Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Wananchi wenye hasira kali wamejichukulia sheria mkononi kwa kulichoma gari aina ya Lori baada ya dereva wake kumgonga na kufa papo hapo muuguzi wa zahanati ya Kaseme wilayani Geita.
Tukio hilo limetokea jana usiku katika Kijiji cha Kaseme wakati marehemu huyo akiwa katika bodaboda pamoja na watoto wake wawili, mmoja amefahamika kwa jina la Paulo Talafa mwenye miaka 3 na mwingine mchanga wa miezi miwili ambao wao wamenusurika na kifo hicho.
Mashuhuda wa tukio hilo wanasema Lori hilo lilikuwa kwenye mwendo mkali na walipojaribu kupishana na gari lingine ndipo likawagonga na mama huyo kuumia kuanzia sehemu ya kiuno hadi miguuni na kusababisha utumbo kutoka nje.
Wamesema sababu kubwa iliyochangia watoto hao kutopatwa na madhara kama mama yao ni kuwa alikuwa amewapakata kifuani ambako hawakuguswa na gari hilo.
Marehemu amefahamika kwa jina la Martha Paulo mwili wake umehifadhiwa katika chumba cha maiti kwenye hospitali ya rufaa mkoani Geita.
Chanzo: Azam Tv