PreGE2025 G55 Henry Kileo, Moza Ally, Patrick Assenga, Asha Abubakari na Glory Tausi wajiondoa CHADEMA

PreGE2025 G55 Henry Kileo, Moza Ally, Patrick Assenga, Asha Abubakari na Glory Tausi wajiondoa CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
2,786
Reaction score
7,567
Wakuu,

Ni mwendo wa kuendelea kuangalia panapovuja mpaka iache kunyesha.


View: https://www.youtube.com/live/7DyNX31-xaQ?si=rDbUhzxMfwptm2Q-

1747214802453.png


Meza Kuu inajumuisha;



Henry Kileo - Mwenyekiti CHADEMA Mkoa wa Kinondoni - Nimekaa kwenye chama kwa uaminifu sana, lakini chama sasa kimepoteza muelekezo wa kiongozi, demokrasia hamna, na haya yametokea baada ya G55 kutaka kutoa maoni yetu. Sisi ni waasisi wa G55, Katibu Mkuu alituaita kwaajili ya No Reforms No Election, tukaunda group la watsap ili twende kushauri, tulieleza faida na hasara za kampeni hiyo na kushauri tushiriki uchaguzi na kuzuia uchaguzi tukiwa washiriki. Lakini tukaanza kuitwa wasaliti na kupangiwa mikakati ya kufukuzwa na matawi ya chama. Chuki hii inaendelezwa na baadhi ya viongozi wa kamati kuu. Natangaza rasmi nimejivua uachanama CHADEMA, nimefanya hivyo ili kwenda kutafuta jukwaa lingine la kuwatumikia wananchi kisiasa, nna uhakika jukwaa ntakalolipata nitalitumia vizuri. Natafuta Jukwaa lininge ambalo si CCM, ntawajulisha baadaye naenda jukwaa gani kwaajili ya kuendeleza mapigano.

Patrick Assenga - Mwenyekiti Jimbo la Segerea, Mweka Hazina Kanda ya Pwani
Nimewahi kuwa mbunge na diwani, na kukipigania chama kwelikweli, CHADEMA ilikuwa chama cha mapambano tulikuwa hatuogopi kitu, kulikuwa na demokrasia na kila mtu alikuwa anaweza kuongea na kushauri chochote, lakini toka uongozi mpya uingie haturusiwa wala kuhoji, ukifanya hivyo unaitwa msaliti. Kama alivyosema Kileo tulianzisha G55 kwa malengo ya kushauri chama kushiriki uchaguzi na si kukwepa, tukae chini na kutengeza mkakati wa kuwashinda CCM na si kuwakimbia. Kati ya sisi tunaotaka kupambamana na CCM nao wanaotaka kukimbia nani kahongwa? Leo Mei 14, 2025 natangaza rasmi kujivua uanachama CHADEMA na kuachia nafasi zangu zote. Tunaenda kuendeleza harakati kwengine, na hii ni nchi nzima na wanachama wengine ambao wapo nyuma yetu

Moza Ally - Makamu Mwenyekiti BAVICHA
Siasa na katiba ipo katika mfumo wa vyama vingi na mustakabali wa nchi yetu unatokana na siasa, mwanzo nilikuwa naunga mkono No Reforms No Election, baada ya kutafakari sana nimeona chama kimekosa kunipa mbinu halisi ya kwenda kuzuia uchaguzi. Nimeona nisisaliti dhamira ya kweli ya kuwasema watanzania kwenye vyombo halisi vya maamuzi, nitafute jakwaa lingine la kisiasa kuwasemea watanzania. Nitakapokwenda kwenye jukwaa jingine la kisiasa na tutaposema tunapoelekea ninaomba mniunge mkono. Natangaza rasmi kujivua uanachama wangu CHADEMA

Glory Tausi - Mwanzilishi wa CHADEMA Digital, Mtiania Jimbo la Morogoro Kusini
La kutoshiriki uchaguzi kwangu halijakaa sawa, kwenda kuzuia uchaguzi tunazuia na kumnyima raia haki yake ya kupiga kura na kuchaguliwa kama amekidhi vigezo vya kuchaguliwa. Suala hili kwangu limekuwa gumu na siko tayari kushiriki dhambi ya kumzuia raia kushiriki kwenye uchaguzi. Pia umoja, amani na demokrasia ambayo tumezoea ndani ya chama vimepungua au kuondoka kabisa, na hii imetukuta zaidi kwa sisi ambao tulikuwa tunamsapoti Mbowe. Nimejivua uanachama CHADEMA

Asha Abubakari - Katibu CHADEMA Wilaya ya Segerea, Mjumbe Baraza Kuu Tiafa, Mjumbe Kamati Kuu Taifa.
Nimekulia kwenye familia ya wapinzani, nimesomeshwa kwa pesa ya CHADEMA, na malengo yalikuwa nije kupila fadhila kwa chama lakini chama sasa hivi hakifuati Katiba, hatuwezi kuendesha chama kwa matamko. Unawezaje kuzuia uchaguzi wakati hauna silaha yoyote ya kupambana? Viongozi wetu wa juu wameongea sana kuhusu No Reforms No Election lakini hawajawahi kusema madhara ya kutokuwepo uchaguzi, ili watanzania wenyewe wapime. Chama cha siasa kinaenda na upepo, tulikuwa tunamsema Lowassa lakini 2015 alikuwa mgombea wetu, Lissu alipokamatwa maaskari hawakuzidi 20 lakini Watanzania hawa hawa walibaki kuangalia, hawakuweza kuzuia. Wanzania hawa tunaowategemea kwenda kuzuia uchaguzi bado hawapo tayari, naona chama changu kinaenda nje ya malengo. Najivua uanachama CHADEMA na nafasi zote nilizokuwa nashikilia
 

View: https://www.youtube.com/watch?v=7DyNX31-xaQ


Henry John Kilewo, Mwenyekiti wa CHADEMA Kinondoni, atangaza kujivua Uanachama


Henry John Kilewo: Naondoka CHADEMA tukutane kwenye jukwaa lingine, siendi kuanza upya

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa kichama wa Kinondoni, Henry Kilewo, ametangaza kujiondoa rasmi ndani ya chama hicho, akitaja kupotea kwa mwelekeo wa kiuongozi na uminywaji wa demokrasia ya ndani kama sababu kuu ya uamuzi wake.

Kilewo, ambaye pia ni mmoja wa waanzilishi wa kundi la G-55 ndani ya chama hicho, amesema hatua hiyo inatokana na kile alichokiita kuvunjika kwa misingi ya maadili ya chama, kukithiri kwa vitendo vya kulipiza visasi dhidi ya wanachama waliotoa maoni ya tofauti, na kukosekana kwa mazingira ya usawa wa kidemokrasia.

“Chama kama kimepoteza mwelekeo wa kiuongozi, kimepoteza mwelekeo wa kutovumiliana kidemokrasia. Haya yalionekana wazi baada ya sisi G-55 kutoa mapendekezo,” amesema Kilewo akizungumza na waandishi wa habari siku ya Jumatano mkoani Dar es Salaam.

Ameeleza kuwa badala ya chama kuangalia hoja zilizotolewa kwa nia ya kujenga, viongozi wa juu waliibuka na kampeni za wazi za kuwashambulia na kupanga mikakati ya kuwaondoa wale waliokuwa na mitazamo tofauti, akisema hata Mwenyekiti wa sasa wa chama aliwahi kuenda majukwaani na “kukinanga chama chake mwenyewe”.

Kilewo ameongeza kuwa kinachoendelea sasa ndani ya chama hicho kinaashiria uwezekano wa hali kuzidi kuwa mbaya kwa viongozi waliobaki, akisema: “Kwa kasi hii, ipo siku tutakuta hata Mwenyekiti wa chama amefukuzwa chama. Hii ndiyo hali halisi iliyopo.”

Akieleza kujiondoa kwake CHADEMA, Kilewo amesema: “Nimetafakari sana, na nimekubaliana na nafsi yangu kuwa dhana iliyonivutia kujiunga na CHADEMA haipo tena. Kwa hiyo leo ninatangaza kujiondoa rasmi, na si mwanachama wa CHADEMA tena, wala kiongozi wa chama hicho.”

Hatua hiyo ya Kilewo inakuja siku chache tu baada ya Tawi la CHADEMA Kisutu kumwandikia barua ya wito wa kujieleza, likimtuhumu kwa kuhujumu shughuli halali za chama, usaliti, na kuendesha kampeni za kuwashawishi wanachama kuondoka.

Katika barua hiyo ya Mei 11, 2025, iliyosainiwa na Katibu wa tawi hilo, Anaely Sarakikya, Kilewo alitakiwa kuwasilisha maelezo ya maandishi ndani ya siku 14 juu ya tuhuma zinazomkabili. Barua hiyo inadai kuwa Kilewo amekuwa kinara wa “usambazaji wa mabango ya mikutano ya waandishi wa habari inayoratibiwa kwa nia ovu ya kushawishi wanachama na viongozi wa CHADEMA kuhama chama.”

Kwa sasa bado haijajulikana kama Kilewo atajibu barua hiyo au la, lakini uamuzi wake wa kujiondoa rasmi unaweza kuwa umejibu hoja hiyo kwa vitendo.

=====================

CHADEMA INAONGOZWA KWA UOGA
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Jimbo la Segerea na Mhasibu wa Kanda ya Pwani, Patrick Assenga, ametangaza kujivua nyadhifa na kujiondoa rasmi ndani ya chama hicho akilalamikia kile alichokiita kukatishwa tamaa kwa watu wanaotoa ushauri na kukandamizwa kwa demokrasia ya ndani ya chama.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam siku ya Jumatano, Assenga amesema hali ndani ya chama imebadilika mno tangu uongozi mpya wa juu ulipoingia madarakani, huku wakosoaji wakibandikwa majina kama “wasaliti”, “waliopokea rushwa” au “waliohongwa”.

“Tumeshangaa, baada ya uongozi mpya kuingia haturuhusiwi tena kuhoji. Ukishauri jambo unaitwa msaliti, unaitwa umehongwa, unaitwa umepewa pesa. Sisi tulianzisha G-55 kwa malengo ya kushauri chama,” amesema Assenga.

Akiwa mmoja wa waanzilishi wa kundi la G-55 ndani ya CHADEMA, Assenga amesema kundi hilo lililenga kuibua hoja za maboresho ya chama, lakini sasa linatazamwa kama tishio.

Assenga pia amewataja kwa majina baadhi ya viongozi wa juu wa CHADEMA, akiwemo Mjumbe wa Kamati Kuu, Godbless Lema, na Makamu Mwenyekiti Bara, John Heche, akidai wamekuwa wakihusishwa na biashara zisizoeleweka huku wakishindwa kujibu hoja za msingi wanazotakiwa kueleza kwa wanachama.

“Lema amesema hawa watu wamepewa milioni mia. Nafikiri amezoea hizi biashara ambazo wao na Makamu wamekuwa wakifanya. Tumeshazungumza mara kadhaa, tumemwambia Mheshimiwa Heche ajitokeze atueleze magari anayomiliki, ameyatoa wapi, na mahusiano yake na baadhi ya mawaziri,” amesema kwa ukali.

Assenga ameongeza kuwa chama sasa kinaendeshwa kwa woga, na kimekosa mwelekeo wa wazi wa kisiasa, akisema hali hiyo imemlazimu kuchukua hatua ya kujiondoa.

“Wamekuwa waoga. Chama kimekosa mwelekeo. Chama hiki hakiwezi kwenda mbele. Najivua uanachama, naachia uhasibu wa Kanda na uenyekiti wangu wa Segerea,” ametangaza rasmi mbele ya wanahabari
 
Ripoti ya CAG ya 2025/2026, inawza. Kuja na taarifa ya matrilioni kutojulikana yalivyotumika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom