Foleni Kimara Inatisha.

Foleni Kimara Inatisha.

yaani nimepanda gari kimara mwisho nimemaliza saa 1 mpaka ss hata tanesco sjafika!!

Hahahah...pole Tina, maana naona muda ulioandika hii post ni kama saa 6 mchana....ndio kwetu huko jirani.
Ngoja watutengeneze BRT's mbona watatukoma....
 
Ndio mambo ya mvua hayo, dawa ni kuwahi kuamka haina ujanja.
Mimi naishi Mbezi ila nimefika mjini saa 7:00 kwa kuwa nilitoka mapema zaidi huko.
Kwa hiyo utafanyeje wakati wa kurudu? kuna jamaa yangu kaganda hapo jirani na Ubungo mataa, toka saa sita hadi muda huu hajatembea hata sentimeta moja
 
Kwa hiyo utafanyeje wakati wa kurudi? kuna jamaa yangu kaganda hapo jirani na Ubungo mataa, toka saa sita hadi muda huu hajatembea hata sentimeta moja

Kurudi sio shida kaka mkubwa...
Kuna njia ya Makongo Juu - Goba - Mbezi, au kuna Kinyerezi - Mbezi
 
Toka HUKO kaa manzese ni pazuri sanaaa,

kuna upumbavu pale ubungo terminal inatumika njia moja tu.. wakati ya pili imefungwa bila kuwa na kazi



Mimi nimetoka saa kumi na mbili na nusu nimefika saa 4, ile kua njia moja inakua tatizo trafic wanajitahidi mahali pale ila toka jana panawasumbua Strabarg, DART waangalie namna ya kupunguza tatizo lile watafute alternative solution
 
Wewe una undugu na rais wangu eeh? Kwa hiyo ukijiajiri ndo unalala hadi saa sita? Ngoja nisiseme sana...-don mangi njoo bwana
Acha uzembe wa kufikiri unazani wote wanawahi akuna aliejiajiri.
 
Back
Top Bottom