Ndugu zangu leo nimevamiwa na vibaka ofisini kwangu wakafanikiwa kumwibia mteja simu, begi na hela. Nilichofanya nimeripoti polisi kisha wakati tunarudi tukakutana na wale vibaka nikawaambia tafadhali rudisheni begi letu kusikia hivyo wakatoa mapanga na visu mimi nikatoa panga langu pia kukabiliana nalo kisha nikamwambia dogo akawaite polisi kwani kituo hakiko mbali huku mimi nikipiga kelele za wezi lakini hakutokea mtu na polisi wakamjibu dogo tutawakamata kesho.
Imagine niko mwenyewe nakabiliana na vibaka watano halafu polisi wanajibu tutawakamata kesho ilihali wako na vitu vyetu na bado wanakabiliana na mimi.
Jamani nimeshindwa hata kuelewa msaada wangu uko wapi kama polisi wananiachia soo mwenyewe na vibaka wakatokomea na begi simu na hela.
Imagine niko mwenyewe nakabiliana na vibaka watano halafu polisi wanajibu tutawakamata kesho ilihali wako na vitu vyetu na bado wanakabiliana na mimi.
Jamani nimeshindwa hata kuelewa msaada wangu uko wapi kama polisi wananiachia soo mwenyewe na vibaka wakatokomea na begi simu na hela.