Hapana Teacher,
Lazima uongee na watu kwa lugha watakayoielewa. Ndo maana enzi hizo kumtajia mtu jambo lolote linahusu uchawi ilikuwa inatosha kumjenga hofu. Hata akina Shekhe Yahaya wanatumia hiyo philosophy bila kujua kuwa mambo yamebadilika.
Katika maisha ya kawaida lazima itumike lugha inayoleta maana halisi (the language which makes senses). Kama ni viboko, vitisho etc.
mtu haruhusiwi kuomba chumvi jioni
my take:
ni aibu kwa mwanamke mpaka jioni chakula kinatakiwa hujamaliza kupika kwa kuwa huna chumvi. Kuficha aibu unamwambia jirani unaomba dawa!
Sio wewe tu! Hata mm.....sasa mpaka umpige mwanao na uume unatafuta nn? Hahahaa..bsh*t
athari yake ni kuwa watu wanafuta vitu kutokana na hofu......nidhamu ya woga. sio kwa kuelewa maana.
Nakubaliana na wewe DC lugha lazima iwe sambamba na maendeleo ya kijamii, lakini isiwafunge watu sana kwenye woga kiasi cha kuwa wakashindwa kujitambua au hata kushindwa kufanya jambo walilokatazwa pale inapolazimu.
na kumpaka mtoto wanja aidha kwenye nyusi nao kunazuia nini? waswahili twapenda sana!!
namaba nne ya kwanza kweli ni mambo impossible......sasa utakuwa watafuta nini duh!!! iamani zingine we acha tu!
it is pure BS!....huo wa kumpiga mwanao na ub** ni utaahira moja kwa moja.
Kufagia nyumba usiku nyumba zetu miaka ile zilikuwa zina sakafu ya udongo na madirisha nyingine zilikuwa hazina au ya ushahidi tu hivyo ni vumbi mtindo mmoja na mafua tele!
Kuna nyingine, ila nadhani ilikuwa ni utani zaidi.
Kwamba kama unaumwa macho, basi chukua kidole chako uingize kwenye nanihii ya ma wife wako utoe majimaji upake kwenye macho. Kwamba hiyo ni dawa ya macho.
Ngoja nisubiri wataalamu wanipe maoni kabla sijaiongeza.
hahah ppl u r sick! lol
mie najua nyengine it goes like this " yes yes yes, mzungu hali fenes, akila fenes huja*ba upes"
:A S 13:
Hivi mnaamini kwamba infanticidal behaviour ziko nyingi? Mfano mzuri ni kwa simba.
Hata hivyo, hii kitu watu wanaamini kuwa ilikuwa inatumika kuwamaliza watoto ambao mama zao wamekuja wanawanyonyesha ili wasichelewe kuzaa. It was against lactation amenorrhea (kwa wanawake ambao hawawezi kuona siku zao hadi waache kunyonyesa).
Huku kwa kawaida, yaani kutoa hewa au ni yale mambo ya Infii?
Kuna mambo mengi yanayoaminika sana katika jamii zetu na huwapa watu mashaka. Nimejaribu kuweka hii list. Naamini wengine wataongezea.
Kuhusu mambo ya uzazi:
1. Wazazi wakifanya tendo la ndoa mtoto anapata madhara (maziwa yanachacha)
2. Mapacha wakirukwa wanakufa (endapo mzazi mmoja atafanya ngono nje ya ndoa kabla au baada ya kuzaliwa)
3. Wazazi wakifanya ngono nje ya ndoa wanambemenda mtoto
4. Baba akimpiga mtoto kichwani na uume wake mtoto anakufa
5. Mama akimlaani mtoto wake kwa kumwonyesha sehemu nyeti anakuwa kichaa
6. Ukitembea na ndugu yako wa damu watoto wanaozaliwa wanakuwa mazezeta
7. Ukifanya tendo la ndoa na mama mja mzito (karibia na kujifungua) mtoto anazaliwa na uchafu kichwani.
8. Bundi akilia karibu na nyumba basi lazimi kuna mtu atakufa kwenye familia hiyo
9. Mwanamume akitembea na mtu na mwanaye anakuwa na uwezo wa ajabu. Mfano, akitemea mate siafu wanatawanyika na kupoteza dira
10. Ukipanda nevu ya mwanamke (kwa wale wenye ndevu) utafanikiwa kwenye biashara na kuwa tajiri mkubwa sana.
11. Kuna mbegu za mimea fulani na mkia wa ndege fulani ukigusisha kwenye mkojo wa mwanamke basi atakutafuta kwa udi na uvumba (ni dawa ya mapezi)
12. Ndoa, siku ya harusi lazima mwanamume ahakikishe anamkanyaga kidole cha mguu mwanamke, akimuacha mwanamke akamkanyaga yeye, mwanamke atamuendesha kwenye ndoa yao
13. marufuku kutwanga usiku kwa sababu wachawi watakuja na pia aliamini kwamba
14. mtu haruhusiwi kufagia usiku kwa kuwa ataita wachawi na haruhusiwi kununua au kuomba chumvi usiku. akihitaji aseme anaomba 'dawa
15. Ukimwimbia mtu chupi au nywele za sehemu za siri (kwa wanawake) basi unaweza kumfunga uzazi.
16. Ukinyoa nywele lazima uzizike ardhini vinegenvyo wachawi wakiziokota watakuua.
17. n.k.....
Kuhusu mambo ya watoto
1. Kuna baadhi ya watu hawatakiwi kumwona mtoto mchanga kabla ya kitovu kudondoka kwa hofu kuwa anaweza kufa au kudhurika. Kwa hiyo inabidi mtoto afichwe
2. Kitovu kikidondokea dudu ya mtoto (uume kwa mtoto wa kiume) anakuwa ******* (hawezi kuzaa)
3. Kitovu kikidondoka lazima kitunzwe vinginevyo mtoto anaweza kufanyiwa mambo ya uchawi endapo walozi watakiokota
4. Kitovu anafungwa mtoto kiunoni ili asipate mchango (basically ni utapiamlo)
5. Kuna dawa lazima mototo afungwe kiunonni au kwenye mkono ili asipate mchango.
6. Mtoto asipopelekwa kwa babu zake atakuwa anapata ndoto za ajabu na kustuka stuka usiku. Lazima wazee wamwone, wamwekee mikono na baadhi ya makabila wampatie na jina.
7. mtoto akizaliwa lakini akiwa analia sana labda nyumba haijamkaribisha........mzee wake apige hodi kila kona ya nyumba!
8. Mtoto lazima apewe jina la utoto (la ukoo) na la ukubwani (may be la dini)
9. N.K
Nitaendelea kuongeza na nyingine nikizikumbuka. Pia wengine wanaweza kuongezea kutoka kwenye makabila yao.
Kweli kuna umuhimu wa kuweka hivi vitu kwenye kumbukumbu. Vijana kama mdogo wangu Teamo watayahitaji haya mambo muda si mrefu.
duh mkuu we kiboko...umetoa wapi hizi....kuna ile nyingine inasema ukipiga mluzi usiku nyoka wanakuja...hii sijui ilikuwa ina maana gani
Halafu kuna hii nyingine (natanguliza samahani kwa wakereketwa wa mambo ya gender),
Kama unaenda safari, mtu wa kwanza kukutana naye akiwa mwanamke (na hasa hasa vile vibibi) bas safari yote imeinga mikosi.
Kwa wale wenye wake wengi, walikuwa na mmoja ambaye analeta bahati nzuri (hana mkosi. Kwa hiyo endapo mtu anasafiri au anaenda kuwinda, basi siku ya kuamkia safari lazima akalale na yule mke mwenye bahati ili mambo yaende mswano. Wakina Shekh Yahaya wanaendeleza haya mambo kupitia nyota. Kwamba kuna wanaume wanasafiria nyota za wapenzi au waume zao. n.k.....
hiyo mie naijua ....
ukiwa unaenda safari ukikutana na 'shoga' njiani wakati wowote wa safari yako...............imekula kwako! na iwapo atakusalimia ndo bora ugeuze tu kabisa