Gari lisipotumika nini madhara yake?

Gari lisipotumika nini madhara yake?

Daddo

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2013
Posts
1,435
Reaction score
1,025
Habari zenu wakuu!
Samahanini jamani naomba mwenye kujua anisaidie yafuatayo;

> Endapo gari langu nitaliacha kwa muda mrefu bila kulitumia je kuna matatizo ambayo yanaweza kujitokeza?

> Kama jibu la hapo juu ni ndiyo je inatakiwa liwe angalau linawashwa na kuendeshwa kila baada ya muda gani na liendeshwe at least umbali gani?

Natanguliza shukrani kwenu.
 
Kama hulitumii si uliuze? Kwanini kukaa na pambo?

Ni dharura tu ambapo imenibidi kusafiri kwa muda flani. Si kweli kwamba gari lipo kama pambo. Nalipenda sana ndiyo maana sijafikiria kuliuza.
 
Mmh! Aku hil haliniusu maan cna hat mkokoten wa kubeba maji!
 
Liweke sehemu nzuri na salama toa betri yake utalikuta poa, hasa kama unarudi baada ya siku si nyingi.
 
Likikaa muda mrefu laweza kuwa na kutu (rust) kwenye baadhi ya vitu muhimu kwakuwa humidity (amount of water vapor in the air) inaweza kuingia kwenye vyuma vya gari. Kumbuka kutu (rust) reaction of iron and oxygen in the presence of water or air moisture eg. humidity. Kwahiyo mkuu kuliacha muda mrefu huenda ukaja ukaingia gharama kubwa kubadili baadhi ya vipuri hasa ambayo vinaweza vikawa exposed easly na humidity. Hakikisha japo linawashwa hata kwa robo saa au zaidi japo salience hata kwa wiki mara mbili sio mbaya. Ila likitembea hata kama ni mita 20 sio mbaya ili mradi kila kifaa kiwe in rotation hususani kwa vile ambavyo vina rotate.
Ni ushauri wangu tu according to different engines I have met in my site.
 
Kama ni wiki 1 au 2 basi toa battery au la mtu aliwashe after atleast 3days. Kama ni muda mrefu hakikisha unaacha mtu wa kiwasha na kuendesha mara kwa mara. Langu niliacha kama 4 months nakuja baadae kurekebisha starter, battery, gearbox na matairi... Ilini cost vibaya mno..
 
Mmh! Aku hil haliniusu maan cna hat mkokoten wa kubeba maji!

Siyo kweli kwamba kama huna gari ndiyo hata uelewa unakuwa hauna. Inawezekana ukawa haunalo ila unajua mambo kuzidi hata wamiliki wa magari.
Hata kama hujui unaweza pia kujifunza kitu hapa kikakusaidia mbeleni. Kumbuka hakuna aliyezaliwa na gari kutoka tumboni kwa mamaye. Ni vitu vinatafutwa na vinapatikana tena hakuna aliyezaliwa akaandikiwa kuwa na gari au asiwe nalo. Hivyo nakukaribisha kwa ushauri au hata kusoma comments za watu uongeze maarifa.
 
Likikaa muda mrefu laweza kuwa na kutu (rust) kwenye baadhi ya vitu muhimu kwakuwa humidity (amount of water vapor in the air) inaweza kuingia kwenye vyuma vya gari. Kumbuka kutu (rust) reaction of iron and oxygen in the presence of water or air moisture eg. humidity. Kwahiyo mkuu kuliacha muda mrefu huenda ukaja ukaingia gharama kubwa kubadili baadhi ya vipuri hasa ambayo vinaweza vikawa exposed easly na humidity. Hakikisha japo linawashwa hata kwa robo saa au zaidi japo salience hata kwa wiki mara mbili sio mbaya. Ila likitembea hata kama ni mita 20 sio mbaya ili mradi kila kifaa kiwe in rotation hususani kwa vile ambavyo vina rotate.
Ni ushauri wangu tu according to different engines I have met in my site.

Asante sana mkuu kwa maelezo yako.
 
Likikaa muda mrefu laweza kuwa na kutu (rust) kwenye baadhi ya vitu muhimu kwakuwa humidity (amount of water vapor in the air) inaweza kuingia kwenye vyuma vya gari. Kumbuka kutu (rust) reaction of iron and oxygen in the presence of water or air moisture eg. humidity. Kwahiyo mkuu kuliacha muda mrefu huenda ukaja ukaingia gharama kubwa kubadili baadhi ya vipuri hasa ambayo vinaweza vikawa exposed easly na humidity. Hakikisha japo linawashwa hata kwa robo saa au zaidi japo salience hata kwa wiki mara mbili sio mbaya. Ila likitembea hata kama ni mita 20 sio mbaya ili mradi kila kifaa kiwe in rotation hususani kwa vile ambavyo vina rotate.
Ni ushauri wangu tu according to different engines I have met in my site.

Ilishawahi nitokea exactly kama hivyo, gari ilikufa betri, nikasafiri kwa miezi kama nane, niliporudi badala ya kununua betri peke yake (kama laki na ishirini) nikatumia zaidi ya milioni na nusu kuirudisha sawa.

Hizi engine za siku hizi zina vitu vingi vya automatic, kurekebisha hewa inayoingia kwenye engine, mafuta, silence, air condition na kadhalika, vikipata kutu kidogo tu gari linasumbua mbaya.

Nakushauri kama utakaa zaidi ya miezi mitatu, tafuta mtu wa kuliwasha na kulitembeza kidogo, hata mara moja kwa wiki, ukirudi fanya full service kisha piga misele kama kawa. Usidharau ndugu yangu yameshanikuta!
 
Ilishawahi nitokea exactly kama hivyo, gari ilikufa betri, nikasafiri kwa miezi kama nane, niliporudi badala ya kununua betri peke yake (kama laki na ishirini) nikatumia zaidi ya milioni na nusu kuirudisha sawa.

Hizi engine za siku hizi zina vitu vingi vya automatic, kurekebisha hewa inayoingia kwenye engine, mafuta, silence, air condition na kadhalika, vikipata kutu kidogo tu gari linasumbua mbaya.

Nakushauri kama utakaa zaidi ya miezi mitatu, tafuta mtu wa kuliwasha na kulitembeza kidogo, hata mara moja kwa wiki, ukirudi fanya full service kisha piga misele kama kawa. Usidharau ndugu yangu yameshanikuta!

Siwezi kudharau ushauri ninaopewa mkuu. Hiki ndicho nilichokifuata hapa. Asante sana kwa ushauri wako.
 
Siyo kweli kwamba kama huna gari ndiyo hata uelewa unakuwa hauna. Inawezekana ukawa haunalo ila unajua mambo kuzidi hata wamiliki wa magari.
Hata kama hujui unaweza pia kujifunza kitu hapa kikakusaidia mbeleni. Kumbuka hakuna aliyezaliwa na gari kutoka tumboni kwa mamaye. Ni vitu vinatafutwa na vinapatikana tena hakuna aliyezaliwa akaandikiwa kuwa na gari au asiwe nalo. Hivyo nakukaribisha kwa ushauri au hata kusoma comments za watu uongeze maarifa.

bahati mbaya natumia opera browser. pokea like hiyo kiongozi kwa namna ulivyojibu hoja ya mdau.
wengine wakipata response kama hizo ndo na matusi na kebehi huanza
 
bahati mbaya natumia opera browser. pokea like hiyo kiongozi kwa namna ulivyojibu hoja ya mdau.
wengine wakipata response kama hizo ndo na matusi na kebehi huanza

Wewe unatumia opera version gani? Mbona like button ipo? Like iko katika website na sio browser. Usiwanyime tu watu haki yao fungua desktop version ya jamiiforums utapata like.
 
Kuegesha muda mrefu kunaweza kuharibu gari lako ikiwa tahadhari haitachukuliwa:-
(1)Battery...ifungue isiwe imeungwa kwenye mfumo. Hakikisha haiishiwi charge.
(2)Engine iwashwe angalau mara mbili kwa mwezi na kuachwa iungurume japo kwa dakika kumi hadi nusu saa.
(3)Gari itembezwe angalau mara moja kwa mwezi au miezi miwili ili kusambaza oil na grease kuzuia kutu na kukauka kwa seal.
(4)Paka grease kwenye terminal za battery pamoja na vichwa vya nyaya za battery, vitasa, na maeneo yenye movement.
Ukiweza fanya mwenyewe au tumia mtu mwenye uwezo wa kufanya hayo
 
Back
Top Bottom