Johnny Sins
JF-Expert Member
- Nov 4, 2019
- 2,536
- 3,885
Ameishi akiwa muuza mwili familia ikamtenga. Alipopata mimba iliyotokana na kazi yake hiyo akaamua kuachana nayo na kutoka kabisa nje ya mji kulea mimba na mwanae ataezaliwa. Akabadilika kimaisha, akaamua kuwa mama, badala ya kahaba.
Siri aliyonayo moyoni waliijua ndugu zake tu, walioishi nae hawakuwahi kumuona akiivujisha siri hiyo sababu hakuionesha hadharani.
Kikundi cha maharamia wanaofanya kazi ya kuteka watoto na kwenda kuwafanyia operesheni na kuwatoa figo na kuziuza, walivamia kijiii alichoishi mama huyu wakachukua watoto waliokuwa wanazagaa kiajabu ajabu. Walipomaliza kuwateka, wakafanya kosa lililowagharimu, waakamchukua na mtoto wa mama huyu, bonge la kosa.
Siri aliyonayo mama huyu ni siri ya familia aliyotoka, ni familia ya wana martial arts. Nyumba nzima wanapiga ngumi mpaka kero. hakuna mtu katika familia yake aliekuwa anaweza kuguswa kizembe, kaka moto, dada moto, mama usiseme, baba ndo mwalimu. Ni nyumba ya mashujaa haswa.
Maharamia wateka nyara wana kauli yao wanasema "ukitufata ukatupata utakuwa umefika sehemu isiyo sahihi" Sababu wanajiamini wana watu.
Mwanamama huyu aliwatafuta akawapata, akawaambia "mmemchukua mtoto asie sahihi"
#Kwa wapenda ngumi tu#.
#One of da best thriller martial arts movie#