Freeman Mbowe aombwe msamaha

Freeman Mbowe aombwe msamaha

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,768
Reaction score
49,934
Siku zote msamaha anaombwa aliyekosewa.

Kwa kila mwenye akili, mkweli wa nafsi, anayemtumikia Mungu wa kweli, na mwenye Roho wa Mungu, hawezi kusita wala kuwa na kigugumizi kutamka kuwa Mh. Mbowe amekosewa mara nyingi, si mara moja wala mara mbili.

Kama itakuja kutokea siku moja Taifa letu likabahatika kupata uongozi wenye hekima, uongozi unaojua maana ya umoja, upendo, utu, haki, na unaojua umuhimu wa tunu hizi katika kuleta maendeleo ya kweli, Mh. Mbowe ni mtu ambaye atatakiwa kuwa wa kwanza kuombwa msamaha kuliko mtu yeyote, kwa uovu mwingi aliotendewa wakati mbalimbali:

1. Mbowe, mashamba yake yaliwahi kuteketezwa kwa uonevu.

2. Mbowe, club yake ya Bilcanas iliwahi kunyang'anywa kwa uonevu.

3. Mbowe amewahi kuwekwa mahabusu mara nyingi kwa uonevu.

4. Mbowe amewahi kuhukumiwa kulipa mamilioni ya pesa kwa uonevu.

5. Mbowe amewahi kubambikiziwa kesi zisizo na vichwa mala miguu kwa nia tu ya kumkomoa.

6. Mbowe akaunti zake za benki ziliwahi kufungiwa kwa uonevu.

7. Mbowe, hoteli yake ya familia imewahi kubambikiziwa kodi zinazozidi mapato maradufu.

Mbowe, mpaka leo bado anaonewa, na yumkini ataendelea kuonewa, lakini bado kitambo kidogo, ushindi wa haki utapatikana. Siyo ushindi wa Mbowe, bali ni ushindi wa haki dhidi ya uovu.

Makaburu kule Afrika Kusini waliowaonea sana wapigania haki wazalendo, wakiongozwa na kiongozi shupavu, mzalendo wa kweli wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela. Utawala wa makaburu, chini ya Fredrick De Clerk, ulipoijiwa na hekima, ulitaka maridhiano na Waafrika weusi waliokuwa wakibaguliwa. Jambo la kwanza, walimwachia Nelson Mandela na wapigania haki wote. Ukafanyika uchaguzi huru, huru hasa siyo kama hivi viinimacho vyetu vya Tanzania.

Mandela aliposhinda kwenye uchaguzi huru, alitaka Afrika Kusini yenye umoja na upendo, naye akanena, 'kama ubaguzi wa mzungu dhidi ya mtu mweusi haukuwa mzuri, basi vivyo hivyo, ubaguzi wa mtu mweusi dhidi ya mzungu, hautakuwa mzuri. Mandela hakutaka roho ya kisasi miongoni mwa wananchi wa Afrika Kusini. Aliamua kuunda tume ya maridhiano. Kisha wahalifu na waliofanyiwa uhalifu walitakiwa kwenda mbele ya Tume. Walikutanishwa. Wahalifu walieleza uovu wao wote, kisha waliofanyiwa uhalifu waliombwa msamaha, nao baada ya kutoa msamaha, wahalifu walikabidhiwa vyeti vya kusamehewa ambapo walihakikishiwa kuwa kamwe wasingeshtakiwa kwa makosa waliyoyatenda ambayo wameyakiri mbele ya Tume. Kama umeficha uhalifu, na baadaye ukapatikana ushahidi wa uhalifu wako, ujue utashitakiwa na kuhukumiwa.

Rais Samia anasema tusahau yaliyopita, tuanze upya. Je, anafahamu kanuni za maridhiano? Unaweza ukafanya maridhiano na mtoto, huku baba yake au kaka yake, umemfunga pingu kwa kumwonea?
 
Kweli kabisa pamoja familia yake, CDM na Watanzania kwa ujumla. Ili kauli ya Mama iwe na mashiko " Tusahau yaliyopita tuanze ukurasa mpya..."
 
Nadhani tatizo ni mila zetu, mkubwa akimkosea mdogo hukaa kimya, lakini huyu mkubwa wa sasa pamoja na kukosea namshangaa bado anapiga kelele.
 
Rugemalira pia usimsahau!
Rugemarila, angalao ni mara moja. Wapo na wengine pia. Lakini Mbowe na mara nyingi zaidi. Niliyoandika ni machache tuliyopata kuyafahamu.
 
Nadhani tatizo ni mila zetu, mkubwa akimkosea mdogo hukaa kimya, lakini huyu mkubwa wa sasa pamoja na kukosea namshangaa bado anapiga kelele.
Ni kweli ni mila zetu lakini hizi ni mila potofu, zinazotakiwa kufutwa, sawa na zile za matapeli wa kupiga ramli.
 
..polisi wanadai wakina Adamoo walikiri makosa ya njama za ugaidi mwezi August 2020.

..Mbowe ambaye anatuhumiwa kuwa recruiter, financier, na mastermind, wa ugaidi huo alikamatwa mwezi July 2021.

..kipindi chote hicho Mbowe alikuwa akitembelea maeneo mbalimbali hapa nchini, na hata kusafiri nje ya nchi na kurudi.

..kwa kweli "gap" ya ukamataji wa watuhumiwa wa kesi hii imeniacha na maswali mengi kuliko majibu, na zaidi imenifanya nitilie mashaka ukweli wa tuhuma dhidi ya washtakiwa.
 
..polisi wanadai wakina Adamoo walikiri makosa ya njama za ugaidi mwezi August 2020.

..Mbowe ambaye anatuhumiwa kuwa recruiter, financier, na mastermind, wa ugaidi huo alikamatwa mwezi July 2021.

..kipindi chote hicho Mbowe alikuwa akitembelea maeneo mbalimbali hapa nchini, na hata kusafiri nje ya nchi na kurudi.

..kwa kweli "gap" ya ukamataji wa watuhumiwa wa kesi hii imeniacha na maswali mengi kuliko majibu, na zaidi imenifanya nitilie mashaka ukweli wa tuhuma dhidi ya washtakiwa.
Kelele za Katiba Mpya ndio zinazomuumiza Mbowe.
 
Mama aliona bila kudhibiti jamaa alikuwa anaobgeza pressure ya ajabu kwenye suala la kudai katiba mpya.

Sasa Mama analala usingizi.
 
..polisi wanadai wakina Adamoo walikiri makosa ya njama za ugaidi mwezi August 2020.

..Mbowe ambaye anatuhumiwa kuwa recruiter, financier, na mastermind, wa ugaidi huo alikamatwa mwezi July 2021.

..kipindi chote hicho Mbowe alikuwa akitembelea maeneo mbalimbali hapa nchini, na hata kusafiri nje ya nchi na kurudi.

..kwa kweli "gap" ya ukamataji wa watuhumiwa wa kesi hii imeniacha na maswali mengi kuliko majibu, na zaidi imenifanya nitilie mashaka ukweli wa tuhuma dhidi ya washtakiwa.
Hii kesi, hata asiye na ABC ya sheria, hata ambaye hajawahi kugusa chuo kikuu, alimradi ana akili ya kawaida, anajua kabisa, ni kesi ya uwongo, ni kesi ya kumbambikizia Mbowe. Hii kesi ukifuatilia kila kitu, utaishia kwenye possibilities 2 kubwa:

1) Rais ana akili ndogo sana, alidanganywa na Siro, na kwa sababu ana akili chini ya kiwango cha kawaida, aliamini kila alichoambiwa. Hii ni sawa Rais aambiwe kwamba kuna mtu anasafirisha silaha nzito kutoka Dar kwenda Mwanza. Kila siku anabeba vifaru 5 kwenye pickup yake ya Toyota Hilux. Halafu na Rais akatika kuutangazia umm. Hivi ikitokea hivyo, mtasema kiongozi alidanganywa au mtasema tuna kiongoz8 asiye na akili?

2) Rais ni mwenye akili timamu, na ni yeye mwenyewe ndiye aliamuru Mbowe akamatwe, na akawapa maagizo akina Siro wahakikishe anawekwa ndani. Akina Siro wakaona wambambikizie kesi ya ugaidi. Labda Samia alidhani watatumia akili kumbambikizia Mbowe kesi itakayoelekeana na ukweli, lakini kwa bahati mbaya kwenye kundi la akina Kingai, hakukuwa na hata mmoja mwenye akili ya kiwango cha kawaida, wakaamua kuamka na shtaka la ugaidi.

Kama ulivyosema, yaani umesikia kuna gaidi, halafu ukae mwaka mzima bila kumkamata! Basi tuna jeshi la polisi na serikali inayoendeshwa na wendawazimu. Huyo gaidi, kwa mwaka mzima si angeweza kuwa ameunda kundi jingine na kuelra maafa makubwa?
 
Mama aliona bila kudhibiti jamaa alikuwa anaobgeza pressure ya ajabu kwenye suala la kudai katiba mpya.

Sasa Mama analala usingizi.
Usingizi wa muda mfupi, Aman ya moyo hana
 
Hii kesi, hata asiye na ABC ya sheria, hata ambaye hajawahi kugusa chuo kikuu, alimradi ana akili ya kawaida, anajua kabisa, ni kesi ya uwongo, ni kesi ya kumbambikizia Mbowe. Hii kesi ukifuatilia kila kitu, utaishia kwenye possibilities 2 kubwa:

1) Rais ana akili ndogo sana, alidanganywa na Siro, na kwa sababu ana akili chini ya kiwango cha kawaida, aliamini kila alichoambiwa. Hii ni sawa Rais aambiwe kwamba kuna mtu anasafirisha silaha nzito kutoka Dar kwenda Mwanza. Kila siku anabeba vifaru 5 kwenye pickup yake ya Toyota Hilux. Halafu na Rais akatika kuutangazia umm. Hivi ikitokea hivyo, mtasema kiongozi alidanganywa au mtasema tuna kiongoz8 asiye na akili?

2) Rais ni mwenye akili timamu, na ni yeye mwenyewe ndiye aliamuru Mbowe akamatwe, na akawapa maagizo akina Siro wahakikishe anawekwa ndani. Akina Siro wakaona wambambikizie kesi ya ugaidi. Labda Samia alidhani watatumia akili kumbambikizia Mbowe kesi itakayoelekeana na ukweli, lakini kwa bahati mbaya kwenye kundi la akina Kingai, hakukuwa na hata mmoja mwenye akili ya kiwango cha kawaida, wakaamua kuamka na shtaka la ugaidi.

Kama ulivyosema, yaani umesikia kuna gaidi, halafu ukae mwaka mzima bila kumkamata! Basi tuna jeshi la polisi na serikali inayoendeshwa na wendawazimu. Huyo gaidi, kwa mwaka mzima si angeweza kuwa ameunda kundi jingine na kuelra maafa makubwa?
Chanzo halisi cha hii kesi ni "no brainer", so no use wasting your time putting up elaborate scenarios of what might be the reason behind. Acha hii kesi iendelee, if only for the simple fact kwamba tunajifunaza mengi juu ya the evil, unjust and totally corrupt collusion/conspiracy kati ya CCM, Serikali, Polisi na Mahakama.
 
Siku zote msamaha anaombwa aliyekosewa.

Kwa kila mwenye akili, mkweli wa nafsi, anayemtumikia Mungu wa kweli, na mwenye Roho wa Mungu, hawezi kusita wala kuwa na kigugumizi kutamka kuwa Mh. Mbowe amekosewa mara nyingi, si mara moja wala mara mbili.

Kama itakuja kutokea siku moja Taifa letu likabahatika kupata uongozi wenye hekima, uongozi unaojua maana ya umoja, upendo, utu, haki, na unaojua umuhimu wa tunu hizi katika kuleta maendeleo ya kweli, Mh. Mbowe ni mtu ambaye atatakiwa kuwa wa kwanza kuombwa msamaha kuliko mtu yeyote, kwa uovu mwingi aliotendewa wakati mbalimbali:

1. Mbowe, mashamba yake yaliwahi kuteketezwa kwa uonevu.

2. Mbowe, club yake ya Bilcanas iliwahi kunyang'anywa kwa uonevu.

3. Mbowe amewahi kuwekwa mahabusu mara nyingi kwa uonevu.

4. Mbowe amewahi kuhukumiwa kulipa mamilioni ya pesa kwa uonevu.

5. Mbowe amewahi kubambikiziwa kesi zisizo na vichwa mala miguu kwa nia tu ya kumkomoa.

6. Mbowe akaunti zake za benki ziliwahi kufungiwa kwa uonevu.

7. Mbowe, hoteli yake ya familia imewahi kubambikiziwa kodi zinazozidi mapato maradufu.

Mbowe, mpaka leo bado anaonewa, na yumkini ataendelea kuonewa, lakini bado kitambo kidogo, ushindi wa haki utapatikana. Siyo ushindi wa Mbowe, bali ni ushindi wa haki dhidi ya uovu.

Makaburu kule Afrika Kusini waliowaonea sana wapigania haki wazalendo, wakiongozwa na kiongozi shupavu, mzalendo wa kweli wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela. Utawala wa makaburu, chini ya Fredrick De Clerk, ulipoijiwa na hekima, ulitaka maridhiano na Waafrika weusi waliokuwa wakibaguliwa. Jambo la kwanza, walimwachia Nelson Mandela na wapigania haki wote. Ukafanyika uchaguzi huru, huru hasa siyo kama hivi viinimacho vyetu vya Tanzania.

Mandela aliposhinda kwenye uchaguzi huru, alitaka Afrika Kusini yenye umoja na upendo, naye akanena, 'kama ubaguzi wa mzungu dhidi ya mtu mweusi haukuwa mzuri, basi vivyo hivyo, ubaguzi wa mtu mweusi dhidi ya mzungu, hautakuwa mzuri. Mandela hakutaka roho ya kisasi miongoni mwa wananchi wa Afrika Kusini. Aliamua kuunda tume ya maridhiano. Kisha wahalifu na waliofanyiwa uhalifu walitakiwa kwenda mbele ya Tume. Walikutanishwa. Wahalifu walieleza uovu wao wote, kisha waliofanyiwa uhalifu waliombwa msamaha, nao baada ya kutoa msamaha, wahalifu walikabidhiwa vyeti vya kusamehewa ambapo walihakikishiwa kuwa kamwe wasingeshtakiwa kwa makosa waliyoyatenda ambayo wameyakiri mbele ya Tume. Kama umeficha uhalifu, na baadaye ukapatikana ushahidi wa uhalifu wako, ujue utashitakiwa na kuhukumiwa.

Rais Samia anasema tusahau yaliyopita, tuanze upya. Je, anafahamu kanuni za maridhiano? Unaweza ukafanya maridhiano na mtoto, huku baba yake au kaka yake, umemfunga pingu kwa kumwonea?
Yaani tuwasamehe kina Kingai,Mahita na Jumanne
 
Back
Top Bottom