Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,096
- 828,939
Unajisikiaje ikiwa moyo wako una huzuni?
Kausha macho yako mwenyewe ili kufuta machozi ya mwingine
Katika ulimwengu huu mzuri kuna mabehewa mengi
Mengine yamebeba roho zilizovaa mavazi meusi zaidi.
Nafsi zilizopigwa na ukiwa , sononi na kukata tamaa, zingine zikiomboleza wafu wao,
matumaini yaliyokufa, furaha iliyokufa, miaka iliyokufa,
Kipofu anayetamani kuona nyota ambayo kila usiku wa manane hung'ara
Kiziwi anayetamani kusikia wimbo unaofurahisha kila asubuhi.
Toa chakula mahali ambapo mioyo yenye njaa inapigana na amri ya hatima;
Pumzika mahali ambapo mikono na miguu imechoka! Yape lesi macho yaliyojaa machozi
Imba ala zenye kuamsha hisia wape furaha, na furaha itakuvika taji la utu na kukuenzi
Umechaguliwa wewe kati ya wote.. Simama, nenda katende! Uwape furaha
Uwape tumaini jipya! Uwape faraja



Sent using Jamii Forums mobile app
Kausha macho yako mwenyewe ili kufuta machozi ya mwingine
Katika ulimwengu huu mzuri kuna mabehewa mengi
Mengine yamebeba roho zilizovaa mavazi meusi zaidi.
Nafsi zilizopigwa na ukiwa , sononi na kukata tamaa, zingine zikiomboleza wafu wao,
matumaini yaliyokufa, furaha iliyokufa, miaka iliyokufa,
Kipofu anayetamani kuona nyota ambayo kila usiku wa manane hung'ara
Kiziwi anayetamani kusikia wimbo unaofurahisha kila asubuhi.
Toa chakula mahali ambapo mioyo yenye njaa inapigana na amri ya hatima;
Pumzika mahali ambapo mikono na miguu imechoka! Yape lesi macho yaliyojaa machozi
Imba ala zenye kuamsha hisia wape furaha, na furaha itakuvika taji la utu na kukuenzi
Umechaguliwa wewe kati ya wote.. Simama, nenda katende! Uwape furaha
Uwape tumaini jipya! Uwape faraja




Sent using Jamii Forums mobile app