mkute
Member
- Jan 12, 2011
- 80
- 12
Jamani naomba ufafanuzi kama sheria inaruhusu gari la serikali kama linavyooneka katika picha kutengenezwa pindi linapoharibika katika karakana ya moja ya wawekezaji wakubwa katika sekta ya uwindaji nchini,ambayo hivi karibuni iliwahi kuhusishwa na tuhuma za kuhonga gari kwa Dc mmoja wa wilaya iliyopo kanda ya ziwa na kupelekea wananchi kuchomewa nyumba zao na polisi eti kuwalazimisha kuhama katika maeneo ambayo inadaiwa kuwa ni sehemu ya hifadhi,jambo lilopelekea mbunge wa wananchi hao kulisemea bungeni mwaka huu na kutakiwa kupeleka ushahidi na mh. spika.
Gari hili ambalo inasemekana lipo ndani ya garage ya kampuni hiyo inasemekana limetoka wilaya husika, swali langu ni je hizi ndio fadhila za wawekezaji kwa serikali? kama sivyo inamaana serikali haina pesa za kukarabati hata magari yake kiasi cha kuishiwa hata matairi kama inavyoonyesha katika gari hili ikitegemea wawekezaji?
Tunakwenda wapi kwa mtindo huu kweli serikali yetu itakuwa na sauti ya kutetea wananchi wake au itatetea wawekezaji wanaoifadhili namna hii?,naomba kutoa hoja!