Mambo aliyoyafanya Mjerumani ndani ya miaka 30 ya utawala wake hapa Tanganyika, hata kama unawachukia wakoloni lakini alama zake zipo!
1. Upangaji Miji ( Tanga, Dar etc)
2. Reli
3. Kupima madini almost nchi nzima
4. Mashamba ya Mikonge
5. Kanda za Kiserikali ( Wilaya etc)
6. Kukiendeleza na kukipa nafasi Kiswahili Tanganyika badala ya lugha yao ya Kijerumani
7. Meli kama vile Liemba
8. Shule
9. Kututengenezea mifumo ya kitawala kama vile mahakama
10. Kuintroduce mazao ya biashara kama vile kahawa
11. Kuchonga barabara za awali za vumbi, na baadhi hasa mijini kuziweka lami
12. Kuanzisha mashamba makubwa ya karanga etc
Kuna watu wanasema eti hivyo vitu vililenga kuwanufaisha wao, Sasa kwa nini visiwanufaishe kama walikuwa na akili ya kuona fursa na wakaitumia?, Kwani raia wetu nao hawakunufaika au mlitaka tuendelee kuishi zama za stone age za kukimbizana na swala porini?
Kama Mjerumani kuwatandika viboko mababu zetu ndiyo hoja ya kuwachukia mbona serikali za CCM huwa zinatuma mapolisi kuwapiga wananchi wanaoandamana kudai haki zao za kikatiba? ( R.I.P Akwilina)
Mimi nasema waje tushirikiane nao tu, maadamu nia iwe njema kwamba Hawatufanyi Second class citizens bali tunakuwa na usawa, haki, demokrasia, uhuru, freedom of speech, uchumi unaokua, rasilimali zinazotunufaisha, NA SISI NDO TUNAKUA NA SAUTI YA MWISHO JUU YA KUONGOZWAJE!
Mimi yeyote mwenye uwezo wa kuprovide uongozi bora hata kama ni mchina, mweusi , Mzungu kwangu huyo poa tu, anafaa!