Jackbauer
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,068
- 2,225
Siku chache baada ya ccm kutangazia wanachama wake ambao wamekua wakitajwa kuhusika na vitendo vya ufisadi kwamba wanatakiwa kujiuzulu nafasi zao za chama katika muda wa siku tisini,kuna habari kwamba mmoja wao amepanga kuihama nchi.
Mwanachama huyo ambaye amewahi kushikilia nafasi kwenye ngazi mbalimbali za chama hicho,amepanga kutoroka nchini ili kuepuka hatua zilizopangwa kuchukuliwa na ccm dhidi yake na wengine wanaotuhumiwa ambazo anahisi zitamzalilisha.
Kada huyo ambaye amesakamwa kwa muda mrefu kuhusika na kashfa mbalimbali za usanyaji wa fedha za kodi za wananchi kiasi cha kusababisha serikali ya rais kikwete kushambuliwa,anaelezwa kuingiwa na hofu kwamba hatua ilipofikia hawezi tena kuendelea kuishi kwa raha humu nchini kutokana na kunyooshewa kidole na watu kila anapopita.kada huyo ambaye ni mfanyabiashara amegundua pia kwamba kwa hali ilivyo hawezi kuendelea kufanya biashara kwa utulivu humu nchini na hivyo kuamua kuchukua uamuzi wa kuhama lakini amepanga kufanya hivyo baada ya kuivuruga ccm na kisha kutimkia nchi ambayo bado anafanya siri kubwa.
Source:gazeti la sauti huru
Mwanachama huyo ambaye amewahi kushikilia nafasi kwenye ngazi mbalimbali za chama hicho,amepanga kutoroka nchini ili kuepuka hatua zilizopangwa kuchukuliwa na ccm dhidi yake na wengine wanaotuhumiwa ambazo anahisi zitamzalilisha.
Kada huyo ambaye amesakamwa kwa muda mrefu kuhusika na kashfa mbalimbali za usanyaji wa fedha za kodi za wananchi kiasi cha kusababisha serikali ya rais kikwete kushambuliwa,anaelezwa kuingiwa na hofu kwamba hatua ilipofikia hawezi tena kuendelea kuishi kwa raha humu nchini kutokana na kunyooshewa kidole na watu kila anapopita.kada huyo ambaye ni mfanyabiashara amegundua pia kwamba kwa hali ilivyo hawezi kuendelea kufanya biashara kwa utulivu humu nchini na hivyo kuamua kuchukua uamuzi wa kuhama lakini amepanga kufanya hivyo baada ya kuivuruga ccm na kisha kutimkia nchi ambayo bado anafanya siri kubwa.
Source:gazeti la sauti huru