OllaChuga Oc
JF-Expert Member
- Jul 4, 2016
- 21,933
- 25,245
Mkuu huo uzi wa Bavaria naomba kuuona. Sijawahi uona..Mkuu hujakosea maana hata kabla ya Ontario
Bavaria alileta Uzi Wa forex hapa jf Na watu walichangia sana
Alipokuja Ontario alichofanya ni kumpa credits Bavaria ila hakuunga Uzi wake wala kuendeleza pale kwa Bavaria!
Jamaa kafanya vyema Ku share alichokipata wewe ukija mkuku kukosoa tunakushangaa kabisa maana yamkini wewe hujawahi kushare chochote!
Halikadharika Ontario hajasema kuwa ana hatimiliki za Uzi Wa forex jf!
Sisi sote ni binadamu ina maana kwa mfano Ontario akiondoka basi forex trade humu zinakoma!
Big up mleta uzi
DJ sepetu
Ukitafuta avatar ya Bavaria bofya avatar yake kisha bofya post utauona
Aina kwere mbabaa. .Ukitafuta avatar ya Bavaria bofya avatar yake kisha bofya post utauona
Au kwenye Uzi Wa Ontario Wa forex ameweka link ya huo uzi
DJ sepetu
Poa
Habari za muda ndugu zangu wana JF, natumai mu wazima wa afya.
Awali ya yote ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa mkuu ONTARIO na wachangiaji wengine wengi kama mashujaa wetu katika suala zima la kufamishana na kuelimishana kuhusu biashara hii ya Forex.
Katika pita pita na harakati zangu za kuhakikisha tonge linaenda kinywani ndipo nikabahatika kukutana na mnaijeria mmoja ndani ya bus la kuelekea mjini Mbabane nchini Swaziland kutokea Maputo nchini Msumbiji akiwa ameshika simu yake busy huku akifurahi mwenyewe na kucheka.
Ghafla uvumilivu ulinishinda na kutaka kufahamu ni nini haswa jamaa yule alikuwa akifanya maana alipatwa na furaha isiyo na kifani.
Baada ya kutupia jicho ndipo nikaona namba za bluu na nyekundu zikisoma kwenye kioo cha simu yake, kutazama kwa umakini ndipo nilipogundua kuwa alikuwa anatrade forex na kwa kuwa nilikuwa nimeshapata mwangaza wa taarifa kadhaa kutoka kwa boss ONTARIO miezi kadhaa iliyopita humu JF ikanibidi nimsalimie bwana yule na kumuuliza ni nini haswa kiini cha furaha yake.
Katika maongezi ikabidi nimueleze ukweli kuwa mimi ni 'mweupe' kabisa yaani sifahamu ni jinsi gani ya kutrade forex ingawa nilikuwa nimeshapata kusikia kidogo ni nini forex.
Ndipo hapo aliponiambia kuwa laiti kama ungalijua utamu wa kitu hii wala usinge poteza muda wako kufanya mambo mengine. Baada ya kufika Mbabane akanipatia namba yake pamoja na FOREX pdf file ambayo nitaiattach hapa kwa ajili ya kujifunza na akaniomba nisisome kwa pupa wala haraka na pindi nitakapo maliza nisisite kumtafuta kwa msaada wowote ule.
Nimejaribu kuanzia mbali kidogo ili nanyi ndugu zangu muweze kupata picha halisi how really this Forex thing is, katika kipindi hiki ambapo tunasubiri Mafunzo zaidi kutoka kwa mkuu ONTARIO .
This PDF file is very informative kwa beginners wote ambao wana nia ya kufahamu na kufanya FOREX TRADING.
Na pia si vibaya kuongezea hapa resources zozote ambazo zitasaidia kujinoa kuhusiana na forex trading maana walio wengi bado hawajapata mwangaza katika forex trading, maana haitakuwa vizuri kuingia darasani tukiwa vichwa vitupu.
Napenda kuwasilisha. Ahsanteni.
==========================
An introduction to the Basics of Forex Trading
How to manage a Forex Account
=========• UPDATE •==========
Nimebahatika kupata hii link ya group Maarufu kwaajili ya materials na Books kuhusu Forex Trading so nikaona si mbaya kushare nanyi tena ingawa hapo awali kuna baadhi ya wachangiaji walijitokeza kunishambulia kwa maneno makali wakidhani kwamba kila mtu anaeleta uzi au mada yoyote humu JF kuhusu Forex trading basi anamuonea wivu au Kumpinga ndugu Ontario wakati kiukweli si hivyo bali tunajaribu kusaidiana ili kuhakikisha sisi sote tunasonga mbele.
Hili ni group la TELEGRAM so ili kujiunga inabidi kwanza upakue App ya telegram kwa wale ambao watakuwa hawana.
FOREX LIBRARY
Traders Library
Habari za muda ndugu zangu wana JF, natumai mu wazima wa afya.
Awali ya yote ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa mkuu ONTARIO na wachangiaji wengine wengi kama mashujaa wetu katika suala zima la kufamishana na kuelimishana kuhusu biashara hii ya Forex.
Katika pita pita na harakati zangu za kuhakikisha tonge linaenda kinywani ndipo nikabahatika kukutana na mnaijeria mmoja ndani ya bus la kuelekea mjini Mbabane nchini Swaziland kutokea Maputo nchini Msumbiji akiwa ameshika simu yake busy huku akifurahi mwenyewe na kucheka.
Ghafla uvumilivu ulinishinda na kutaka kufahamu ni nini haswa jamaa yule alikuwa akifanya maana alipatwa na furaha isiyo na kifani.
Baada ya kutupia jicho ndipo nikaona namba za bluu na nyekundu zikisoma kwenye kioo cha simu yake, kutazama kwa umakini ndipo nilipogundua kuwa alikuwa anatrade forex na kwa kuwa nilikuwa nimeshapata mwangaza wa taarifa kadhaa kutoka kwa boss ONTARIO miezi kadhaa iliyopita humu JF ikanibidi nimsalimie bwana yule na kumuuliza ni nini haswa kiini cha furaha yake.
Katika maongezi ikabidi nimueleze ukweli kuwa mimi ni 'mweupe' kabisa yaani sifahamu ni jinsi gani ya kutrade forex ingawa nilikuwa nimeshapata kusikia kidogo ni nini forex.
Ndipo hapo aliponiambia kuwa laiti kama ungalijua utamu wa kitu hii wala usinge poteza muda wako kufanya mambo mengine. Baada ya kufika Mbabane akanipatia namba yake pamoja na FOREX pdf file ambayo nitaiattach hapa kwa ajili ya kujifunza na akaniomba nisisome kwa pupa wala haraka na pindi nitakapo maliza nisisite kumtafuta kwa msaada wowote ule.
Nimejaribu kuanzia mbali kidogo ili nanyi ndugu zangu muweze kupata picha halisi how really this Forex thing is, katika kipindi hiki ambapo tunasubiri Mafunzo zaidi kutoka kwa mkuu ONTARIO .
This PDF file is very informative kwa beginners wote ambao wana nia ya kufahamu na kufanya FOREX TRADING.
Na pia si vibaya kuongezea hapa resources zozote ambazo zitasaidia kujinoa kuhusiana na forex trading maana walio wengi bado hawajapata mwangaza katika forex trading, maana haitakuwa vizuri kuingia darasani tukiwa vichwa vitupu.
Napenda kuwasilisha. Ahsanteni.
==========================
An introduction to the Basics of Forex Trading
How to manage a Forex Account
=========• UPDATE •==========
Nimebahatika kupata hii link ya group Maarufu kwaajili ya materials na Books kuhusu Forex Trading so nikaona si mbaya kushare nanyi tena ingawa hapo awali kuna baadhi ya wachangiaji walijitokeza kunishambulia kwa maneno makali wakidhani kwamba kila mtu anaeleta uzi au mada yoyote humu JF kuhusu Forex trading basi anamuonea wivu au Kumpinga ndugu Ontario wakati kiukweli si hivyo bali tunajaribu kusaidiana ili kuhakikisha sisi sote tunasonga mbele.
Hili ni group la TELEGRAM so ili kujiunga inabidi kwanza upakue App ya telegram kwa wale ambao watakuwa hawana.
FOREX LIBRARY
Traders Library
kweli kabisaAwali nilikuwa na wazo la kuattach kule kwenye Main thread ya Forex ila nikaona italeta usumbufu kidogo na haitokuwa rahisi kwa wengi kuweza kuipata sababu ya comments kuwa nyingi.