Wala cjachanganya mambo... mimi nilichotaja ni yale ambayo nayaona matatizo ya msingi yanayolikabili taifa hili... manung'uniko hayawezi kuwa matatizo ya msingi kv sidhani kama patatokea muundo ambao hautakuwa na manung'uniko. Kusini, kwa maana ya Lindi na Mtwara na Kaskazini kwa maana ya Arusha na Kilimanjaro, zote zipo Tanganyika lakini bado kusini hawajaacha kunung'unika kwamba serikali inaelekeza shughuli za maendeleo kwa upendeleo... manung'uniko ni silika ya mwanadamu, labda jambo la kuangalia ni endapo manung'uniko yenyewe yana msingi na kweli yana athari kwa jamii husika na si tu kwamba ni manung'uniko ya watu wachache wenye sauti lakini kutokana na sauti zao yanabadilika kuwa ni manung'uniko ya wengi ambayo kimsingi athari ama chanzo cha manung'uniko hayo ni ya hao wachache. Mathalani, watu wanaoongoza kwa manung'uniko ni Zanzibar... hususani wafuasi wa CUF. Ni wananchi ndio wananung'unika lakini ukiangalia kwa makini ni manung'uniko yenye maslahi kwa viongozi na wala sio watu wa kawaida unless wawe ni wale wenye mwamko wa utaifa!
Kwamba tatizo la muungano ni manung'uniko ambayo yanasababisha hata kufunika matatizo ya msingi, hapa naomba nisikubaliane na wewe! Sidhani kama mwananchi wa kawaida ana shida sana na muundo wa muungano kuliko kushughulikwa matatizo yake ya msingi. Mimi binafsi, wala sioni kama kuna kitu chochote ninakikosa kwavile tu tupo kwenye mfumo wa serikali mbili lakini kuna mengi nayakosa kwa sababu tu watu hawataki kuwajibika, kuna uzembe kila mahali, kuna ufisadi na wizi wa hovyo n.k.... haya yote wala hayasababishwi na muundo wa muungano otherwise kwenye mataifa ambako suala la muundo si tatizo, haya yasingekuwepo!!!!