FIFA: Zanzibar sio nchi

Tindikali

JF-Expert Member
Mar 26, 2010
2,070
2,806


Kuna huu ujumbe mzito ulienda Zurich, Uswisi, kuiombea ZFF uanachama wa FIFA ukiongozwa na Naibu Waziri Kiongozi wa wakati huo Juma Shamhuna, Naibu Waziri wa Michezo Joel Bendera na wengineo kutoka TFF na ZFF.

FIFA iliporudisha majibu faili likafichwa, wakakaa kimya kirefu kumbe wamepigwa chini. Imefahamika Bungeni leo kwa taarifa ya Nape Nnauye, Waziri wa Michezo alipolazimika kujibu swali la Mbunge wa Zanzibar, Hafidh Tahir.

Sababu zilizotolewa: FIFA imesema, kwa mujibu wa ibara ya 10 ya katiba ya FIFA, ZFF haiwezi kupata uanachama kwa vile Zanzibar hapa duniani sio nchi!

Je, Muungano unawazuia Zanzibar kupata misaada ya FIFA kama ilivyokuwa kwa OIC na hivyo kushindwa kuwa "Singapore"?

NB: Nimeongezea video ya Bunge hapo juu kwa vile mchangiaji mmoja amenishambulia kwamba nimeandika uongo kwa umma.
 
National prestige bado inawasumbua waafrica wa Zanzibar iwe nchi, kisiwa kilichokuwa part of tangannyika ila waarabu/ukoloni wakakitenganisha kwa maslahi yao! Huwezi toka Oman ukaja mbali kote huku eti ni sehemu ya Oman, rubbish!
Mkuu CHUA " jibu hoja ? usiingize ya waKoloni hapa... Maombi yalienda kwa radhaa na baraka ya nani?
Tindikali hapa kuna wanaokurupuka !!
 
Mkuu CHUA " jibu hoja ? usiingize ya waKoloni hapa... Maombi yalienda kwa radhaa na baraka ya nani?
Tindikali hapa kuna wanaokurupuka !!
Ridhaa ya serikali may be ya Muungano, lakini sidhani kama mtu sensible anaweza kujiingiza kwenye aibu ya kuvunja katiba wazi wazi. Ni kutojua au ni makusudi kutingisha kiberiti kuwa wakipitiwa tumeula!
 
Zanzibar ni nchi ilio na internal sovereighnty . Ktk muungn zanzibar imepoteza external sovereighnty.
Nahis wanacho fanya fifa ni ukoloni mamboleo na kutaka kutugombanisha wa Tanzania.
Scotland ni sw sw na zanziba mbn wao wamewakubl na kuwa wanachama wa fifa?
Scotland ipo ktk muungano na england na tulichopoteza sisi ktk muungn ndicho walichopoteza scotland sasa kwann wao wakubaliwe sisi tusikubaliwe ? Au kwa kuwa sisi ni waafrika?
 
Kumbe ule wimbo wao wa taifa na bendera ni kazi bure? Kumbe ni kwa vile wana desturi tuu zinazo tofautiana na bara?
Ngoja nasi wa Lushoto tumuombe mshana jr atutungie wimbo wetu wa mahadhi ya mdumange maana Lushoto kuna desturi na mazingira yaliyo tofauti na maeneo mengine ya Tanganyika ili kulinda fahari yetu.
Elli, MANI na zumbemkuu mnahusika
 
Kumbe ule wimbo wao wa taifa na bendera ni kazi bure? Kumbe ni kwa vile wana desturi tuu zinazo tofautiana na bara?
Ngoja nasi wa Lushoto tumuombe mshana jr atutungie wimbo wetu wa mahadhi ya mdumange maana Lushoto kuna desturi na mazingira yaliyo tofauti na maeneo mengine ya Tanganyika ili kulinda fahari yetu.
Elli, MANI na zumbemkuu mnahusika
Hahahahahahhaha Mpwa hao ndio akili zao zimefikia mwisho
 
Kuna huu ujumbe mzito ulienda Zurich, Uswisi, kuiombea ZFF uanachama wa FIFA ukiongozwa na Naibu Waziri Kiongozi wa wakati huo Juma Shamhuna, Naibu Waziri wa Michezo Joel Bendera na wengineo kutoka TFF na ZFF.

FIFA iliporudisha majibu faili likafichwa, wakakaa kimya kirefu kumbe wamepigwa chini. Imefahamika Bungeni leo kwa taarifa ya Nape Nnauye, Waziri wa Michezo alipolazimika kujibu swali la Mbunge wa Zanzibar, Hafidh Tahir.

Sababu zilizotolewa: FIFA imesema, kwa mujibu wa ibara ya 10 ya katiba ya FIFA, ZFF haiwezi kupata uanachama kwa vile Zanzibar hapa duniani sio nchi!

Je, Muungano unawazuia Zanzibar kupata misaada ya FIFA kama ilivyokuwa kwa OIC na hivyo kushindwa kuwa "Singapore"?
Usipotoshe umma, hivi mnapata wapi ari ya kudanganya tu. Suala likuwa Zanzibar inihoji FIIFA njia zilizotumiwa na TFF kupata usajili wa FIFA hazikuwa sahihi. Tanzania ni muunganoi wa nchi mbili, hivyo haipaswi chama cha mpira wa mshirika mmoja kuchukua mamalaka ya kumsemea mshirika mwengine,

FIFA haijasema kama Zanzibar sio nchi, na si wa pumbavu wa kusema hivyo. Nakufahamisha kilichotokea kwa faida yako na watu wenye akili zinazolingana wewe. Hivyo ndivyo Zanzibar ilivyoituhumu TFF kuvaa koti la muungano walipokwenda kuomba uanachama. Jambo hili ndio lilounda jopo kwenda Zurich ili wapate ufumbuzi, FIFA ilieleza wazi kuwa si Tanganyika wala Zanzibar kama washirika wa muungano ambayo ana haki ya kupata uanachama wa FIFA. Hivyo FIFA waliitaka TFF na ZFF kukaa pamoja na kuwafikiana na wapeleke chombo kinachokubaliwa na pande hizo mbili.Taarifa ime sema si Tanganyika wala Zanzibar itakayokubaliwa kuwa mwana chama wa kujitegemea.Tanganyika na Zanzibar hazitakuwa wanachama wa Fifa na chombo mahsusi kitakachoundwa ndio kitasimamia michezo

Uamuzi huu TFF hawakuupenda na matokeo yake kufichwa mpaka yalipotokea mabadiliko ya mfumo wa uongozi Zanzibar, na cheo cha Naibu Waziri Kiongozi kufutwa na Shamhuna kupoteza madaraka hayo. Hayo ndio yaliojiri. na hata hivyo hilio halijafa na ulipokuja mchakato wa katiba nawazanzibari kuunga mkono uwepo wa serikali tatu, hilo litajadiliwa .
 
Nimefurahi na Jibu la Nape
Maaana CUF kila siku tukisema kua huu muungano una matatizo hawataki na wanatutukana tukiwaambia kua tunataka Zanzibar yenye mamlaka kamili walikua wakitutukana sasa leo sijui wanasemaje
Ukweli kua zanzibar haiwezi kua mwanachama mpaka tuwe na mamlaka kamili
 
National prestige bado inawasumbua waafrica wa Zanzibar iwe nchi, kisiwa kilichokuwa part of tangannyika ila waarabu/ukoloni wakakitenganisha kwa maslahi yao! Huwezi toka Oman ukaja mbali kote huku eti ni sehemu ya Oman, rubbish!
Ubali wa America na Hawaii vipi?
 
National prestige bado inawasumbua waafrica wa Zanzibar iwe nchi, kisiwa kilichokuwa part of tangannyika ila waarabu/ukoloni wakakitenganisha kwa maslahi yao! Huwezi toka Oman ukaja mbali kote huku eti ni sehemu ya Oman, rubbish!

unakijua ulichokiandika? hiv tanganyika imekuwepo toka lin? na je uanzishwaji wa tanganyika ulijumuisha zanzibar?
 
Back
Top Bottom