Gari yenye full time 4wd

Tricker

Member
Nov 26, 2010
95
25
Wadau kuna anaejua wapi au jinsi ya kubadilisha full time 4wd inaweza kubadilishwa kuwa 2wd?manake fuel inaenda si mchezo

Thanks
 
Nijuavyo ni kuwa kuna magari yanayotengenezwa kuwa na 4wd full time na kuna yale ya kizamani ambayo ili kupata 4wd inabidi uingize gear maalumu.
Magari ya kisasa hayana option ya kufanya gari isukume kwa kutumia matari ya upande mmoja, hata hivyo kinacho tafuna mafuta sio 4wd kwa magari ya kisasa bali ni ukubwa wa injini
 
Nijuavyo ni kuwa kuna magari yanayotengenezwa kuwa na 4wd full time na kuna yale ya kizamani ambayo ili kupata 4wd inabidi uingize gear maalumu.
Magari ya kisasa hayana option ya kufanya gari isukume kwa kutumia matari ya upande mmoja, hata hivyo kinacho tafuna mafuta sio 4wd kwa magari ya kisasa bali ni ukubwa wa injini

ni cc 1580,sidhani kama hii ni engine kubwa ila roughly inaenda 6km/litre!!
 
Kwa maelezo yako (1.6 Litre engine) haikutakiwa kuwa na ulaji wa mafuta mbaya. Labda uangalie mambo mawili.
1) Ifanyie service gari yako huenda ina matatizo
2) Angalia unavyoendesha gari, hapa ninamaanisha mambo kama vile kuondoa gari kwa kasi kubwa, kukanyaga sana mafuta n.k, ukiwa "dereve mpole" inasaidia sana kuokoa mafuta. Kama unayo manual ya gari soma zaidi kwani kampuni nyingi huandika kipengele cha namna ya kuokoa mafuta katika matumizi ya gari.
 
ni cc 1580,sidhani kama hii ni engine kubwa ila roughly inaenda 6km/litre!!
Mkuu cc 1580 mbona ni inji inayotumia mafuta kidogo kulinganisha na magari mengi yenye cc 2000?
sijui umejuaje inakula sana mafuta, lakini fuata ushauri wa mkuu https://www.jamiiforums.com/members/tricker.html Millah kwa kufanyia sevisi na hakikisha umebadilisha nozeli maranyingi zikiwa zimechoka gari hula mafuta kuliko kawaida.
 
Kwa maelezo yako (1.6 Litre engine) haikutakiwa kuwa na ulaji wa mafuta mbaya. Labda uangalie mambo mawili.
1) Ifanyie service gari yako huenda ina matatizo
2) Angalia unavyoendesha gari, hapa ninamaanisha mambo kama vile kuondoa gari kwa kasi kubwa, kukanyaga sana mafuta n.k, ukiwa "dereve mpole" inasaidia sana kuokoa mafuta. Kama unayo manual ya gari soma zaidi kwani kampuni nyingi huandika kipengele cha namna ya kuokoa mafuta katika matumizi ya gari.

Sawa mkuu ntazingatia hiloo swala la service though kuhusu kuendesha najitaidi kuwa mpole sana,sema nna implication kwamba labda kitendo cha gari kuwa ''full time 4wd'' inaweza kuongeza ulaji wa mafuta richa ya kuwa ni cc 1.6
 
Mkuu cc 1580 mbona ni inji inayotumia mafuta kidogo kulinganisha na magari mengi yenye cc 2000?
sijui umejuaje inakula sana mafuta, lakini fuata ushauri wa mkuu https://www.jamiiforums.com/members/tricker.html Millah kwa kufanyia sevisi na hakikisha umebadilisha nozeli maranyingi zikiwa zimechoka gari hula mafuta kuliko kawaida.

Nilijaza mafuta full tank,nikaweka zero km then mshale ilipoonesha umefika nusu tanki nikajaza tena nijue lita halisi zilizoingia afu nikagawanya kwa km gari iliyotembea ndo nikapata 6.smthing km/lt,au hii sio njia sahihi?
 
Nilijaza mafuta full tank,nikaweka zero km then mshale ilipoonesha umefika nusu tanki nikajaza tena nijue lita halisi zilizoingia afu nikagawanya kwa km gari iliyotembea ndo nikapata 6.smthing km/lt,au hii sio njia sahihi?
Mkuu kwani gari yako ni aina gani then tunaweza jua specification na fuel consumption yake.
Njia uliyotumia inategemea, kumbuka unapokuwa katika foleni speed meter inakuwa imesimama na mafuta yanaendelea kulika kama kawa.
posta to tabata ni mwendo wa nusu saa, lakini utatumia masaa matatu kwenye foleni sidhani kama hapa utapata majibu sahihi kwa km/lt
 
Mkuu kwani gari yako ni aina gani then tunaweza jua specification na fuel consumption yake.
Njia uliyotumia inategemea, kumbuka unapokuwa katika foleni speed meter inakuwa imesimama na mafuta yanaendelea kulika kama kawa.
posta to tabata ni mwendo wa nusu saa, lakini utatumia masaa matatu kwenye foleni sidhani kama hapa utapata majibu sahihi kwa km/lt

Nimekuelewa sana Paulss kweli lazima kutake into consideration foleni na AC pia
 
Back
Top Bottom