KERO Responded Foleni Mbagala inakera sana, ‘Trafiki’ wapo bize na Daladala tu

KERO Responded Foleni Mbagala inakera sana, ‘Trafiki’ wapo bize na Daladala tu

  • Thread starter Thread starter Anonymous (d74a)
  • Start date Start date
Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Foleni ya kutoka Mbagala Kizuiani kwenda Mbagala Rangi Tatu ni foleni ambayo haina ulazima kama askari wataamua kusimamia.

Unakuta muda askari wapo tu na vyanzo vya foleni wanaviona ila hawana muda navyo, wao wanaelekza nguvu zao kusimamisha Daladala ili kufanya yao huku Wananchi tukiendelea kuteseka kila siku.

Pia, watu wengine wanaochangia uwepo wa foleni ni Machinga, wanapanga vitu hadi barabarani, yaani inakuwa kero kero.

Barabara ya Watembea kwa miguu wamechukua yote na saizi wengine wanashuka hadi kwenye barabara kubwa wanapanga vitu.

Mamlaka zipo zinatazama tu, watembea kwa migu wanakosa pa kupita, magari nayo yanatembea kidogokidogo ili kutokuwajeruhi wafanyabiashara.

Imekuwa kero kubwa sana hii, tutaendelea na hali hii hadi lini?

Pia soma ~ Mbagala (Dar): Baadhi ya maeneo ya barabara yaliyokuwa yanazibwa na 'machinga' yaanza kuwa wazi
 
Na hapo bado CFS hii iliyojengwa hapa Jeshini haijaanza kazi tutapata kukatisha toka Mbagala kipati mpaka Rangi 3 ni masaa 4 na zaidi. Mungu tuhurumie sisi watawaliwa.
 
Ili foleni isiwepo inabidi Mgambo waondoe wote wanaofanya biashara kando ya barabara
 
Dsm ndo maana panachosha, hizo Foleni, nakerekwa mie. Lol
 
Na hapo bado CFS hii iliyojengwa hapa Jeshini haijaanza kazi tutapata kukatisha toka Mbagala kipati mpaka Rangi 3 ni masaa 4 na zaidi. Mungu tuhurumie sisi watawaliwa.
Uongozi ukibadirika tuandamane Hilo jengo lisiwepo hapo, hii itakuwa balaa kubwa. lilipojengwa Mimi nilidhani shopping Mall,nilichoka kuambiwa ni bandari sehemu ilistahili iwe ya watu kupumzika Park hiyo.
 
Uongozi ukibadirika tuandamane Hilo jengo lisiwepo hapo, hii itakuwa balaa kubwa. lilipojengwa Mimi nilidhani shopping Mall,nilichoka kuambiwa ni bandari sehemu ilistahili iwe ya watu kupumzika Park hiyo.
Ni uwanja wa jeshi ule ndugu yangu, waliupataje mimi na wewe hatujui kikubwa tujiandae na msongamano zaidi.
 
Dsm ndo maana panachosha, hizo Foleni, nakerekwa mie. Lol
Kuna saa unajiuliza je!? viongozo wetu hawapo? Je mawazo yao yameshindwa kutafuta ufumbuzi wa foleni mjini? kwanini hatuwezi kuamua kama Nchi kutafuta suluhu ya kurekebisha miji yetu? Ni maswali zaidi ya moja au mawili na zaidi na yasiyo na majibu kamili zaidi ya kuwashukuru Trafiki kusimamia uongozwaji wa magari ktk msongamano huu.
 
CCM haijawahi kuwa serious na MATATIZO yetu, rejea changamoto ya Usafiri wa pantoni feri to Kigamboni..yaani baada ya zaidi ya miaka 40 ndio wamekuja na suluhu..tena baada ya kuishirikisha sekta binafsi( Bakheresa) na viboti vyake..tutasubiri sana
 
Kuna saa unajiuliza je!? viongozo wetu hawapo? Je mawazo yao yameshindwa kutafuta ufumbuzi wa foleni mjini? kwanini hatuwezi kuamua kama Nchi kutafuta suluhu ya kurekebisha miji yetu? Ni maswali zaidi ya moja au mawili na zaidi na yasiyo na majibu kamili zaidi ya kuwashukuru Trafiki kusimamia uongozwaji wa magari ktk msongamano huu.
Sasa tutafanyajee??
 
Foleni ya kutoka Mbagala Kizuiani kwenda Mbagala Rangi Tatu ni foleni ambayo haina ulazima kama askari wataamua kusimamia.

Unakuta muda askari wapo tu na vyanzo vya foleni wanaviona ila hawana muda navyo, wao wanaelekza nguvu zao kusimamisha Daladala ili kufanya yao huku Wananchi tukiendelea kuteseka kila siku.

Pia, watu wengine wanaochangia uwepo wa foleni ni Machinga, wanapanga vitu hadi barabarani, yaani inakuwa kero kero.

Barabara ya Watembea kwa miguu wamechukua yote na saizi wengine wanashuka hadi kwenye barabara kubwa wanapanga vitu.

Mamlaka zipo zinatazama tu, watembea kwa migu wanakosa pa kupita, magari nayo yanatembea kidogokidogo ili kutokuwajeruhi wafanyabiashara.

Imekuwa kero kubwa sana hii, tutaendelea na hali hii hadi lini?
Hii Nchi hakuna Viongozi, kuna madalali tu. Rais alikua JK Nyerere na JPM tu
 
Back
Top Bottom