Geita Gold FC na akili za Daraja la kwanza

Hadrianus

JF-Expert Member
Feb 19, 2020
2,112
5,208
Ukizoea vya kunyonga...

Baada ya kusota kwa muda mrefu wakiwa Ligi daraja la kwanza hatimaye wakapanda Ligi kuu Tanzania bara maarufu kama NBC PREMIER LEAGUE (Ligi yetu kivyetu vyetu).

Misimu waliyocheza Ligi daraja la kwanza Geita Gold FC walitumia viwanja viwili, kimoja ni cha Shule ya wavulana WAJA na cha pili ni kiwanja cha shule ya sekondari ya wasichana Nyankumbu iliyojengwa kwa udhamini mnono wa GGML (ila upigaji ukawa mkubwa shule ikajengwa tofauti na matarajio si unajua wabongo tena).

Geita Gold FC wakiwa wanatumia uwanja wa shule ya wasichana Nyankumbu, hawakuwahi kupoteza mechi yoyote pale hivyo kupelekea kupaita "Machinjioni".

Kama unakumbuka lile sakata la Geita Gold, Jkt Kanembwa, Polisi Tabora & Jkt Oljoro kushushwa daraja kwa kosa la upangaji matokeo, leo nataka nikupe kisa kwanini wanahangaika kupata matokeo ya ushindi katika michezo ya Ligi kuu hadi kupelekea kumtimua mapema kabisa Ettiene Ndayiragije.

Hawa wakauitwa Geita Gold FC mwanzo walikua wanadhaminiwa vizuri na mgodi wa GGML, jamaa walimwaga pesa za kutosha ili timu isajili, inunue usafiri wake, ilipe vizuri wachezaji hatimaye ipande Ligi kuu.

Kama unavowajua wabongo zile "noti" zikatumiwa vibaya, wakanunua usafiri wa bei rahisi ili wapate pa kupiga, kwa kifupi pesa hazikutumika ipasavyo mbaya zaidi walianza kununua mechi na marefarii.

Geita Gold kila walipokua wanacheza mechi pale Nyankumbu, wanahonga waamuzi ili kuwaminya wapinzani ili mradi wao washinde mechi, mfano unakuta mshambuliaji wa timu pinzani kila akipigiwa pasi, mwamuzi wa pembeni ananyoosha kibendera kwamba ni offside hata kama hajaotea.

Baada ya kashfa hizo za upangaji matokeo na hatimae kushushwa Daraja, GGML walijiondoa kuidhamini timu hiyo na Halmashauri ikaichukua na kukomaa nayo hatimaye ikapanda Ligi Kuu (Ligi daraja la kwanza mipango ni mingi kuliko mpira).

Mashabiki wa Geita Gold FC kumbukeni kwamba mnapolalamika kua timu yenu haipati matokeo mazuri nyumbani ni kwasababu zamani mlikua mnabebwa kwa nguvu, mnashinda kwa ubabe, mfano mechi ile ya JKT Oljoro mchezaji anashika mpira nje ya 18 refa anatenga tuta, mchezaji anapiga penat, kipa anatoa refa anasema penati irudiwe, pakazuka ugomvi mkubwa sana na refa akapigwa ngumi za kutosha.

Nasikitika Wallace Karia ulipoenda kuomba "indosimenti" mkoani Geita viongozi wakakupa masharti kuwa uwanja wa Nyankumbu utumike kuchezewa michezo ya Ligi Kuu ili hali uwanja haukidhi vigezo hata nusu (pichi yake nyasi ni ngumu sana), viongozi wakaomba mechi zao dhidi ya timu kubwa za Dar es Salaam zipangwe mzunguko wa pili na kweli imekua hivyo.

Geita Gold mliuza wafungaji kidogo walikua wanajitahidi mkaenda kusajili wachezaji wabovu kama GEORGE MPOLE na DANY LYANGA mkitegemea mtabaki Ligi kuu? (Hapana lazima mshuke daraja).

Mkamleta Ettiene Ndayiragije ndani ya mechi 4 mmefukuza, mlitegemea awafunge Namungo, Yanga, Mtibwa & Mbeya City? (Lazima mrudi mlikotoka).

Huku Ligi Kuu vyakunyonga havipo, huku kuna kunyongwa tu.

Hali kama yenu ndiyo aliyopitia Gwambina, alinunua mechi, akawa anatembea na marefa kila mechi ni hao hao tu hawabadiliki leo hii Gwambina wako wapi?

Mtarudi mlikotokaaa.

Mlizoea vya kunyonga.

NB: Ligi yetu inatimu nyingi nzuri zinacheza mpira mzuri sana, ila tatizo ni viwanja vingi.

havifai kuchezewa mechi.
 
Kama sijakosea nazani hii Geita gold ni timu iliyonunuliwa zamani ilikua ikiitwa mshikamano fc na sizani kama walimaliza kulipa.
 
Kama sijakosea nazani hii Geita gold ni timu iliyonunuliwa zamani ilikua ikiitwa mshikamano fc na sizani kama walimaliza kulipa.
Walinunua baada ya kushushwa daraja, nadhani bado wanadeni.
 
Ukizoea vya kunyonga...

Baada ya kusota kwa muda mrefu wakiwa Ligi daraja la kwanza hatimaye wakapanda Ligi kuu Tanzania bara maarufu kama NBC PREMIER LEAGUE (Ligi yetu kivyetu vyetu).

Misimu waliyocheza Ligi daraja la kwanza Geita Gold FC walitumia viwanja viwili, kimoja ni cha Shule ya wavulana WAJA na cha pili ni kiwanja cha shule ya sekondari ya wasichana Nyankumbu iliyojengwa kwa udhamini mnono wa GGML (ila upigaji ukawa mkubwa shule ikajengwa tofauti na matarajio si unajua wabongo tena).

Geita Gold FC wakiwa wanatumia uwanja wa shule ya wasichana Nyankumbu, hawakuwahi kupoteza mechi yoyote pale hivyo kupelekea kupaita "Machinjioni".

Kama unakumbuka lile sakata la Geita Gold, Jkt Kanembwa, Polisi Tabora & Jkt Oljoro kushushwa daraja kwa kosa la upangaji matokeo, leo nataka nikupe kisa kwanini wanahangaika kupata matokeo ya ushindi katika michezo ya Ligi kuu hadi kupelekea kumtimua mapema kabisa Ettiene Ndayiragije.

Hawa wakauitwa Geita Gold FC mwanzo walikua wanadhaminiwa vizuri na mgodi wa GGML, jamaa walimwaga pesa za kutosha ili timu isajili, inunue usafiri wake, ilipe vizuri wachezaji hatimaye ipande Ligi kuu.

Kama unavowajua wabongo zile "noti" zikatumiwa vibaya, wakanunua usafiri wa bei rahisi ili wapate pa kupiga, kwa kifupi pesa hazikutumika ipasavyo mbaya zaidi walianza kununua mechi na marefarii.

Geita Gold kila walipokua wanacheza mechi pale Nyankumbu, wanahonga waamuzi ili kuwaminya wapinzani ili mradi wao washinde mechi, mfano unakuta mshambuliaji wa timu pinzani kila akipigiwa pasi, mwamuzi wa pembeni ananyoosha kibendera kwamba ni offside hata kama hajaotea.

Baada ya kashfa hizo za upangaji matokeo na hatimae kushushwa Daraja, GGML walijiondoa kuidhamini timu hiyo na Halmashauri ikaichukua na kukomaa nayo hatimaye ikapanda Ligi Kuu (Ligi daraja la kwanza mipango ni mingi kuliko mpira).

Mashabiki wa Geita Gold FC kumbukeni kwamba mnapolalamika kua timu yenu haipati matokeo mazuri nyumbani ni kwasababu zamani mlikua mnabebwa kwa nguvu, mnashinda kwa ubabe, mfano mechi ile ya JKT Oljoro mchezaji anashika mpira nje ya 18 refa anatenga tuta, mchezaji anapiga penat, kipa anatoa refa anasema penati irudiwe, pakazuka ugomvi mkubwa sana na refa akapigwa ngumi za kutosha.

Nasikitika Wallace Karia ulipoenda kuomba "indosimenti" mkoani Geita viongozi wakakupa masharti kuwa uwanja wa Nyankumbu utumike kuchezewa michezo ya Ligi Kuu ili hali uwanja haukidhi vigezo hata nusu (pichi yake nyasi ni ngumu sana), viongozi wakaomba mechi zao dhidi ya timu kubwa za Dar es Salaam zipangwe mzunguko wa pili na kweli imekua hivyo.

Geita Gold mliuza wafungaji kidogo walikua wanajitahidi mkaenda kusajili wachezaji wabovu kama GEORGE MPOLE na DANY LYANGA mkitegemea mtabaki Ligi kuu? (Hapana lazima mshuke daraja).

Mkamleta Ettiene Ndayiragije ndani ya mechi 4 mmefukuza, mlitegemea awafunge Namungo, Yanga, Mtibwa & Mbeya City? (Lazima mrudi mlikotoka).

Huku Ligi Kuu vyakunyonga havipo, huku kuna kunyongwa tu.

Hali kama yenu ndiyo aliyopitia Gwambina, alinunua mechi, akawa anatembea na marefa kila mechi ni hao hao tu hawabadiliki leo hii Gwambina wako wapi?

Mtarudi mlikotokaaa.

Mlizoea vya kunyonga.

NB: Ligi yetu inatimu nyingi nzuri zinacheza mpira mzuri sana, ila tatizo ni viwanja vingi.

havifai kuchezewa mechi.
Hawa watu wa kanda ya ziwa kuna siku madini yataisha na hawatakuwa na cha kuonesha. Hata uwanja wa mpira hawatakuwa nao. Watabaki na mashimo tu. Hivi inakuaje mtu unahujumu kwenu kwa kiwango hicho? Unamkomoa nani?
 
Hawa watu wa kanda ya ziwa kuna siku madini yataisha na hawatakuwa na cha kuonesha. Hata uwanja wa mpira hawatakuwa nao. Watapaki na mashimo tu. Hivi inakuaje mtu unahujumu kwenu kwa kiwango hicho? Unamkomoa nani?
Watu wametanguliza maslahi yao binafsi.
 
Hivi si ndio hawa kipindi cha nyuma walifungana 8-0, 9-0, .Daraja la kwanza janja janja nyingi sana.
Ndiyo hao hao mkuu, walipiga pesa za mgodi kipindi hicho. Wakashindwa kucheza mpira wakawa wananunua mechi eti saivi wanafukuza kocha wakati wachezaji wao ni viwango vya daraja la 4
 
Binafsi huwa ninawashangaa sana watu wa kanda ya ziwa, sijui ni kwanini wanazi chukia sana na kuzihujumu tim za mikoa yao zilizopo ligi kuu??? Ukiwauliza ni kwa nini wanafanya hivyo yaani ni full visingizio sisivyo na matinki yoyote!
 
Binafsi huwa ninawashangaa sana watu wa kanda ya ziwa, sijui ni kwanini wanazi chukia sana na kuzihujumu tim za mikoa yao zilizopo ligi kuu??? Ukiwauliza ni kwa nini wanafanya hivyo yaani ni full visingizio sisivyo na matinki yoyote!
Tatizo ya hizi timu zinamakundi ndani yake, na sababu kubwa ni upigaji wa pesa.
 
Binafsi huwa ninawashangaa sana watu wa kanda ya ziwa, sijui ni kwanini wanazi chukia sana na kuzihujumu tim za mikoa yao zilizopo ligi kuu??? Ukiwauliza ni kwa nini wanafanya hivyo yaani ni full visingizio sisivyo na matinki yoyote!
Mmiliki wa Gwambina mwaka jana alilalamika kuhujumiwa na wenzake kwenye mechi za nyumbani
 
Mmiliki wa Gwambina mwaka jana alilalamika kuhujumiwa na wenzake kwenye mechi za nyumbani
Wanasingiziwa kuhujumiwa, ila ukweli ni kwamba Daraja la kwanza walikua wanashinda "kwa mipango" wakati Ligi kuu unatakiwa ushinde mechi kwa uwezo wako halisi.
 
Back
Top Bottom