nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
* Yajipanga kutumia Mungiki kuvuruga amani
NA MWANDISHI WETU
Gazeti la Uhuru
WAKATI CHADEMA ikitangaza kuanza maandamano ya nchi nzima kupinga muswada wa kuruhusu kuundwa tume ya kupokea maoni kuhusu katiba mpya, kuna taarifa kuwa chama hicho kimepanga kutumia wafuasi wa kikundi cha Mungiki kutoka Kenya kuhamasisha vurugu nchini.
CHADEMA pia inadaiwa kuandaa vijana wa Kitanzania 60,000 watakaoshirikiana na kikundi hicho kuwajenga kisaikolojia kushiriki kwa nguvu katika maandamano hayo.
Mkakati huo upo kwenye waraka (Uhuru ina nakala yake) uliosambazwa na uongozi wa juu wa chama hicho kwenda kwa makatibu wakuu wa CHADEMA katika mikoa ya Tanzania Bara.
Taarifa za kuaminika kutoka makao makuu ya chama hicho zilidai mpango huo utawapa ujasiri vijana kupitia wanaharakati hao kutoka Kenya.
"Tunapaswa kuwajengea uwezo wa kujiamini na kutosikiliza vitisho vinavyotolewa na serikali ili wawe tayari kushiriki kwenye maandamano,'' ilisema sehemu ya waraka huo kwenda kwa makatibu wakuu.
Waraka huo pia uliwataka makatibu wakuu kuhakikisha wanapata fedha za kutosha na kuziwasilisha makao makuu ili zitumike kuwalipa wanaharakati hao.
Alipoulizwa kuhusu habari hizo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema amepokea jalada la CHADEMA kuhusu maandamano lakini hajalisoma na kwamba leo atalitolea ufafanuzi.
"Jalada limefika mezani kwangu ila bado sijalisoma. Nitatoa ufafanuzi kuhusu maandamano hayo, hilo la Mungiki tutalifuatilia na tulitolea taarifa,'' alisema. Kwa upande wake, Mkuu wa Operesheni wa chama hicho, Benson Singo, alikana madai ya kushirikiana na kikundi cha Mungiki. Hata hivyo, alikiri kuwepo maandamano hayo, yatakayoanza Jumamosi katika mikoa 10.
"Kweli tuna maandamano yatakayohusisha viongozi wote wa kitaifa katika mikoa 10, lengo ni kupinga muswada wa maboresho ya katiba,'' alisema. Alisema maandamano hayo yatafanyika Arusha, Mbeya, Kigoma, Kilimanjaro, Ruvuma, Dodoma, Pwani, Mtwara, Tabora na Morogoro.
Katika hatua nyingine, Taasisi ya Demokrasia na Utawala Bora Tanzania (CEGODETA), imelaani tabia ya baadhi ya vyama vya siasa kupeleka vijana wahuni wa vijiweni kwenye midahalo ya katiba.
Inadaiwa vijana hao hupelekwa kwenye midahalo hiyo ili wakawazomee na kufanya fujo wakati wachangiaji wa vyama vingine wanapozungumza.
Mkurugenzi wa CEGODETA Thomas Ngawaiya alisema: "Tabia hiyo si ya kistaarabu na inaonyesha kuna baadhi ya vyama ambavyo viongozi wake bado hawajakomaa kisiasa, na wala hawakustahili kupewa nyadhifa walizonazo ndani ya vyama vyao."
Ngawaiya alisema endapo baadhi ya vyama vinaona utaratibu uliopendekezwa kupata katiba mpya haufai, ni vyema vipeleke maoni na malalamiko kwenye mamlaka husika au kupitia mikutano ya kujadili katiba badala ya kufanya fujo, kuzomea au maandamano.
Taasisi hiyo imetoa wito kwa vyama vyote vya siasa na wananchi kuwa watulivu katika kipindi cha kukusanya maoni. Pia wameiomba serikali kuongeza muda wa ukusanyaji maoni.
NA MWANDISHI WETU
Gazeti la Uhuru
WAKATI CHADEMA ikitangaza kuanza maandamano ya nchi nzima kupinga muswada wa kuruhusu kuundwa tume ya kupokea maoni kuhusu katiba mpya, kuna taarifa kuwa chama hicho kimepanga kutumia wafuasi wa kikundi cha Mungiki kutoka Kenya kuhamasisha vurugu nchini.
CHADEMA pia inadaiwa kuandaa vijana wa Kitanzania 60,000 watakaoshirikiana na kikundi hicho kuwajenga kisaikolojia kushiriki kwa nguvu katika maandamano hayo.
Mkakati huo upo kwenye waraka (Uhuru ina nakala yake) uliosambazwa na uongozi wa juu wa chama hicho kwenda kwa makatibu wakuu wa CHADEMA katika mikoa ya Tanzania Bara.
Taarifa za kuaminika kutoka makao makuu ya chama hicho zilidai mpango huo utawapa ujasiri vijana kupitia wanaharakati hao kutoka Kenya.
"Tunapaswa kuwajengea uwezo wa kujiamini na kutosikiliza vitisho vinavyotolewa na serikali ili wawe tayari kushiriki kwenye maandamano,'' ilisema sehemu ya waraka huo kwenda kwa makatibu wakuu.
Waraka huo pia uliwataka makatibu wakuu kuhakikisha wanapata fedha za kutosha na kuziwasilisha makao makuu ili zitumike kuwalipa wanaharakati hao.
Alipoulizwa kuhusu habari hizo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema amepokea jalada la CHADEMA kuhusu maandamano lakini hajalisoma na kwamba leo atalitolea ufafanuzi.
"Jalada limefika mezani kwangu ila bado sijalisoma. Nitatoa ufafanuzi kuhusu maandamano hayo, hilo la Mungiki tutalifuatilia na tulitolea taarifa,'' alisema. Kwa upande wake, Mkuu wa Operesheni wa chama hicho, Benson Singo, alikana madai ya kushirikiana na kikundi cha Mungiki. Hata hivyo, alikiri kuwepo maandamano hayo, yatakayoanza Jumamosi katika mikoa 10.
"Kweli tuna maandamano yatakayohusisha viongozi wote wa kitaifa katika mikoa 10, lengo ni kupinga muswada wa maboresho ya katiba,'' alisema. Alisema maandamano hayo yatafanyika Arusha, Mbeya, Kigoma, Kilimanjaro, Ruvuma, Dodoma, Pwani, Mtwara, Tabora na Morogoro.
Katika hatua nyingine, Taasisi ya Demokrasia na Utawala Bora Tanzania (CEGODETA), imelaani tabia ya baadhi ya vyama vya siasa kupeleka vijana wahuni wa vijiweni kwenye midahalo ya katiba.
Inadaiwa vijana hao hupelekwa kwenye midahalo hiyo ili wakawazomee na kufanya fujo wakati wachangiaji wa vyama vingine wanapozungumza.
Mkurugenzi wa CEGODETA Thomas Ngawaiya alisema: "Tabia hiyo si ya kistaarabu na inaonyesha kuna baadhi ya vyama ambavyo viongozi wake bado hawajakomaa kisiasa, na wala hawakustahili kupewa nyadhifa walizonazo ndani ya vyama vyao."
Ngawaiya alisema endapo baadhi ya vyama vinaona utaratibu uliopendekezwa kupata katiba mpya haufai, ni vyema vipeleke maoni na malalamiko kwenye mamlaka husika au kupitia mikutano ya kujadili katiba badala ya kufanya fujo, kuzomea au maandamano.
Taasisi hiyo imetoa wito kwa vyama vyote vya siasa na wananchi kuwa watulivu katika kipindi cha kukusanya maoni. Pia wameiomba serikali kuongeza muda wa ukusanyaji maoni.