Form five selection

Zee Real

Member
Joined
May 2, 2021
Posts
57
Reaction score
66
Habari za wakati huu vijana wenzangu, wakubwa zangu shikamoo.

Naomba kujuzwa kama selection za
kujiunga kidato cha tano kwa mwaka 2022/2023, zimeshatoka?

Kwa yeyote mwenye taarifa naomba anijuze tafadhali.

Natanguliza shukrani.
 
Habari za wakati huu vijana wenzangu,wakubwa zangu shikamoo.

Naomba kujuzwa kama selection za
kujiunga kidato cha tano kwa mwaka 2022/2023, zimeshatoka??.

Kwa yeyote mwenye taarifa naomba anijuze tafadhali.

Natanguliza shukrani.
bado, hii ni very big event, zikitoka tu utajua. TULIA kama Ackson!
 
Kwani form five huwa zinaanza lini rasmi?

Je Kwanini wasitoe mwenzi mmoja kabla au hata miezi 2 ili yafanyike maandalizi?
Mwezi wa saba ndio huwa wanaripoti shuleni.Labda kwa sababu kwa sasa elimu ni bure wanadhani maandalizi sio mengi kama huko nyuma.
 
Hadi Sasa hakuna Taarifa yeyote kuhusu siki ambayo Form Five Selection zitatoka ila mategemeo ni mwisho wa mwezi huu. As long as unaufaulu mzuri kidato cha nne, hauna haja ya kupata mtetemo utapangwa kwenye shule nzuri tuu. Kama huna uhakika na ufaulu wako soma >>TAMISEMI Form Five Selection 2023/2024 - Jinsi Ya Online wameelezea vizuri namna ya izi selection zinavyo fanyika.
 
MCHANGANUO WA SELECTION FORM FIVE AND COLLEGE'S MWAKA 2023


Kutokana na ufaulu wa wanafunzi waliomaliza kidato cha nne mwaka 2022 kuongezeka kwa 2.9% zaidi ya ufaulu wa mwaka 2021 kumeifanya selikari kuja na mikakati madhubuti ya kuhakikisha kila mwanafunzi wa ufaulu wa juu anapewa kipaumbele




TAMISEMI imeweza kupanga selection hizo kwa makundi tofautitofauti




UFUATAO NI MCHANGANUO WA JINSI TAMISEMI ILIVOPANGA SELECTIONI HIZO


Tukianza na

1. Masomo ya Sayansi
PCB, na PCM
wakiume tutachukua kuazia daraja la I point ya 7 -15
wakike daraja la I point ya 7-17
CBG na PGM
Wakiume tutachukua mpaka daraja la II point ya 21
Wakike mpaka daraja III ya 22

2. Masomo ya Biashara

EGM na EC
Wakiume mpaka daraja II ya 21
Wakike mpaka daraja III ya 22

HGE na CBA
wakiume mpaka daraja II ya 21
wakike mpaka daraja III ya 22

3. Masomo ya sanaa

HGL,HGK, na HKL
wakiume mpaka daraja II ya 21
Wakike mpaka daraja III ya 23

4. Masomo ya Lugha

KLF
wakiume mpaka daraja II ya 21
wakike mpaka daraja III ya 23


VYUO /COLLEGE'S

1. Vyuo vya sayansi (Afya na Ufundi)
Wakiume mpaka daraja la III point ya 23
Wakike mpaka daraja IIIya 25
NB: Mwanafunzi wa sayansi watachukuliwa endapo wana D nne za masomo ya sayansi ikiwemo na Hesabu

2. Vyuo vya kati na biashara
Wakiume daraja la III point ya 25
Wakike mpaka daraja la IV point ya 26.




NB:
1. Hatutachukua
wakiume yeyote mwenye daraja la III kujinga na kidato cha tano
Wakike yeyote mwenye daraja la III point ya 24-- kujiunga na kidati cha tano

2. Hatutachukua
wakiume yeyote mwenye daraja la IV kujiunga na vyuo vyovyote vya selikari





NB: Mchakato wa kutoa selection post bado upo mbioni mtaarifiwa pindi post zitakapotoka




Imetolewa na katibu mkuu wa TAMISEMI
Dodoma
S.L.P , 11524 DAR ES SALAAM
 
Serikali Kwa hili imefanya upuuzi, haiwezekani matokeo yalitolewa January, selection wanataka wazitoe mwezi mmoja kabla ya shule kufunguliwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…