Gari inaungua muda huu maeneo ya Makumbusho

Gari inaungua muda huu maeneo ya Makumbusho

Davetz

Member
Joined
Dec 21, 2013
Posts
49
Reaction score
16
Wakuu nimepita eneo la Makumbusho muda huu na kukuta kuna gari inawaka moto pale jirani na ile restaurant iliyoko pembezoni mwa barabara. Kwa kuwa nilikuwa ndani ya gari sikuweza kupata taarifa kamili juu ya gari lile nini kilisababisha liungue na kama kuna majeruhi wowote.
Mwenye taarifa zaidi atujuze !!!!
 

Attachments

  • 1419863144221.jpg
    1419863144221.jpg
    33.3 KB · Views: 4,354
  • 1419863162529.jpg
    1419863162529.jpg
    52.3 KB · Views: 4,324
Wakuu nimepita eneo la makumbusho muda huu na kukuta kuna gari inawaka moto pale jirani na ile restaurant iliyoko pembezoni mwa barabara. Kwa kuwa nilikuwa ndani ya gari sikuweza kupata taarifa kamili juu ya gari lile nini kilisababisha liungue na kama kuna majeruhi wowote.
Mwenye taarifa zaidi atujuze !!!!

...mkuu 'Davetz' Asante kwa taarifa!
 
Mh hapakua na dalili za tukio fulani? na watu hawajakuwapo mahali hapo
 
Pole sana kwa mhanga, hivi naweza kupata wapi elimu ya uhakika kuhusu aina na faida za bima mbalimbali kama vile magari na nyumba? maana mawakala wa bima walio wengi wanashindwa kutoa elimu hii sijajua ni kutokana na nini mpaka wanashindwa kutoa elimu vilivyo, nimewatembelea baadhi wanakuahidi njoo kesho, ukienda hiyo kesho humkuti anamwachia secretary wake maelekezo yasiyokidhi kiu.
 
ukute ni gari la mkopo na bado hajamaliza kulipa, atapagawa, pole yake.
 
Natamani lingekuwa na mtu ndani ili atutumie picha za ndani wakati linaungua...
 
Natamani lingekuwa na mtu ndani ili atutumie picha za ndani wakati linaungua...

Hahahaaa, mkuu, sidhani kama kuna kiumbe mwenye ujasiri wa namna hiyo, badala ajiokoe eti apige picha kwa ajili ya wanJF...hilorious
 
hilo lilikua chuma chakavu si unaona hata alina rim, au na rim zimeungua zimeisha
 
Pole sana kwa mhanga, hivi naweza kupata wapi elimu ya uhakika kuhusu aina na faida za bima mbalimbali kama vile magari na nyumba? maana mawakala wa bima walio wengi wanashindwa kutoa elimu hii sijajua ni kutokana na nini mpaka wanashindwa kutoa elimu vilivyo, nimewatembelea baadhi wanakuahidi njoo kesho, ukienda hiyo kesho humkuti anamwachia secretary wake maelekezo yasiyokidhi kiu.

1.third party-ukipata ajali analipwa uliemgonga endapo wewe una makosa ila wewe hutalipwa.
2.third party,fire and theft-hii kama hio hapo juu ila unalipwa iwapo gari itaungua au kuibiwa
3.comprehensive-hii unalipwa ukipata ajali[aidha una makosa au huna],gari ikiibiwa,gari ikiungua moto.
kama unataka peace of mind uwe na bima hio no.3

nb/;terms and conditions apply.....soma vi maandishi vidogo kwa umakini sana.
 
1.third party-ukipata ajali analipwa uliemgonga endapo wewe una makosa ila wewe hutalipwa.
2.third party,fire and theft-hii kama hio hapo juu ila unalipwa iwapo gari itaungua au kuibiwa
3.comprehensive-hii unalipwa ukipata ajali[aidha una makosa au huna],gari ikiibiwa,gari ikiungua moto.
kama unataka peace of mind uwe na bima hio no.3

nb/;terms and conditions apply.....soma vi maandishi vidogo kwa umakini sana.

Hivi comprehensive hata kama makosa yako unalipwa? Fr example umegonga gari yako ukutani?
 
Hivi comprehensive hata kama makosa yako unalipwa? Fr example umegonga gari yako ukutani?

common sense ina apply ukipata 'ajali'.....kugonga ukutani makusudi sio ajali....ni fraud/suicide/sabotage etc

kupata ajali unaweza kuwa na makosa wewe au derevaa mwingine,vile vile unaweza kugonga ukuta au mti kwa bahati mbaya ni 'ajali' utalipwa ila ukiwa na third party hulipwi.....ndio ajali
 
common sense ina apply ukipata 'ajali'.....kugonga ukutani makusudi sio ajali....ni fraud/suicide/sabotage etc

kupata ajali unaweza kuwa na makosa wewe au derevaa mwingine,vile vile unaweza kugonga ukuta au mti kwa bahati mbaya ni 'ajali' utalipwa ila ukiwa na third party hulipwi.....ndio ajali

OK, na ukigonga ukuta bahati mbaya kwako, unamuita traffic apime??? Na ipi company ya bima ambayo haina usumbufu kulipa?
 
OK, na ukigonga ukuta bahati mbaya kwako, unamuita traffic apime??? Na ipi company ya bima ambayo haina usumbufu kulipa?

ili kulipwa lazima traffic apime na atoe ripoti ya ajali. ripoti hio ndio itatumiwa na watu wa insurance kuamua unastahili kulipwa au la.....ukipata ajali na unahitaji bima wakulipe usitoe gari mpaka trafiki wapime....siku hizi competition kubwa kampuni nyingi hazina usumbufu kulipa......ukienda kwa broker ana list ya kampuni nyingi atakuchagulia ila kuwa makini na hawa brokers.
 
Back
Top Bottom