Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Gari la wizi lanaswa likiwa na mabango ya picha za Masha
Jeshi la Polisi la Polisi Mkoani Mwanza limekamata gari moja la wizi kutoka nchini Kenya likiwa na mabango ya picha za mgombea ubunge jimbo la Nyamagana jijini Mwanza, ambaye pia ni waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha.
Gari hilo aina ya Rav4 lilikamatwa Septemba 29 mwaka huu majira ya saa 7 mchana, katika kituo cha kuoshea magari kilichopo barabara ya Makongoro jijini hapa, ambapo ilikuwa limeibiwa na watu wasiojulkana jijini Nairobi, nchini Kenya.
Kaimu kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Nonosius Komba aliwaambia waandishi wa habari jana ofisini kwake kuwa gari hilo liliingia nchini siku hiyo hiyo (sept 29) likiwa na namba bandia za T 274 ACM.
Kamanda Komba alisema gari hilo ni mali ya Peter Nisiah wa jijini Nairobi, namba zake halisi ni KBK 222 A, na kwamba kukamatwa kwake kulitokana na mawasiliano ya Satelaiti kati ya jeshi la polisi Mwanza na Nairobi Kenya……..
…………Alisema namba hizo za bandia zilizotumiwa na ambazo zipo hadi sasa hivi kwenye gari hilo la wizi zinaonekana kwenye kumbukumbu ni gari moja aina ya Toyota Mac III lenye injini Na. IAZ4483564 linalomilikiwa na raia wa Kichina aliyetajwa kwa jina la Young Fredyong anayeishi jijini Dar es Salaam.
Alipoulizwa kuhusu kuwepo kwa mabango ya kampeni ya picha za Waziri Masha yaliyobandikwa kwenye gari hilo la wizi, kamanda Kova aling'aka na kukataa kuzungumzia juu ya mabango hayo.
"Usiniulize suala la mabango ya waziri Masha kuwepo kwenye gari hilo, wewe tambua tu kwamba tumelikamata, sisi hatujui hayo mabango yapo kwa minajili ipi," alisema kwa ukali.
Gazeti hili lilishuhudia kuwepo kwa picha moja ya Masha ambayo imebandikwa mbele ya gari hilo la wizi, huku mabango kadhaa yakiwa yamewekwa ndani ya gari hilo karibu na kiyoo cha mbele.
Waziri Masha alipotafutwa kuzungumzia hali hiyo ya kuwepo kwa mabango ya picha zake katika gari hilo la wizi hakuweza kupatikana mara moja.
Chanzo: Tanzania Daima.
Ni proof ya kile Dr slaa alichokisema akiwa Arusha, kwamba CCM ni kichaka cha wahalifu. Wahalifu wengi, wakiwemo majambazi, wanyang'anyi, wauaji wa albino, wizi wa magari etc hujificha nyuma ya pazia la CCM. Wanaoweka bendera za CCM kwenye sehemu zao za biashara wanaficha maovu. Hata muendesha daladala au texi akibandika picha ya JK utakuta gari hilo lina makosa kibao etc.
Kitu kinachoshangaza ni kwamba huyo RPC Komba kwa nini hakuyanyofoa hayo mabango ya 'mwajiri' wake kutoka kwenye gari kabla ya kuita waandishi wa habari? Hivi anafikiria bado kibarua anacho?
Wandugu hebukuweni makini kwani bango linahusiananini na ubiwaji wa hilo gari mbona mama lishe wanabandika kwenyemabenchi hapa igoma tunatandikiwa mabango ya dk silaa tunakalia wakati mengine ya masha tumewekewa juu kamakinga tusipatwe na jua hamkuona ajabu mabango yanagawiwa bure hayana uzibitwaji huyo alitumia janja ya nyani kulamaihindi mabichi lakini kumbe wenzake wapo zaid jamani tuwe na busara tusichukulie mpaka tukawa na chuki kiasi hicho
Hakuna siasa hapa ni uhalifu tu, hata kama Chadema wangekua madarakani, wezi wangetumia mabango ya kampeni kupita vikwazo vya polisi; Nafahamu hata maeneo yenye mageti ya polisi jamaa wanapamba gari na mabango ya "chagua Kikwete" na wengine huweka hata loud speaker na kupita kilaini!??? Ss kazi kweli kweli, usishangae hata magari ya polisi ama ya zimamoto na ambulance kutumika katika uhalifu. Lakni tusishangae pia ikawa mhusika anafanya kweli kampeni kumsaidia jamaa maana wahalifu nao ndio kipindi cha kujisogeza na pia anaweza kuwa mtu inocent akaingizwa mkenge na majizi akauziwa gari la wizi maana fedha za CCM huwa zinawafanya watu wehu na wahalifu hutumia nafasi hiuyo kujinufaisha. Tunakumbuka wakati wa operesheni ya kamata ya magari ya wizi toka Afrika Kusini, mengi yaliyokamatwa yalikua ya vigogo na wafanyabiashara maarufu. Kwa hiyo hili tukio ni alama ya jambo kubwa zaidi.siasa balaa