Igwachanya
Senior Member
- Oct 19, 2010
- 142
- 70
Duniani kote, hususan kwa wenzetu waliotutangulia kiuchumi na kwenye magari mengi, usafiri wa treni ndio ulioonyesha matokeo chanya. Matumizi ya usafiri wa treni unapunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya usafiri binafsi. Sio kwamba watu wanapenda kutumia gharama kubwa ya kuendesha magari yao binafsi bali usafiri tulionao wa daladala hauna staha, ni wa kero na kuibiwa juu na vibaka.
Binafsi, tatizo la foleni kwa mapana yake halitokani na polisi bali miundombinu yetu imezidiwa. Ukienda Posta ama Kariakoo ukiwa na gari binafsi tatizo lingine utakalokumbana nalo ni sehemu ya parking. Hivyo, tukijenga flyovers, say, Tazara, Chang'ombe, Ubungo, nk tutasaidia flow ya magari kuwa kubwa. Swali ni je, huko yanakoelekea kumeandaliwa kupokea magari kwa wingi?
Nadhani strategy ambayo itasaidia ni kuja na mkakati wa usafiri wa umma ambao ni bora, utakaovutia hata wenye magari kupaki magari yao majumbani. Jawabu ni usafiri wa treni. Huwa nasikitika mradi wa DART kama tungekuwa tuliamua kujenga reli basi jiji la Dar lingekuwa limepitiwa na reli kila kona kwa kuwa ujenzi wa reli ni gharama ndogo kuliko barabara. Hivyo tngekuwa tumefanikiwa kutatua kero ya foleni kwa kiasi kikubwa, kama si kuimaliza kabisa.
Binafsi, tatizo la foleni kwa mapana yake halitokani na polisi bali miundombinu yetu imezidiwa. Ukienda Posta ama Kariakoo ukiwa na gari binafsi tatizo lingine utakalokumbana nalo ni sehemu ya parking. Hivyo, tukijenga flyovers, say, Tazara, Chang'ombe, Ubungo, nk tutasaidia flow ya magari kuwa kubwa. Swali ni je, huko yanakoelekea kumeandaliwa kupokea magari kwa wingi?
Nadhani strategy ambayo itasaidia ni kuja na mkakati wa usafiri wa umma ambao ni bora, utakaovutia hata wenye magari kupaki magari yao majumbani. Jawabu ni usafiri wa treni. Huwa nasikitika mradi wa DART kama tungekuwa tuliamua kujenga reli basi jiji la Dar lingekuwa limepitiwa na reli kila kona kwa kuwa ujenzi wa reli ni gharama ndogo kuliko barabara. Hivyo tngekuwa tumefanikiwa kutatua kero ya foleni kwa kiasi kikubwa, kama si kuimaliza kabisa.
Tatizo ni Polisi,kwa nini hawa achii taa zikaongoza magari,Polisi ni binadamu wakati mwingine wanajisahau na kusababisha msongamano mkubwa wa magari,cha kufanya ni kuwezesha traffic lights kuwa programmable ili Traffic Polisi akiona msongamano wa magari umezidi anakwenda kwenye taa za kuongozea na ku set manually enough time ya kuruhusu magari kila upande say robo saa au nusu saa kutegemea ukubwa wa msongamano.
Alternatively waweke barabarani sensors karibu na traffic lights ambazo zitawezesha taa kujirekebisha zenyewe kwa kuruhusu barabara yenye msongamano mkubwa wa magari yapite kwa muda mrefu kuliko kule kwenye msongamano mdogo.