P. Majaribu
JF-Expert Member
- Jun 2, 2014
- 1,192
- 625
Baada ya muda mfupi,kuteuliwa kuwa mwanasheria mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.Ndugu George Masaju ameanza kuonesha unafiki mkubwa aidha kwa utashi wake au kuanza kulipa fadhila kwa waliomteua.Mwanasheria huyu mzoefu amenukuliwa akijibu swali aliloulizwa na waandishi wa habari, "kwanini mikataba mingi ya nchi hii haipo wazi".Muheshimiwa huyu bila aibu,amejibu kuwa yeye bado hajakabidhiwa ofisi.Lakini anajisahaulisha kuwa yeye ndiye aliyekuwa naibu mwanasheria mkuu katika ofisi hiyo hiyo.Pia ameshakuwa mshauri wa serikali wa mambo ya sheria kwa muda mrefu.
Hawa ndiyo wale wale tu.
Hawa ndiyo wale wale tu.