Sasa ni saa11:30 alfajiri na tayari foleni kama kawaida TAZARA. Tatizo kubwa ni junction. Kinachotokea licha ya kutokuwepo kwa flyovers ni magari yasiyohusika kukaa kwenye foleni. Traffic control management haijaangaliwa vizuri. Nitatoa mfano. Mtu anaetoka Tabata kwenda Posta anaweza kupita barabara ya Mandela kupitia Buguruni(Uhuru road na au Nyerere road,achana na ile ya Tabata dampo-Kigogo)
Sasa akifika tu Matumbi anakutana na foleni, ambapo kama anataka kupitia njia ya Uhuru atasubiri sawa na yule anaetaka kupitia Njia ya Nyerere. Kumbe ingewezekana kabisa kwa huyu ambae haendi Through yaani Weaving/diverging angetumia service road na kupita pale Sheli ya Buguruni na akaenda zake. Kwa anaekumbuka vema, ilikua ukitoka Buguruni kwenda Tabata, hadi ufike Tabata junction ilikua kazi kubwa. Lakini tangu ruhusa ya kutumia service road kuanzia matumbi kwenda Tabata, foleni haipo kabisa. Jambo la kuzingatia hapa ni Kuboresha tabaka la lami kwa maeneo ambayo service road inatumika kama diverging road, na kamwe mtu anaenyoosha asiruhusiwe kupita kwenye service road, nakuambia itapubgyza foleni sana kama ilivyotokea Junction ya Tabata ukitokea Buguruni. Folen nyingi ni za kujitakia kabisa. Hakuna ulazima mtu atokae Temeke kwenda Gongo la Mboto kukaa muda mrefu wakati service road kuanzia Vetenary iko empty, ingeandaliwa namna bora tu kama ilivyofanyika pale Tabata, lakini iwe strictly tu kwa wale wanaoenda kushoto. Anaenyoosha akikamatwa apewe adhabu kali. Pale Tabata imeonyesha mafanikio makubwa!