Niliwahi sema humu mwananchi linakoelekea litakuwa gazeti la udaku na pengine la kisiasa kama uhuru na tz daima. Leo katika toleo lake limetoka na kichwa cha habari"katiba mpya shakani" point yao kuwa ukawa kujitoa.
Ukisoma wamepiga porojo tu ndani hakuna uchambuzi wa kina kivipi theluthi mbili hazipatikani bila ukawa kuwepo. Wanasema ccm walitegemea wajumbe 16 toka ukawa ili wapitishe.
Hawaelezi theluthi mbili wajumbe wangapi toka 629 jumla. Na ukawa wako 190. Mwananchi tunzeni heshima yenu mnapoteza mweleko la sivyo mjitangaze nanyi ni kama uhuru na taz daima.
Nyuma mlitoka pia sita apata pigo kuwa hati ya muungano hakuna hakuna muungano kwa kubeba maneno ya tindu lissu, je mlikwenda mamlaka husika kujua hamkwenda hati imetoka taarifa yake mumeificha.
Mwananchi rudini kwa mstari mnapotea mumekuwa gazeti la ushabiki zaidi kwa sasa na kuacha kufanya tafiti kwa habari zenu.
Mhariri mwananchi upo au haupo. Au mnaongozwa na mmiliki wenu huyo mkenya.
=====
Habari yenyewe.
Ukisoma wamepiga porojo tu ndani hakuna uchambuzi wa kina kivipi theluthi mbili hazipatikani bila ukawa kuwepo. Wanasema ccm walitegemea wajumbe 16 toka ukawa ili wapitishe.
Hawaelezi theluthi mbili wajumbe wangapi toka 629 jumla. Na ukawa wako 190. Mwananchi tunzeni heshima yenu mnapoteza mweleko la sivyo mjitangaze nanyi ni kama uhuru na taz daima.
Nyuma mlitoka pia sita apata pigo kuwa hati ya muungano hakuna hakuna muungano kwa kubeba maneno ya tindu lissu, je mlikwenda mamlaka husika kujua hamkwenda hati imetoka taarifa yake mumeificha.
Mwananchi rudini kwa mstari mnapotea mumekuwa gazeti la ushabiki zaidi kwa sasa na kuacha kufanya tafiti kwa habari zenu.
Mhariri mwananchi upo au haupo. Au mnaongozwa na mmiliki wenu huyo mkenya.
=====
Habari yenyewe.
Bunge la Katiba Mpya shakani
![]()
"Ni kweli kwamba kutokuwapo kwao kunaweza kuwa na athari katika kufanya uamuzi, lakini pia hatuwezi kusema ni athari zipi kwa sasa kwa sababu hakuna suala ambalo linapaswa kufanyiwa uamuzi kwa sasa."PICHA|MAKTABA
Posted Ijumaa,Aprili18 2014 saa 24:0 AM
KWA UFUPI
Hamad alisema kama alivyosema Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta ipo fursa za kufanya mazungumzo na kwamba anaamini ikitumika vizuri, Bunge litaweza kuendelea na kufikia mwisho mwema.
Dodoma. Hatua ya baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba kususia vikao vya Bunge hilo imezua hofu kwamba inaweza kukwamisha mchakato wa kupatikana kwa Katiba mpya hasa katika kufanya uamuzi wa kupitisha ibara za Katiba hiyo.
Wajumbe ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), juzi walitoka nje na kususia vikao vya Bunge hilo kwa madai kwamba hawaridhishwi jinsi mambo yanavyokwenda.
Kanuni za uendeshaji wa Bunge hilo za 2014, zinasema ili ibara au Rasimu ya Katiba iweze kupitishwa itahitaji kuungwa mkono na theluthi mbili ya wajumbe kwa pande zote za Muungano.
Kanuni ya 37 (1), inasomeka: "… ili ibara au rasimu iweze kupitishwa, itahitaji kuungwa mkono na wingi wa theluthi mbili ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na theluthi mbili kutoka Zanzibar."
Taarifa zisizo rasmi zinasema awali ili kuwezesha kupatikana kwa theluthi mbili kutoka upande wa Zanzibar, CCM kilikuwa kinakihitaji kupata kura 16 ikilinganishwa na idadi ya wajumbe wanaokiunga mkono.
Kwa maana hiyo kuondoka kwa wanachama wa Ukawa kunamaanisha kwamba Bunge Maalumu haliwezi kupata akidi inayotakiwa wakati wa kufanya uamuzi wa kupitisha ibara kwa mujibu wa kanuni hizo.
Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba alisema jana kuwa hawatarejea katika Bunge hilo hadi kutakapokuwa na maridhiano ambayo kwa upande wao ni kuzingatiwa kwa rasimu iliyotokana na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba. Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad alisema hivi sasa si vyema kutabiri kama wajumbe wa Ukawa watarejea bungeni au la.
"Mimi na wewe hatuwezi kutabiri, maana hawa ni viongozi wa kisiasa, wanaweza kuondoka leo, lakini kesho wakawa na mazungumzo na wenzao halafu wakarejea bungeni na shughuli zikaendelea," alisema Hamad na kuongeza:
"Ni kweli kwamba kutokuwapo kwao kunaweza kuwa na athari katika kufanya uamuzi, lakini pia hatuwezi kusema ni athari zipi kwa sasa kwa sababu hakuna suala ambalo linapaswa kufanyiwa uamuzi kwa sasa."
Hamad alisema kama alivyosema Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta ipo fursa za kufanya mazungumzo na kwamba anaamini ikitumika vizuri, Bunge litaweza kuendelea na kufikia mwisho mwema.
"Kwa hiyo mimi nasema sisi tusubiri, maana hadi sasa hatujapata kufahamu kama kuondoka kwao watarejea baada ya Pasaka, Jumanne ijayo au ndiyo wameondoka moja kwa moja au ni vipi, ndiyo maana nasema ni vigumu kudhania kitakachotokea," alisema Hamad ambaye pia ni Katibu wa Baraza la Wawakilishi.
Wasusia Kamati ya Uongozi.