Figisufigisu Ligi Kuu:Mtihani mgumu kwa Waziri Mwakyembe

kkarumekenge

JF-Expert Member
Aug 14, 2013
1,708
1,026
Ligi Kuu Soka Tanzania inafikia ukingoni. Inachezwa pote, baa, magazetini, tv,sokoni, viwanjani nk. Uamuzi wa kamati ya saa 72 umezua jambo na natabiri utamu wote wa ligi hii pamoja na makandokando yake umeishia hapo. Je, ni kweli Simba hawakustahili pointi tatu? Je, ni kweli mchezo wake na Kagera haukuwa na kumbukumbu zozote? Je, Yanga na Africa Ryon kulikuwa na malalamiko, ya timu gani naje, hayakusikilizwa? Je, Mwesigwa (Katibu Mkuu wa Yanga zamani) na Malinzi ambaye pia aliwahi kuwa kiongozi/mfadhili wa Yanga hawatakuwa na mkono katika hili ukizingatia pia kwamba wote wanatoka mkoa wa Kagera nk, nk. Haya, kama malalamiko ya Yanga yatajadiliwa sasa, je, yale ya ndugu zangu Ndanda dhidi ya Simba nayo yapitiwe? TFF ni kimeo na imeharibu ligi. Karibu Mwakyembe.
 
Mwakyembe anajua Shilawadu tu na utekaji mpira ndo ilitakiwa aweke nguvu nyingi na uangalizi ila kasahau kama ni wizara yake
 
ukisikia disco kaingia mmasai ndio hivi sasa...mtu amezoea kukamua maziwa leo unamlazimisha kuingia disco na kukata mauno......ataelewa lkn itachukua muda
 
Sijaelewa, naomba mnifahamishe, hivi zile point tatu walizopewa simba dhidi ya kagera sugar wamenyang'anywa tena ama imekuwaje?
 
"usipotembea utabebwa mgongoni" Mbumbumbu FC wameshindwa kutembea/kucheza mpira uwanjani sasa wameamua kubebwa/kuchezea mpira kwenye meza kupitia TFF.
 
yule mchezaji wa Kagera sugar Fakhi ana kadi 3 za njano.
Kadi mbili alizipata kwenye VPL na kadi moja aliipata kwenye FA, kamati ya masaa 72 imelikoroga kwa kutumia kadi hizo 3 za mashindano tofauti kutoa uamuzi.
 
6f6a45f602134277243ae50d9ddc743c.jpg
Picha inaongea
 
kumbe sikuhizi waziri ana mamlaka pia ya urais wa tff!!!!
unamkaribisha afanye nin ndan ya tff????
 
yule mchezaji wa Kagera sugar Fakhi ana kadi 3 za njano.
Kadi mbili alizipata kwenye VPL na kadi moja aliipata kwenye FA, kamati ya masaa 72 imelikoroga kwa kutumia kadi hizo 3 za mashindano tofauti kutoa uamuzi.
Inaaply kote kwa sababu ni mashindano yaliyo chini ya TFF fwatilia vizuri
 
Mwakyembe sheria aliyosoma hadi ngazi ya PhD haijui sasa mpira ambao hakusoma wala hana mapenzi nao ndio ataweza? Hiyo wizara ni kama haina Waziri!!!
 
Back
Top Bottom