Fly Over 7 kujengwa jijini Dar

Fly Over 7 kujengwa jijini Dar

Kati ya majina haya ni lipi mbarawa atajenga Dar ndani ya miezi 3 au 6? Flyover,interchange,intersection,pedestrian bridge au bridge?
 
Stori zingine ni kama mastori ya town...
Hio ya TAZARA tu toka kipindi cha Mwinyi hadi leo...
 
Jamani tutowe maoni chanya. Narudia: 'Carpooling' ni utaratibu wa kupunguza magari binafsi kwenye njia kuu za kuingia na kutoka CBD.
Chini ya mpango huu, wakati wa peak traffic, asubuhi (kuelekea CBD) na jioni (kutoka CBD), gari ndogo ya binafsi (private car) lazima iwe na watu 5 pamoja na dereva. Hii ni pamoja na zile za umma, ST, SM, DFP, SU kwa barabara kuu zote ie. Morogoro Rd, Pugu Rd, Kilwa Rd, Bagamoyo Rd, nk. Maana yake ikiwa mtu hataki kupakia watu asiowajua kwenye gari yake aendapo kazini asubuhi atawachukua jirani zake waendao mjini siku hiyo au hata kila asubuhi na jioni. Ndivyo wenzetu wavyopunguza foleni. Sio kuwalazimisha wenye vigari vyao kuviacha nyumbani au kwenye parking Kimara ambako hawana usalama wa vyombo vyao. Na wakiwa na mizigo au mgonjwa? Wengine wakitaka kwenda shopping je watabeba vipi mizigo yao, wakodi taxi wakati wanayo magari yao?
 
hebu weka mchanganuo wako vizuri, katika hizi namba (13000x2000) 2000 ni nini na 13' ni nini!?
Nasikia gari dogo ni 1,500/- na watumiaji wanataka ipunguzwe. Na ukiangalia rate ya upitaji magari roughly unaweza kusema ni gari moja kila baada ya dakika 5, na hapo usiku wa manane mpaka alfajiri unaweza kupata gari moja baada ya dakika 7-13.
Ukijumlisha operating costs, depreciation na interest ya pesa inahitaji kama miaka zaidi ya 65 kurejesha billion 270.
Ukisoma bandiko kwa utulivu mpaka mwisho utaelewa but, hiyo 2000 nimeweka maximum price iwe gari kubwa au ndogo NA 13000 ni magari yanayopita kila siku hapo Nyerere Bridge.

Je,
Lingine ambalo hujaelewa?
 
Ukisoma bandiko kwa utulivu mpaka mwisho utaelewa but, hiyo 2000 nimeweka maximum price iwe gari kubwa au ndogo NA 13000 ni magari yanayopita kila siku hapo Nyerere Bridge.
Je,
Lingine ambalo hujaelewa?
Nimekuelewa sasa. Hebu tafakari kama kweli kitu hiki kinawezekana hasa ukitilia maanani kuwa waliolitumia hilo daraja wanadai kukaa dakika zaidi ya tatu kulipia na kupata clearance:
Siku moja ina masaa 24 na kila saa ina dakika 60 (24 x 60 = dakika 1,440). .....twenda sawa
ukichukua magari 13,000 ukagawa kwa 1,440 = magari 9+ kwa dakika.
Je, una uhakika katika lile daraja hata miaka 10 ijayo kunaweza kuwa na flow ya magari tisa kila dakika kwa masaa 24 nonstop!? Kumbuka kuna njia tatu kila upande ...kwenda na kurudi.
Propaganda ziko kote duniani ila walioelimika (sio wenye vyeti) ni rahisi kuzielewa hivyo kuziamini au kutoziamini.
 
Ule mradi wa magari yaendayo kasi ungekuwa na mtazamo wa flyover tatizo la msongamano lingekuwa lilisha kwisha. Suluhisho la kudumu la msongamano ni flyover. Uwekezaji wote wa magari ya mwendo kasi haukuwa umefikiriwa vizuri.
 
Hapo zitajengwa mbili, na ya pili itajengwa mwaka 2025 wakati Magu akitaka kuachia ngazi

Pia wakati wa uzinduzi watajaa makada wa CCM na nguo zao kama kawaida, utafikiri wamejenga wao kumbe ni KODI YA WANANCHI kwa ujumla.

Kwani nguo za CCM zinakuuma nini? Hata CHADEMA mngekuwa madarakani hizo gwanda zenu mngezivaa kwenye uzinduzi wa miradi ya serikali yenu
 
Tuwe na uelewa kidogo tutambua kati ya madaraja na barabara za juu ....kinachojengwa Tazara si flyover bali ni bridge........ili iitwe barabara ya juu au flyover ....angalau iwe kuanzia kilomita kumi na kuendelea

Mkuu hata mm nilishahoji kitu ka hcho sehemu...
 
lukondo
Ndugu yangu mtanzania, hebu angalia waziri alivodanganywa hapa....

Naye Mtendaji Mkuu wa Daraja la Nyerere Bw. Gerald Sondo amemueleza Waziri Mbarawa kuwa chanagamoto zinazowakabili kwa sasa ni kubaini magari yenye vibali maalumu, malalamiko ya magari ya abiria (daladala), uelewa mdogo wa matumizi ya daraja na mazoea ya kupita bila ya kulipa tozo.

Zaidi ya magari elfu nane hadi elfu kumi na tatu hupita katika daraja hilo kwa siku huku watembea kwa miguu, baiskeli wakipita bila kulipa tozo.
 
wewe ni mtumwa wa Mwigulu.

swissme
Bora mwigulu kuliko Ngoyai na Ngombale mwiru.. Hao washakunywesha jasho lao kabisaa kila kitu kupinga tu, utakuja umpinge hata bi mkubwa wako kuwa hajakuzaa kisa UKAWA
 
Back
Top Bottom