAMEFIKA KUANGALIA LAKN MPAKA LEO NDO KUONA HI HABARI HAKUNA MATOKEO YA UCHUNGUZ WAO!!MI NI MZAWA WA KIJIJI CHA ISEBELO,KATA YA SWAYA NA Shule ya msingi nimesoma Isebelo
Nimefanya uchunguzi wa kina kuhusu uwepo wa hewa ya sumu ila sijaone ripoti yoyoye katika machapisho yoyote.

Je ni kweli watu wanakufa? Je ni kwa nini wanakufa walevi tu?
Vifo vingapi vimetokea eneo hilo?
 
Back
Top Bottom