Teknolojia ni Yetu sote
JF-Expert Member
- Apr 28, 2020
- 1,221
- 2,425
๐ก Imepita zaidi ya miaka 112 toka friji la kwanza kugunduliwa Mnamo mwaka 1913 kupitia kwa jamaa mmoja mmarekani anaitwa Fred W Wolf ndo alikua mtu wa kwanza kugundua jokofu la umeme lenye kutoa barafu.
๐ Lakini Rasmi yakaanza kuingia sokoni mwaka 1918, ilipofika mwaka 1956, ma friji ya gharama yakaanza kutengeneza yakiwa na muundo wa kipekee sana.
Waliweza kutengeneza friji kama Magari ya kifahari, muundo unayoiona kwenye video ulikua wa kipekee sana ndani Kuna shelving inayoweza kubadilishwa, sehemu ya kuhifadhi mbogamboga, muundo wa kukunjwa kunjwa kuhifadhi vitu.
Kwa Tanzania mtu watu wa Mwanzo kutumia friji walikua wazanzibar miaka ya 1960s ๐ฅ
Mpaka Leo hii friji imekua sehemu moja wapo muhimu kwenye maisha ya watu, unakumbuka mara ya kwanza kwenu kumiliki friji ilikua mwaka Gani tuachie maoni yako ?