Finally leo nimepima UKIMWI

Kichwa Ndio Mtu

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2014
Posts
3,079
Reaction score
1,719
Kama mtakumbuka juzi juzi hapa niliandika hapa kua natakiwa nikapime ukimwi,nimejaribu kukwepa sana hilo jambo ila hatimae nimelazimika leo asubui hii kwenda kupima.

Kweli kupima ukimwi yahitaji moyo,asubui hii nimejipa ujasiri wa kutosha,baada ya kuamka nikaelekea hospitali. Nikiwa nasubiri majibu nimewaza mambo mengi sana kuhusu hatima yangu(je ikitokea ninao ntafanyaje,je ntaoa,je ntapata mtoto, familia yangu watanichukuliaje,wanajamii,nk),nimericall njia zangu za nyuma na jinsi nilivyokua nacheza peku kwenye uwanja wa changarawe kidogo nikimbie majibu.

Thanks majibu yametoka poa,Wajamaa nawashauri mkapime. hapa nilipo najisikia mwepesi sana kama vile nimetua mzigo mzito sana na najisikia nina amani sana moyoni.


cc. Preta
 

maskin kama nakuona umesubiri majib unaangaika mara mkojo mara kuharisha ahaaaa
 
Last edited by a moderator:
hongera sana! kosa ambalo wengi wetu tunafanya ni kuwaona wale ulionao kipindi unapima ni wazima na kwamba hawawezi kukuambukiza!kumbe dawa ni kujikinga kwa uangalifu wa hali ya juu kuanzia muda huo na kuendelea!
 

Hongera sana mkuu......tena juzi kati hapa nilikua nikutafute nikuulize.....vipiii........maswala ya escrow yakawa yamenibana........
sasa basi tulia.......siku ya kesho tar 01 Dec utakuwa umeiadhimisha kifua mbele............

NA WENGINE WOTE........KESHO TWENDENI TUKAPIME........UKIMWI UPO NA UNAUA.........
 

Wanaume vifua mbele wanawake matiti mbele

ila mimi no
 
rudia kupima baada ya siku 90 ukiwa fresh tulizana hongera kwa kujitambua
 

Thanks mkuu,najisikia poa sana sasa.
 
Samahani Wanduguuu,
Unapimaje ? Wanatoa damu na mkojo kama wavyopima kisukari au vipi..wengi tujuzeni!!
 

Umesema ulitakiwa ukapime, vp unaenda polisi nn? Una mchumba watka kuoa? Hebu weka waz hyo sababu inaweza kuwapa nguvu na ujasiri watu wengine.
Kupima? The saints do, I dont.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…