Freeman Mbowe, kwanini una mlaghai Lowassa?

Freeman Mbowe, kwanini una mlaghai Lowassa?

Matusi hayawezi kuwa ni dawa ya nguvu ya hoja.

Hakuna duka wala chuo cha matusi hapa duniani!

Waache watukane.

Mkuu nilipoanza kusoma post yako hii niliyokopi, nilidhani unamkanya huyo anayeita wasiokubaliana naye 'nyumbu'. Kama unashindwa kuona mtukanaji aliye 'usoni' pako huku ukitamba kwa 'watukanaji' wanaotegemewa kuja kwenye mada hii huoni tatizo mkuu?!
Halafu mkuu, nikuulize kitu.... Hivi mtu akiimarisha ulinzi kwenye nyumba/mali yake kwa kuweka walinzi, fence, alarm, nk halafu wezi nao wakaweza kukiuka huo ulinzi wakaiba na wakajulikana walioiba, tunamsakama aliyejitahidi kuweka ulinzi au wezi ambao wamejulikana? Kama taifa turidhike na hali hii ya wizi wa kura ktk kila chaguzi? Hivi ile tabia ya polisi wetu kuwa mtu anadhulumiwa lkn ananyanyaswa yeye iko hata kwa jamii nzima wala siyo kwenye vituo vya polisi tu??
 
Uchaguzi ulishaisha kitambo ww bado unabwela na Ukawa
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni Mbowe is still my Hero.
 
Msemaji Ukweli acha uchonganishi wako. Mheshimiwa Mbowe kamwe hamlaghai Mheshimiwa Lowassa. Hebu tueleze ni kwa nini jeshi la polisi lilikwenda kuwakamata vijana waliokuwa wakijumuisha idadi ya kura wale wa chadema na wale wa LHRC lakini ikawaacha wale wa CCM wakiendelea na majumuisho. Sio siri kwamba kura halali walizopata chadema na ukawa ni nyingi lakini kwa kuwa tu hatuna tume huru ya uchaguzi yaliyofanyika yamefanyika na hakuna pahala pa kupinga. kama mnayo dhamira ya dhati ya kuimarisha demokrasia basi tuirejee katiba tuirekebishe ili tume iwe huru.

Uchaguzi umekwisha, Rais na makamu wake wameapishwa. Rais ameanza kazi kutekeleza ahadi zake ni pamoja na kumteua Mwanasheria mkuu, kutoa maagizo kwa watendaji wakuu wa serikali, nk.

Hayo unayotaka yafanyike ni sehemu tu yatakayoshughulikiwa, na isiwe agenda tena kana kwamba tuko bado kwenye kampeni.

1) Tuache kulalamika bali kuchapa kazi.
2) Tufanye mabadiliko ya kifikra kila mmoja wetu
3) Tuwajibike ipasavyo mahala pa kazi.
4) Tushirikiane katika kujenga Tanzania mpya.
5) Tuwafichue wanaohujumu juhudi za kujenga nchi hii kiuchmi kufikia uchumi wa kati.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
 
Mmejitekenyaaaaa mkachekaaaaa.. Lakini nitaendelea kumtambua shujaa Mbowe katika siasa za nchi hii. Huu ulikuwa mwaka mbaya sana kwa ccm, Siasa za Mbowe zimekausha hazina ya CCM, mmekopa Billions of money kutoka kwa wafanyabiashara. Mmekopa kutoka CWT billion 50, ili kupambana na Ukawa na Mbowe. Viva Mbowe my hero.
Kumtambua Mbowe kama shujaa wako hakuwezi kuondoa ukweli wa hoja zangu.

Mbowe ana mlaghai Lowassa.
 
Kama wewe umekosa mtu wa kumdanganya,basi mdanganye nawewe mkeo na wanao.
 
kitu ambacho watu hawajajua ni kuwa chaguzi za nyuma fisiem walikuwa na watu maalum wa kutoroka na kubadilisha mabox ya kura.
wakati mwingine walikuwa wanawajeruhi hata wasimamizi ili kukimbia na box na kuweka mengine.
mwaka huu wameiba electronically ndio maana hamuelewi nini kimeendelea
Kwa hiyo uchaguzi ni batili?
 
Binafsi nimesoma Lakini ni pumba tupu.....no substance...
Uliposoma na kugundua ni pumba, nadhani kwa akili ndogo ungefahamu ni upumbavu kuanza kutoa comment kwenye andiko ambalo ni pumba.

Mtu mwenye fikra pana angesoma halafu akaachana na andiko bila kutoa comment.
 
Mwanzoni mwa mwaka huu tulishuhudia Mwenyekiti wa CHADEMA-Taifa, Freeman Mbowe akizunguka sehemu mbali mbali nchini kuzindua vikosi vya vijana wanaoitwa Red Brigade kwa ajili ya kuwaandaa kukilinda chama na kuzuia wizi wa kura kwenye Uchaguzi Mkuu.

Mbowe alienda mbali zaidi na kudai CHADEMA imejipanga katika Uchaguzi Mkuu na hakutakuwa na wizi wa kura hata moja.

Kwa sasa Mbowe anamwaminisha Lowassa kwa kumwambia ameibiwa kura wakati anafahamu hakuna kura iliyoibiwa kwa sababu vijana wake wa Red Brigade aliowapa mafunzo ya ulinzi walizilinda kwa umakini kura za CHADEMA/UKAWA.

Mbowe anatakiwa amweleze ukweli Lowassa hasa ikichukuliwa Lowassa alikuwa hafahamu mikakati ya CHADEMA katika kuzilinda kura ambazo pia zimemwezesha Mbowe kurudi tena bungeni.

Kama anachokisema Mbowe siyo ulaghai kwa Lowassa, basi inabidi awaambie pia wabunge wote wa CHADEMA/UKAWA wayakatae matokeo yote ya uchaguzi, hii ni pamoja na matokeo ya udiwani na ubunge. Wasiingie bungeni tena ili wawaache wabunge wa CCM waisimamie serikali yao ya Rais Magufuli iliyopatikana kwa wizi wa kura za Lowassa!

Kuingia bungeni na kuanza kuisimamia serikali ya Rais ambaye amepatikana kwa wizi wa kura ni kumlaghai na kumuhujumu Lowassa.

Gazeti la Nipashe la 10th February 2015 lilimnukuu Mbowe akisema,

Hizi ni baadhi ya thread nyingi zilitueleza mikakati ya Mbowe na CHADEMA katika kuzilinda kura za Uchaguzi Mkuu,

Ni walioko wodi za pale mlimani kupita jengo la shule ya hazina dodoma ndiyo pekee wanaoweza kumwamini Mbowe (yaani wagonjwa wa akili waliolazwa milembe ndiyo wenye sifa za kumwamini Mbowe kama hutoki humo unatakiwa kukaa mbali na discodancer huyo)
 
Mkuu nilipoanza kusoma post yako hii niliyokopi, nilidhani unamkanya huyo anayeita wasiokubaliana naye 'nyumbu'. Kama unashindwa kuona mtukanaji aliye 'usoni' pako huku ukitamba kwa 'watukanaji' wanaotegemewa kuja kwenye mada hii huoni tatizo mkuu?!
Halafu mkuu, nikuulize kitu.... Hivi mtu akiimarisha ulinzi kwenye nyumba/mali yake kwa kuweka walinzi, fence, alarm, nk halafu wezi nao wakaweza kukiuka huo ulinzi wakaiba na wakajulikana walioiba, tunamsakama aliyejitahidi kuweka ulinzi au wezi ambao wamejulikana? Kama taifa turidhike na hali hii ya wizi wa kura ktk kila chaguzi? Hivi ile tabia ya polisi wetu kuwa mtu anadhulumiwa lkn ananyanyaswa yeye iko hata kwa jamii nzima wala siyo kwenye vituo vya polisi tu??
Mtu aliyekuambia usiwe na wasiwasi atahakikisha hakuna mwizi anaingia na kuiba ndani ya nyumba yako. Na wewe ukamwamini na kumwachia nyumba yako ili alinde. Kama wizi ukitokea, mtu wa kwanza kuwajibika nadhani ni yule aliyekuwa analinda nyumba. Mbowe lazima awajibike kwa yale yametokea kwa sababu alisema amejipanga na hakuna hata kura moja itaibiwa.

Tukikubaliana kuwa zoezi la uchaguzi lilikuwa ni batili, basi hata wabunge wote wamepatikana kwenye zoezi batili. Kuna umuhimu wa wabunge wa CHADEMA/UKAWA kuyakataa matokeo yote ya uchaguzi.

Wabunge wa CHADEMA/UKAWA hawawezi kwenda bungeni kufanya kazi ya kuisimamia serikali ya Rais Magufuli ambaye amepatikana kupitia zoezi batili. Wabunge wa tiketi ya CHADEMA/UKAWA kuanza kuisimamia serikali ya Rais Magufuli ni kumuhujumu Lowassa!
 
Mmejitekenyaaaaa mkachekaaaaa.. Lakini nitaendelea kumtambua shujaa Mbowe katika siasa za nchi hii. Huu ulikuwa mwaka mbaya sana kwa ccm, Siasa za Mbowe zimekausha hazina ya CCM, mmekopa Billions of money kutoka kwa wafanyabiashara. Mmekopa kutoka CWT billion 50, ili kupambana na Ukawa na Mbowe. Viva Mbowe my hero.

mbowe no shujssa
 
Msemaji Ukweli acha uchonganishi wako. Mheshimiwa Mbowe kamwe hamlaghai Mheshimiwa Lowassa. Hebu tueleze ni kwa nini jeshi la polisi lilikwenda kuwakamata vijana waliokuwa wakijumuisha idadi ya kura wale wa chadema na wale wa LHRC lakini ikawaacha wale wa CCM wakiendelea na majumuisho. Sio siri kwamba kura halali walizopata chadema na ukawa ni nyingi lakini kwa kuwa tu hatuna tume huru ya uchaguzi yaliyofanyika yamefanyika na hakuna pahala pa kupinga. kama mnayo dhamira ya dhati ya kuimarisha demokrasia basi tuirejee katiba tuirekebishe ili tume iwe huru.

Sasa zile kura milioni 10 alizosema lowasa kapata alipata wapi majumuisho yake?
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni Mbowe is still my Hero.
Mbowe kuwa your hero haina maana kama anachokifanya ni halali.

Kuna watu wengine watakuambia jambazi fulani kwake ni hero. Hii haina maana anachokifanya jambazi ni halali katika jamii.

Kwa nini Mbowe ana mlaghai Lowassa kwa kumwambia kura zake zimeibiwa wakati vijana wa Red Brigade walizilinda kura za CHADEMA/UKAWA.
 
Ni ccm tu anaweAza kumpinga a Mbowe maana anahatarisha hatima yao,,,,,,,,
Hoja siyo Mbowe kuhatarisha hatima ya CCM.

Hoja ni Mbowe kuendelea kumlaghai Lowassa akimwambia ameibiwa kura na ayakatae matokeo ya uchaguzi wakati yeye yuko mbioni kuelekea bungeni kuisimamia serikali ya Rais Magufuli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom