Geita: Askari wanne wa Jeshi la Uhifadhi wakamatwa kwa tuhuma za mauaji

Geita: Askari wanne wa Jeshi la Uhifadhi wakamatwa kwa tuhuma za mauaji

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Baada ya mdau kuweka uzi hapa jukwaani, akihoji ukimya wa TFS na Jeshi la Polisi juu ya mauaji yaliyofanywa na askari hao kwenye pori la uhifadhi (Kwa maelezo ya tukio hilo ingia hapa: DOKEZO - GEITA: Kuna Kijana ameuawa kwa kupigwa risasi na Askari wa Hifadhi ya Pori la Kigosi, TFS na Jeshi la Polisi mbona mpo kimya?), Jeshi la Polisi limetoa ufafanuzi juu ya hatua iliyochokuliwa kwenye tukio hilo:

=====
WhatsApp Image 2025-08-14 at 20.33.04_b556f094.jpg

TAARIFA KWA UMMA
ASKARI WANNE WA JESHI LA UHIFADHI (JESHI USU) WASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA MAUAJI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linawashikilia Askari wanne wa Jeshi la Uhifadhi (JESHI USU) kwa tuhuma za mauaji ya Eziboni Fikiri (20), Mkulima, Mkazi wa Kijiji cha Msonga, Wilaya ya Bukombe.

Tukio hili la mauaji limetokea Agosti 13, 2025 majira ya saa 12:00 asubuhi katika eneo la Pori la Hifadhi ya Kigosi, Wilaya ya Bukombe, Mkoa wa Geita wakati Askari hao wakitekeleza jukumu la ukamataji watu waliokuwa wameingia hifadhini na kukata miti kinyume cha sheria.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Bukombe kwa ajili ya uchunguzi wa kitaalamu. Watuhumiwa wanahojiwa na uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.

Jeshi la Polisi linawaomba wananchi kuwa watulivu wakati uchunguzi wa tukio hili unaoendelea kufanyika ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na:
Kaimu Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Geita
 
TAARIFA KWA UMMA
ASKARI WANNE WA JESHI LA UHIFADHI (JESHI USU) WASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA MAUAJI​

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linawashikilia Askari wanne wa Jeshi la Uhifadhi (JESHI USU) kwa tuhuma za mauaji ya Eziboni Fikiri (20), Mkulima, Mkazi wa Kijiji cha Msonga, Wilaya ya Bukombe.

Tukio hili la mauaji limetokea Agosti 13, 2025 majira ya saa 12:00 asubuhi katika eneo la Pori la Hifadhi ya Kigosi, Wilaya ya Bukombe, Mkoa wa Geita wakati Askari hao wakitekeleza jukumu la ukamataji watu waliokuwa wameingia hifadhini na kukata miti kinyume cha sheria.

Kwa maelezo ya tukio hilo ingia hapa: DOKEZO - GEITA: Kuna Kijana ameuawa kwa kupigwa risasi na Askari wa Hifadhi ya Pori la Kigosi, TFS na Jeshi la Polisi mbona mpo kimya?

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Bukombe kwa ajili ya uchunguzi wa kitaalamu. Watuhumiwa wanahojiwa na uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.

Jeshi la Polisi linawaomba wananchi kuwa watulivu wakati uchunguzi wa tukio hili unaoendelea kufanyika ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na:
Kaimu Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Geita
Duuh hatari,watavuna walichopanda,mbao tuu!
 
Yaani unaua binadamu mwenzako kwa sababu ya kulinda mapori au wanyama!
 
Mi nadhani hawa vijana sababu ya kufeli shule huwa wanatumia nguvu badala ya akili,Yaani mtu kukata misitu unapiga risasi hovyo.wenye nchi wanakula eti nyie mnalinda misitu
 
Baada ya mdau kuweka uzi hapa jukwaani, akihoji ukimya wa TFS na Jeshi la Polisi juu ya mauaji yaliyofanywa na askari hao kwenye pori la uhifadhi (Kwa maelezo ya tukio hilo ingia hapa: DOKEZO - GEITA: Kuna Kijana ameuawa kwa kupigwa risasi na Askari wa Hifadhi ya Pori la Kigosi, TFS na Jeshi la Polisi mbona mpo kimya?), Jeshi la Polisi limetoa ufafanuzi juu ya hatua iliyochokuliwa kwenye tukio hilo:

=====
View attachment 3441510
TAARIFA KWA UMMA
ASKARI WANNE WA JESHI LA UHIFADHI (JESHI USU) WASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA MAUAJI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linawashikilia Askari wanne wa Jeshi la Uhifadhi (JESHI USU) kwa tuhuma za mauaji ya Eziboni Fikiri (20), Mkulima, Mkazi wa Kijiji cha Msonga, Wilaya ya Bukombe.

Tukio hili la mauaji limetokea Agosti 13, 2025 majira ya saa 12:00 asubuhi katika eneo la Pori la Hifadhi ya Kigosi, Wilaya ya Bukombe, Mkoa wa Geita wakati Askari hao wakitekeleza jukumu la ukamataji watu waliokuwa wameingia hifadhini na kukata miti kinyume cha sheria.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Bukombe kwa ajili ya uchunguzi wa kitaalamu. Watuhumiwa wanahojiwa na uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.

Jeshi la Polisi linawaomba wananchi kuwa watulivu wakati uchunguzi wa tukio hili unaoendelea kufanyika ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na:
Kaimu Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Geita
Hakuna kesi hapo.
 
Yaani unaua binadamu mwenzako kwa sababu ya kulinda mapori au wanyama!
Mkuu Waafrika tumelaaniwa utakuta Askari ana muua Mtanganyika Mwenzake kwasababu ya Mali ya Mzungu na Mxungu mwenyewe hiyo Mali siyo ya Kwake ni Mali ya Watanganyika.
 
Alifanya mauaji wakati akitekeleza majukumu yake ktk oparesheni ya kuwakamata watu waliokuwa wameingia kuk hifadhi kukata miti kinyume na sheria. Kuua bila kukusudia. Hakuna kosa hapo.
 
Yaani unaua binadamu mwenzako kwa sababu ya kulinda mapori au wanyama!
Hili ni jambo la kawaida kabisa kwa Watu weusi.

Unabomoa Makazi ya Binadamu, kuwahamisha na kuwafurusha kwa nguvu kwa silaha za moto kama vile bunduki ili kuwapisha Wanyapori ili wapate makazi ya kuishi
Pathetic!
 
Back
Top Bottom